1 Wafalme 12
1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wameenda huko kumfanya mfalme.
2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Sulemani), akarudi kutoka Misri.
3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu; yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
4 “Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
5 Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
6 Kisha Mfalme Rehoboamu akataka ushauri kwa wazee ambao walimtumikia Sulemani baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri niwajibu nini watu hawa?”
7 Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
8 Lakini Rehoboamu akakataa ushauri aliopewa na wazee, na akataka ushauri kwa vijana wa rika lake waliokuwa wakimtumikia.
9 Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu’?”
10 Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Watu hawa walikuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi.’ Wewe waambie, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwapiga mijeledi; mimi nitawapiga kwa nge.’ ”
12 Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Alikataa ushauri alilopewa na wazee,
14 akafuata ushauri wa vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwapiga mijeledi; mimi nitawapiga kwa nge.”
15 Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Mwenyezi Mungu, ili kutimiza neno ambalo Mwenyezi Mungu alikuwa amenena na Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia kwa Ahiya Mshiloni.
16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Je, tuna fungu gani kwa Daudi? Tuna urithi gani kwa mwana wa Yese? Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
17 Lakini kwa habari ya Waisraeli walioishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
18 Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake la vita na kutorokea Yerusalemu.
19 Hivyo, Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
20 Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
21 Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, vijana wenye uwezo elfu mia moja na themanini, ili kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Sulemani.
22 Lakini neno la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani, mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
24 ‘Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’ ” Kwa hiyo wakalitii neno la Mwenyezi Mungu na kurudi nyumbani, kama Mwenyezi Mungu alivyokuwa ameagiza.
25 Kisha Yeroboamu akaimarisha Shekemu, na kuuzungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu, na akaishi huko. Kutoka huko, akaenda akajenga Penueli.
26 Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Kuna uwezekano wa ufalme kurudia nyumba ya Daudi.
27 Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Mwenyezi Mungu huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
28 Baada ya kutafuta ushauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
29 Ndama mmoja akamweka Betheli, na mwingine akamweka Dani.
30 Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
31 Yeroboamu akajenga nyumba za ibada katika mahali pa juu pa kuabudia, na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
32 Pia Yeroboamu akaanzisha sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Haya aliyafanya huko Betheli, akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani katika mahali pa juu pa kuabudia miungu aliyotengeneza.
