Ayubu 6
1 Kisha Ayubu akajibu:
2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au fahali hulia akiwa na chakula?
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 “Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 “Nina nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali yenu,
23 au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 “Nifundisheni, nami nitakaa kimya; nionesheni nilikokosea.
25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 Je, pana uovu wowote mdomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Referencias cruzadas
170
- 1Job 4:1
- 2Job 4:5, Job 31:6, Job 23:2
- 3Pro 27:3, Mat 11:28, Job 37:19–20, Job 23:2, Psa 40:5, Psa 77:4
- 4Psa 38:2, Job 30:15, Psa 88:15–16, Pro 18:14, Psa 143:7, Job 16:12–14, Mrk 15:34, Job 9:17
- 5Psa 104:14, Jer 14:6, Psa 42:1, Jol 1:18–20
- 6Job 34:3, Luk 14:34, Lev 2:13, Job 6:30, Job 12:11, Col 4:6, Job 16:2, Heb 6:4–5
- 7Ezk 4:16, Dan 10:3, Psa 102:9, Job 3:24, Ezk 12:18–19, 1Ki 17:12, Ezk 4:14, 1Ki 22:27
- 8Psa 119:81, Job 17:14–16, Job 6:11–13
- 91Ki 19:4, Jon 4:3, Isa 48:10–13, Jon 4:8, Job 7:15–16, Job 3:20–22, Psa 32:4, Num 11:14–15
- 10Job 23:12, Isa 57:15, Lev 19:2, Psa 71:17–18, Psa 40:9–10, Psa 37:30, 2Pe 2:4–5, Rev 3:7
- 11Psa 103:14–16, Psa 39:5, Psa 102:23, Job 17:1, Job 21:4, Job 7:5–7, Job 13:28, Job 17:14–16
- 12Job 41:24, Job 40:18
- 13Job 26:2, 2Co 1:12, Job 19:28, Job 13:2, Job 12:2–3, Gal 6:4
- 14Pro 17:17, Gal 6:2, 1Co 12:26, Rom 12:15, Heb 13:3, Luk 23:40, 2Co 11:29, Job 16:5
- 15Psa 38:11, Jer 15:18, Psa 41:9, Jhn 16:32, Jhn 13:18, Psa 55:12–14, Mic 7:5–6, Jer 9:4–5
- 171Ki 17:1, Job 24:19
- 19Isa 21:14, Gen 25:15, Jer 25:23, 1Ki 10:1, Gen 10:7, Psa 72:10, Ezk 27:22–23, Gen 25:3
- 20Jer 14:3–4, Rom 5:5, Jer 17:13, Rom 9:33
- 21Psa 38:11, 2Ti 4:16, Jer 17:5–6, Mat 26:56, Rev 18:17–18, Pro 19:7, Mat 26:31, Job 2:11–13
- 22Job 42:11, 1Sa 12:3, Act 20:33
- 23Psa 49:7–8, Psa 107:2, Psa 49:15, Jer 15:21, Job 5:20, Neh 5:8, Lev 25:48
- 24Jas 3:2, Pro 9:9, Job 10:2, Psa 39:1–2, Job 5:27, Psa 32:8, Psa 19:12, Job 33:1
- 25Job 13:5, Pro 16:21–24, Ecc 12:10–11, Pro 12:18, Job 32:3, Pro 25:11, Job 16:3–5, Job 4:4
- 26Job 8:2, Eph 4:14, Mat 12:37, Job 6:4, Job 42:7, Job 10:1, Job 38:2, Job 3:3–26
- 27Psa 7:15, Job 24:9, 2Pe 2:3, Job 24:3, Job 22:9, Nam 3:10, Jas 1:27, Jol 3:3
- 28Job 27:4, Job 33:3, Job 13:4, Job 36:4, Job 11:3
- 29Job 17:10, Mal 3:18, Job 42:6, Job 23:10, Job 27:4–6, Job 34:5
- 30Job 12:11, Job 34:3, Job 6:6, Heb 5:14, Job 33:8–12, Job 42:3–6