Ayubu 41
1 “Je, unaweza kumvua Lewiathani kwa ndoana ya samaki, au kufunga ulimi wake kwa kamba?
2 Unaweza kupitisha kamba puani mwake, au kutoboa taya lake kwa kulabu?
3 Je, ataendelea kukuomba umhurumie? Atasema nawe maneno ya upole?
4 Je, atafanya agano nawe ili umtwae awe mtumishi wako maisha yake yote?
5 Je, utamfuga na kumfanya rafiki kama ndege, au kumfunga kamba kwa ajili ya wasichana wako?
6 Je, wafanyabiashara watabadilishana bidhaa kwa ajili yake? Watamgawanya miongoni mwa wafanyao biashara?
7 Je, unaweza kuijaza ngozi yake kwa vyuma vyenye ncha kali, au kichwa chake kwa mkuki wa kuvulia samaki?
8 Ukiweka mkono wako juu yake, utavikumbuka hivyo vita na kamwe hutarudia tena!
9 Tumaini lolote la kumtiisha ni kujidanganya; kule kumwona tu kunamwangusha mtu chini.
10 Hakuna yeyote aliye mkali athubutuye kumchokoza. Ni nani basi awezaye kusimama dhidi yangu?
11 Ni nani mwenye madai dhidi yangu ili nipate kumlipa? Kila kitu kilicho chini ya mbingu ni mali yangu.
12 “Sitashindwa kunena kuhusu maungo yake, nguvu zake na umbo lake zuri.
13 Ni nani awezaye kumvua gamba lake la nje? Ni nani awezaye kumsogelea na lijamu?
14 Nani athubutuye kuufungua mlango wa kinywa chake, kilichozungukwa na meno yake ya kutisha pande zote?
15 Mgongo wake una safu za ngao zilizoshikamanishwa imara pamoja;
16 kila moja iko karibu sana na mwenzake, wala hakuna hewa iwezayo kupita kati yake.
17 Zimeunganishwa imara kila moja na nyingine; zimeng’ang’aniana pamoja wala haziwezi kutenganishwa.
18 Akipiga chafya mwanga humetameta; macho yake ni kama miali ya mapambazuko.
19 Mienge iwakayo humiminika kutoka kinywani mwake; cheche za moto huruka nje.
20 Moshi hufuka kutoka puani mwake, kama kutoka chungu kinachotokota kwa moto wa matete.
21 Pumzi yake huwasha makaa ya mawe, nayo miali ya moto huruka kutoka kinywani mwake.
22 Nguvu hukaa katika shingo yake; utisho hutangulia mbele yake.
23 Mikunjo ya nyama yake imeshikamana imara pamoja; iko imara na haiwezi kuondolewa.
24 Kifua chake ni kigumu kama mwamba, kigumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 Ainukapo, mashujaa wanaogopa; wanarudi nyuma mbele ya kishindo chake.
26 Upanga unaomfikia haumdhuru, wala mkuki au mshale wala fumo.
27 Chuma hukiona kama unyasi, na shaba kama mti uliooza.
28 Mishale haimfanyi yeye akimbie; mawe ya kombeo kwake ni kama makapi.
29 Rungu kwake huwa kama kipande cha jani kavu; hucheka sauti za kugongana kwa mkuki.
30 Sehemu zake za chini kwenye tumbo zina menomeno na mapengo kama vigae vya chungu, zikiacha mburuzo kwenye matope kama chombo chenye meno cha kupuria.
31 Huvisukasuka vilindi kama sufuria kubwa ichemkayo, na kukoroga bahari kama chungu cha marhamu.
32 Anapopita nyuma yake huacha mkondo unaometameta; mtu angedhani vilindi vilikuwa na mvi.
33 Hakuna chochote duniani kinacholingana naye: yeye ni kiumbe kisicho na woga.
34 Yeye huwatazama chini wale wote wenye kujivuna; yeye ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.”
Referências cruzadas
96
- 1Job 3:8, Psa 74:14, Isa 27:1, Psa 104:26
- 2Isa 37:29, Ezk 29:4–5, Isa 27:1, 2Ki 19:28
- 3Psa 55:21, Isa 30:10, Pro 18:23, Pro 15:1, Pro 25:15
- 4Exo 21:6, Deu 15:17, Gen 1:28, Psa 8:5–6, 1Ki 20:31–34
- 5Jdg 16:25–30, Job 28:11
- 6Jdg 14:11
- 8Luk 14:31–32, 2Ki 10:4, 1Ki 20:11
- 9Isa 28:19, Luk 21:11, 1Sa 3:11, Deu 28:34
- 10Job 9:4, 1Co 10:22, Psa 2:11–12, Job 40:9, Job 3:8, Num 24:9, Jer 12:5, Gen 49:9
- 11Rom 11:35, Psa 24:1, 1Ch 29:11–14, Job 35:7, Deu 10:14, Psa 50:12, Exo 19:5, 1Co 10:26
- 12Gen 1:25
- 13Jas 3:3, Psa 32:9, 2Ki 19:28
- 14Dan 7:7, Psa 58:6, Job 38:10, Ecc 12:4, Psa 57:4, Pro 30:14
- 15Jer 9:23, Rev 5:5, Rev 5:2–3
- 18Job 3:9, Rev 1:14
- 19Psa 18:8
- 20Jer 1:13–14
- 21Psa 18:8, Psa 18:12, Hab 3:5, Isa 30:33
- 22Hos 13:14, Job 39:19, Job 40:16, 1Co 15:55–57
- 24Jer 5:3, Zec 7:12, Isa 48:4
- 25Jon 1:4–6, Psa 107:28
- 26Job 39:21–24
- 28Job 39:7, Hab 1:10
- 292Ch 26:14
- 30Isa 41:15
- 32Job 38:16, Gen 15:15, Gen 42:38, Job 38:30, Job 28:14, Gen 1:15, Gen 1:2, Pro 16:31
- 33Job 40:19
- 34Ezk 29:3, Psa 73:6, Job 28:8, Job 26:12, Psa 73:10, Rev 20:2–3, Exo 5:2, Isa 28:1