33 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaanzisha sikukuu kwa ajili ya Waisraeli, na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.
Перекрёстные ссылки
213
- 12Ch 10:1–19, Jdg 9:6, Gen 33:18–19, Jos 24:1, Gen 12:6, Jdg 9:1, Jos 20:7, Psa 60:6
- 21Ki 11:40, 2Ch 10:2–3, 1Ki 11:26–31
- 41Sa 8:11–18, 1Ki 4:7, Mat 11:29–30, 2Ch 10:4–5, Mat 23:4, 1Ki 4:20–25, 1Jn 5:3, 1Ki 9:22–23
- 51Ki 12:12
- 6Job 32:7, Job 12:12, Pro 27:10, Jer 42:2–5, Jer 43:2, 1Ki 4:2, 2Sa 16:20, 2Sa 17:5
- 7Pro 15:1, 2Sa 15:3–6, Ecc 10:4, Php 2:7–11, 1Ki 12:13, Mrk 10:43–44, Zec 1:13, 2Ch 10:6–7
- 8Pro 19:20, Pro 1:30, Pro 1:2–5, Pro 1:25, 2Ch 10:8, 2Ch 25:15–16, Ecc 10:2–3, Pro 25:12
- 92Ch 18:5–7, 1Ki 22:6–8, 2Ch 10:9, 2Sa 17:5–6
- 102Ch 10:10–11, Pro 10:14, Pro 29:23, Pro 18:6–7, Pro 28:25, Isa 47:6, 2Sa 17:7–13
- 11Isa 58:6, 1Ki 12:14, Jer 28:13–14, Ezk 2:6, Exo 1:13–14, 1Sa 8:18, Exo 5:5–9, Exo 5:18
- 121Ki 12:5, 2Ch 10:12–14
- 13Jas 3:17, Ecc 10:12, Pro 10:11, Pro 13:20, Pro 18:23, Pro 10:32, 1Sa 20:30–31, Gen 16:6
- 141Ki 12:10–11, Exo 5:5–9, Exo 5:16–18, Exo 1:14, Est 1:16–21, 2Ch 22:4–5, Pro 13:10, Est 2:2–4
- 152Ch 25:20, 1Ki 12:24, Jdg 14:4, Deu 2:30, 1Ki 11:29–38, 2Ch 10:15, 2Ch 22:7, 1Ki 11:11
- 162Sa 20:1, Jer 33:15–16, 2Ch 10:16, 1Ki 22:36, Jer 33:21, 1Ki 22:17, Jer 23:5–6, 1Ki 11:13
- 171Ki 11:36, 1Ki 11:13, 2Ch 10:17, 2Ch 11:13–17
- 181Ki 4:6, 1Ki 5:14, 2Sa 20:24, Act 7:57–58, Exo 17:4, 2Ch 10:18, Act 5:26, 1Ki 20:18–20
- 192Ki 17:21, 2Ch 10:19, Isa 7:17, 1Sa 10:19, Jos 4:9, Heb 6:6, 2Ch 13:5–7, 2Ch 13:17
- 201Ki 11:13, 1Ki 11:32, 1Ki 11:36, 1Ki 12:17, 1Sa 10:24, Hos 8:4, Hos 11:12
- 212Ch 11:1–3, 2Ch 14:8, 2Ch 17:14–19, Pro 21:30–31, 1Ch 21:5, 2Ch 14:11
- 222Ch 11:2, 1Ti 6:11, Deu 33:1, 2Ch 12:5–7, 2Ki 4:16, 1Ki 17:18, 1Ki 17:24, 1Ki 13:11
- 231Ki 12:17
- 24Num 14:42, 1Ki 12:15, 2Ch 25:7–8, 2Ch 11:4, 1Ki 11:29–38, Hos 8:4, 2Ch 25:10, 2Ch 28:9–15
- 25Jdg 8:17, Jdg 8:8, Gen 32:30–31, Jdg 9:45–49, 1Ki 9:17–18, 1Ki 16:24, Jdg 9:1, 1Ki 9:15
- 262Ch 20:20, Jhn 11:47–50, 1Sa 27:1, 1Ki 11:38, Jhn 12:10–11, Luk 7:39, Psa 14:1, Act 4:16–17
- 27Deu 16:6, Deu 12:5–7, Pro 29:25, Deu 12:14, 1Co 1:19–20, Gen 26:7, 1Ki 11:32, 1Ki 8:44
- 28Exo 32:4, 2Ki 17:16, 2Ki 10:29, Exo 32:8, Hos 8:4–7, 2Ch 11:15, Exo 20:4, Isa 30:10
- 29Gen 28:19, Jdg 18:27–31, Jer 8:16, Amo 8:14, Gen 14:14, Hos 4:15, Gen 35:1, 2Ki 10:29
- 302Ki 17:21, 1Ki 13:34, 2Ki 10:31
- 312Ch 13:9, 1Ki 13:32–33, 2Ki 17:32, Num 3:10, 2Ch 11:14–15, Deu 24:15, Hos 12:11, Ezk 44:6–8
- 32Num 29:12–40, 1Ki 8:5, Amo 7:10–13, 1Ki 8:2, Ezk 43:8, Mat 15:8–9, Lev 23:33–44
- 331Ki 13:1, Num 15:39, 2Ch 26:6, Mat 15:6, 1Sa 13:12, Isa 29:13, Mrk 7:13, Psa 106:39
Параллельные места
1
- The Kingdom Divided1Ki 12:1–19, 2Ch 10:1–19
Темы в этой главе
54
Adoniram, Altar, Benjamin, Beth-El, Bul, Calf, Canaan, Church and State, Citizens, Counsel, Dan, Ephraim, Fellowship, Gezer, God, Government, High Places, Idolatry, Incense, Israel, Israel, Prophecies Concerning, Jeroboam, Judah, King, Minister, Christian, Month, Nebat, Offerings, Oppression, Penuel, Petition, Predestination, Priest, Prudence, Rashness, Rebellion, Rehoboam, Religion, Revolt, Rulers, Scorpion, Scourging, Shechem, Shemaiah, Shilonite, Solomon, Statecraft, Tabernacles, Feast of, Tax, Temple, Tent, Treason, Whip, Young Men