1 Wafalme 11
1 Mbali na binti Farao, Mfalme Sulemani aliwapenda wanawake wengi wa kigeni: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
2 Walitoka katika mataifa ambayo Mwenyezi Mungu aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Sulemani akakaza kuwapenda.
3 Alikuwa na wake mia saba, binti za uzao wa kifalme, na masuria mia tatu; nao wake zake wakampotosha.
4 Kadiri Sulemani alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitoa kikamilifu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
5 Sulemani akafuata Ashtorethi, mungu wa kike wa Wasidoni, na Moleki mungu wa Waamoni, aliyekuwa chukizo.
6 Kwa hiyo Sulemani akafanya uovu machoni pa Mwenyezi Mungu; hakumfuata Mwenyezi Mungu kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
7 Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Sulemani alijenga mahali pa juu pa kuabudia Kemoshi mungu wa Wamoabu, aliyekuwa chukizo, na pa kuabudia Moleki mungu wa Waamoni, aliyekuwa chukizo.
8 Akafanya vivyo hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
9 Mwenyezi Mungu akamkasirikia Sulemani kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, aliyekuwa amemtokea mara mbili.
10 Ingawa alikuwa amemkataza Sulemani kufuata miungu mingine, Sulemani hakutii amri ya Mwenyezi Mungu.
11 Kwa hiyo Mwenyezi Mungu akamwambia Sulemani, “Kwa kuwa huu ndio msimamo wako, na hukushika agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitakunyang’anya ufalme na kumpa mmoja wa walio chini yako.
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
13 Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
14 Kisha Mwenyezi Mungu akamwinua adui dhidi ya Sulemani, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
15 Hapo awali Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa ameenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote katika Edomu.
16 Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, hadi walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
17 Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Edomu waliokuwa wamemhudumia baba yake.
18 Wakatoka Midiani wakaenda hadi Parani. Wakawachukua watu kutoka Parani, wakaenda nao Misri kwa Farao, mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba na shamba, na pia chakula.
19 Farao akapendezwa sana na Hadadi, hata akampa dada ya mkewe, Malkia Tapenesi, awe mke wake.
20 Huyo dada yake Tapenesi akamzalia Hadadi mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko, Genubathi akaishi pamoja na watoto wa Farao.
21 Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amelala na baba zake, na kwamba Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi pia amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili nirudi nchi yangu.”
22 Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
23 Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Sulemani, Rezoni mwana wa Eliada, aliyekuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
24 Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walienda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
25 Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Sulemani, kuongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na akawa mkatili kwa Israeli.
26 Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Sulemani, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
27 Haya ndio maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Sulemani alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
28 Basi Yeroboamu alikuwa mtu mwenye nguvu na hodari; naye Sulemani alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yusufu.
29 Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
30 naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
31 Kisha akamwambia Yeroboamu, “Jichukulie vipande kumi, kwa kuwa hivi ndivyo Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, asemavyo: ‘Tazama, ninaenda kumnyang’anya Sulemani ufalme na kukupa makabila kumi.
32 Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
33 Nitafanya haya kwa sababu wameniacha na kuabudu Ashtorethi mungu wa kike wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakuenda katika njia zangu wala kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Sulemani, alivyofanya.
34 “ ‘Lakini sitauondoa ufalme wote mkononi mwa Sulemani; nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
35 Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
36 Nitampa mwanawe kabila moja ili Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
