Ezekieli 27
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
3 Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
4 Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
5 Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari kutoka Seniri; walichukua mwerezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
6 Walichukua mialoni kutoka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
7 Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Al-Yasa.
8 Wakaaji wa Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, ndio walikuwa mabaharia wako.
9 Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako kwenye meli. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
10 “ ‘Wanaume wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
11 Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
12 “ ‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali yako.
13 “ ‘Uyunani, Tubali na Mesheki walifanya biashara nawe; walibadilisha binadamu na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
14 “ ‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali yako.
15 “ ‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
16 “ ‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
17 “ ‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe; walibadilishana ngano iliyotoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri kwa bidhaa zako.
18 “ ‘Dameski walifanya biashara nawe kwa sababu ya wingi wa bidhaa zako na ukuu wa utajiri wa mali zako, wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
19 “ ‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali walikuletea mali ya biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
20 “ ‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
21 “ ‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako; walifanya biashara nawe ya kubadilishana wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
22 “ ‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezo, vito vya thamani na dhahabu.
23 “ ‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
24 Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
25 “ ‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
26 Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makuu. Lakini upepo wa mashariki utakuvunja vipande vipande moyoni mwa bahari.
27 Utajiri wako, bidhaa zako na mali yako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliye kwenye meli atazama kwenye moyo wa bahari siku ile meli yako itakapovunjika.
28 Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
29 Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
30 Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
31 Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
32 Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
33 Bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
34 Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
35 Wote wanaoishi katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
36 Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’ ”
Referencias cruzadas
218
- 2Jer 9:10, Ezk 28:12, Ezk 19:1, Jer 9:17–20, