Ezekieli 17
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli fumbo.
3 Waambie hivi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Tai mkubwa mwenye mabawa yenye nguvu, yaliyojaa manyoya marefu ya rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni. Akatua kwenye kilele cha mwerezi,
4 akakwanyua ncha yake na kuichukua hadi nchi ya wafanyabiashara, akaipanda huko katika mji wa wachuuzi.
5 “ ‘Akachukua baadhi ya mbegu za nchi yako na kuziweka katika udongo wenye rutuba. Akazipanda kama mti umeao kando ya maji mengi,
6 nazo zikaota na kuwa mzabibu mfupi, unaoeneza matawi yake. Matawi yake yakamwelekea huyo tai, mizizi yake ikabaki chini ya huo mzabibu. Kwa hiyo ukawa mzabibu na kutoa matawi na vitawi vyenye majani mengi.
7 “ ‘Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa yenye nguvu yaliyojaa manyoya. Tazama! Huu mzabibu ukatoa mizizi yake kumwelekea huyo tai kutoka mle kwenye shamba lile ulikopandwa, na kutanda matawi yake kumwelekea ili aunyweshe maji.
8 Ulikuwa umepandwa katika udongo mzuri wenye maji mengi ili uweze kutoa matawi, kuzaa matunda, na uweze kuwa mzabibu mzuri sana.’
9 “Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Je, utastawi? Je, hautang’olewa na kuondolewa matunda yake, ili uweze kunyauka? Majani yake mapya yanayochipua yote yatanyauka. Hautahitaji mkono wenye nguvu au watu wengi kuung’oa na mizizi yake.
10 Hata kama utapandwa pengine, je, utastawi? Je, hautanyauka kabisa wakati upepo wa mashariki utakapoupiga, yaani hautanyauka kabisa katika udongo mzuri ambamo ulikuwa umestawi vizuri?’ ”
11 Ndipo neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
12 “Waambie nyumba hii ya uasi, ‘Je, mnajua hii ina maana gani?’ Waambie: ‘Mfalme wa Babeli alienda Yerusalemu na kumchukua mfalme wake na watu wake maarufu, akawaleta Babeli.
13 Ndipo akamchukua mmoja wa jamaa ya mfalme na kufanya mapatano naye, akamfanya aape. Akawachukua pia viongozi wa nchi,
14 ili kuudhoofisha ufalme huo, usiweze kuinuka tena, ila uweze kuendelea tu chini ya mapatano yake.
15 Lakini mfalme aliasi dhidi yake kwa kutuma wajumbe wake kwenda Misri ili kupatiwa farasi na jeshi kubwa. Je, atashinda? Je, atafanikiwa? Je, mtu afanyaye mambo kama hayo ataokoka? Je, atavunja mapatano na bado aokoke?
16 “ ‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mungu Mwenyezi, atafia huko Babeli, katika nchi ya mfalme aliyemketisha kwenye kiti cha utawala, ambaye alidharau kiapo chake na kuvunja mapatano yake.
17 Farao pamoja na jeshi lake kubwa na watu wake wengi hawataweza kusaidia chochote katika vita, watakapozingirwa na jeshi likitaka kuangamiza watu wengi.
18 Alidharau kiapo kwa kulivunja agano. Kwa sababu aliahidi kwa mkono wake mwenyewe na bado akafanya mambo haya yote, hataokoka.
19 “ ‘Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Hakika kama niishivyo, nitamwadhibu kwa kudharau kiapo changu, na kulivunja agano langu.
20 Nitautandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa katika mtego wangu. Nitamleta Babeli na kutekeleza hukumu juu yake huko kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwangu.
21 Askari wake wote wanaotoroka wataanguka kwa upanga, nao watakaonusurika watatawanyika katika pande zote za dunia. Ndipo utakapojua kuwa Mimi Mwenyezi Mungu nimesema.
22 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Mimi mwenyewe nitachukua chipukizi kutoka kilele cha juu sana cha mwerezi na kukipanda, nitavunja kitawi kichanga kutoka matawi yake ya juu kabisa na kukipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana.