37 Lakini wewe, Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala yale yote moyo wako unayotamani; utakuwa mfalme wa Israeli.
38 Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kushika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
39 Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya haya, lakini siyo milele.’ ”
40 Sulemani akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko hadi Sulemani alipofariki.
41 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Sulemani, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionesha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za Sulemani?
42 Sulemani alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
43 Kisha Sulemani akalala na baba zake, akazikwa katika mji wa Daudi, baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Перекрёстные ссылки
258
- 1Deu 17:17, Pro 6:24, Pro 2:16, Pro 7:5, Neh 13:23–27, 1Ki 11:8, Pro 5:8–20, 1Ki 3:1
- 2Exo 34:16, Deu 7:3–4, Jos 23:12–13, Exo 23:32–33, 2Co 6:14–16, 1Co 15:33, Num 25:1–3, Rom 12:9
- 3Ecc 7:28, 2Sa 5:13–16, Jdg 8:30–31, 2Ch 11:21, Jdg 9:5, 2Sa 3:2–5
- 41Ki 9:4, 1Ki 8:61, 1Ch 28:9, 1Ki 11:6, 2Ch 17:3, 2Ch 34:2, 1Ki 11:2, Deu 17:17
- 5Jdg 2:13, 1Ki 11:7, 1Ki 11:33, 2Ki 23:13, Jdg 10:6, 1Sa 7:3–4, Lev 20:2–5, Zep 1:5
- 6Num 14:24, Jos 14:14, Jos 14:8
- 7Num 21:29, Jdg 11:24, Act 7:43, Dan 12:11, 2Ki 21:2–3, Num 33:52, Ezk 20:28–29, Psa 78:58
- 81Ki 11:1, Ezk 16:22–29, 1Co 10:20–22, Hos 4:11–12, 1Co 10:11–12
- 91Ki 3:5, 1Ki 9:2, Deu 7:4, Exo 4:14, Deu 3:26, Deu 9:8, 2Sa 6:7, Num 12:9
- 101Ki 6:12–13, 2Ch 7:17–22, 1Ki 9:4–7
- 111Ki 12:15–16, 1Ki 11:31, 1Ki 12:20, 2Ki 17:21, Isa 29:13–14, Num 14:35, 2Sa 12:9–12, Num 14:23
- 122Ki 20:17, Gen 19:29, 2Ki 20:19, Exo 20:5, 2Ki 22:19–20, 1Ki 21:29, 1Sa 9:4–5, Gen 12:2
- 131Ki 12:20, Deu 12:11, 1Ki 11:32, Psa 132:13–14, Luk 1:32–33, Deu 12:5, Isa 62:7, Jer 33:15–26
- 141Ch 5:26, Isa 10:26, 1Ki 12:15, 2Sa 24:1, 1Sa 26:19, Isa 10:5, Psa 89:30–34, Isa 13:17
- 152Sa 8:14, 1Ch 18:12–13, Deu 20:13, Gen 25:23, Gen 27:40, Num 24:18–19, Psa 108:10, Mal 1:2–3
- 17Mat 2:13–14, Exo 2:1–10, 2Sa 4:4, 2Ki 11:2
- 18Num 10:12, Deu 33:2, Deu 1:1, Gen 21:21, Gen 14:6, Gen 25:2, Num 22:4, Gen 25:4
- 19Gen 39:21, Act 7:10, Gen 39:4, Jer 43:7–9, Act 7:21, Gen 41:45
- 201Sa 1:24, Gen 21:7
- 211Ki 2:10, Gen 45:24, 1Sa 9:26, Exo 4:19, 1Ki 2:34, Jos 2:21, 2Sa 3:21, Mat 2:20
- 22Luk 22:35, 2Sa 18:22–23, Psa 37:8, Mrk 14:31, Jer 2:31
- 232Sa 8:3, 1Ki 11:14, 2Sa 10:8, Ezr 1:1, 2Sa 16:11, 1Ch 18:3–9, 1Ch 19:16–19, Isa 45:5
- 242Sa 10:18, 2Sa 10:8, Act 9:2, 1Ki 20:34, Gen 14:15, 1Ki 19:15
- 25Gen 34:30, Zec 11:8, Psa 106:40, 1Ki 5:4, 2Ch 15:2, 2Sa 16:21, Deu 23:7
- 261Ki 12:2, 2Ch 13:6, 1Ki 11:28, Rut 1:2, 2Sa 20:21, 1Sa 1:1, 1Ki 11:11, 1Ch 2:19
- 271Ki 9:24, 1Ki 9:15, Psa 60:2, Isa 22:9, Amo 9:11, Isa 26:11, Pro 30:32, 2Sa 5:7
- 28Pro 22:29, Isa 14:25, 1Ki 5:16, Zec 10:6, Jdg 1:22–23, 2Sa 19:20, Amo 5:6, Jos 18:5
- 292Ch 9:29, 1Ki 12:15, 1Ki 14:2, Jos 18:1, 2Sa 14:6, Gen 4:8
- 301Sa 15:27–28, 1Sa 24:4–5
- 311Ki 11:11–12
- 321Ki 11:13, 1Ki 12:20–21, 1Ki 14:21
- 331Ki 11:5–7, 1Ki 11:9, Hos 4:17, 1Ki 3:14, Jer 2:13, 1Ch 28:9, 2Ch 15:2, 1Ki 9:5–7
- 34Job 11:6, Isa 55:3, 1Ki 11:12–13, Hab 3:2, 1Ki 11:31, Psa 103:10
- 351Ki 12:15–17, Exo 20:5–6, 1Ki 12:20, 2Ch 10:15–17, 1Ki 11:12
- 361Ki 15:4, 1Ki 11:13, 2Ki 8:19, 2Ch 21:7, 2Sa 21:17, Psa 132:17, 2Sa 7:29, Amo 9:11–12
- 37Deu 14:26, 2Sa 3:21, 1Ki 11:26
- 382Sa 7:11, Jos 1:5, Deu 31:8, 1Ki 14:7–14, Zec 3:7, 1Ki 9:4–5, 1Ki 3:14, 2Sa 7:16
- 39Isa 9:7, Luk 2:11, Isa 11:1–10, Luk 1:32–33, Luk 2:4, 1Ki 11:36, Psa 89:49–51, Jer 23:5–6
- 402Ch 12:2–9, Isa 46:10, 1Ki 14:25–26, Lam 3:37, 2Ch 16:10, Pro 21:30, Isa 14:24–27
- 412Ch 9:29–31
- 421Ki 2:11
- 432Ki 21:18, 1Ki 2:10, Mat 1:7, 1Ki 15:8, 1Ki 14:31, 2Ch 13:7, 2Ch 28:27, 1Ki 16:6
Темы в этой главе
66
Ahijah, Ammonites, Anger, Ashtoreth, Backsliders, Canaan, Character, Chemosh, Children, Citizens, Civil Service, Concubinage, Damascus, Disobedience to God, Edomites, Eliadah, Fellowship, Fugitives, Genubath, God, Government, Hadad, Hadadezer, High Places, Hittites, Hospitality, Industry, Instability, Intercession, Israel, Jeroboam, Joab, Judgments, King, Lasciviousness, Light, Millo, Moabites, Molech, Nebat, Obedience, Parables, Paran, Patriotism, Perfection, Pharaoh, Polygamy, Probation, Promotion, Queen, Rehoboam, Rezon, Rulers, Servant, Shilonite, Shishak, Sidon, Solomon, Syria, Tahpenes, Temptation, Wife, Women, Zereda, Zeruah, Zobah