23 Katika vilele vya mlima mrefu wa Israeli nitakipanda, kitatoa matawi na kuzaa matunda na kuwa mwerezi mzuri sana. Ndege wa kila aina watajenga viota vyao ndani yake, nao watapata makazi katika kivuli cha matawi yake.
24 Miti yote ya kondeni itajua kuwa Mimi Mwenyezi Mungu ninaishusha miti mirefu na kuikuza miti mifupi kuwa miti mirefu. Mimi naikausha miti mibichi na kuifanya miti mikavu istawi. “ ‘Mimi Mwenyezi Mungu nimesema, nami nitatenda.’ ”
Referências cruzadas
146
- 2Ezk 20:49, Mat 13:35, Hos 12:10, 1Co 13:12, Jdg 9:8–15, Ezk 24:3, 2Sa 12:1–4, Jdg 14:12–19
- 3Jer 48:40, Hos 8:1, Dan 4:22, Ezk 17:7, Jer 22:23–28, Deu 28:49, Ezk 17:12–21, Dan 2:38
- 4Jer 51:13, Isa 43:14, Rev 18:11–19, Rev 18:3, Isa 47:15
- 5Deu 8:7–9, Isa 44:4, Ezk 17:13, 2Ki 24:17, Isa 15:7, Ezk 19:11–12, Jer 37:1
- 6Ezk 17:14, Pro 16:18–19
- 7Ezk 31:4, Ezk 17:15, 2Ki 24:20, 2Ch 26:13, Jer 37:5–7
- 8Ezk 17:5–6
- 9Ezk 17:10, Jer 32:5, Jer 29:4–7, Jer 21:4–7, Isa 8:9–10, Isa 30:1–7, Num 14:41, Jer 24:8–10
- 10Hos 13:15, Jhn 15:6, Mrk 11:20, Mat 21:19, Hos 12:1, Ezk 19:12–14, Jud 1:12
- 12Ezk 24:19, Ezk 1:2, Ezk 17:3, Jer 22:24–28, Luk 9:45, Ezk 2:8, Isa 1:2, Ezk 2:3–5
- 132Ch 36:13, 2Ki 24:15–17, Ezk 17:5, Jer 5:2, Jer 29:2, Jer 37:1, Jer 24:1
- 14Ezk 29:14, Deu 28:43, 1Sa 2:30, Neh 9:36–37, Jer 27:12–17, Jer 38:17, Lam 5:10, 1Sa 2:7
- 15Jer 52:3, 2Ki 24:20, Jer 34:3, Ezk 17:7, 2Ch 36:13, Jer 38:18, Deu 17:16, Ezk 17:9
- 16Ezk 12:13, Jer 52:11, Jos 9:20, 2Ki 24:17, Ezk 16:59, Psa 15:4, Num 30:2, Exo 8:2
- 17Jer 37:7, Isa 36:6, Ezk 4:2, Ezk 29:6–7, Jer 37:5, Lam 4:17, Jer 52:4, Jer 33:5
- 181Ch 29:24, 2Ch 30:8, Lam 5:6
- 19Jer 5:2, Jer 5:9, Deu 5:11, Ezk 21:23–27, Jer 7:9–15
- 20Ezk 12:13, Ezk 20:35–36, Jer 2:35, Ezk 32:3, Ezk 38:22, Jer 39:5–7, Lam 1:13, Jer 2:9
- 212Ki 25:5, 2Ki 25:11, Ezk 12:14, Ezk 5:12, Amo 9:1, Ezk 6:7, Ezk 15:7, Jer 48:44
- 22Ezk 20:40, Isa 11:1–5, Isa 53:2, Zec 6:12–13, Psa 2:6, Zec 3:8, Psa 72:16, Jer 23:5–6
- 23Mat 13:32, Ezk 31:6, Isa 2:2, Hos 14:7, Jhn 15:5–8, Dan 4:21–23, Psa 22:27–30, Dan 4:10–14
- 24Amo 9:11, 1Co 1:27–28, Luk 1:52–53, Isa 26:5, Ezk 24:14, Ezk 12:25, Psa 75:6–7, 1Sa 2:7–8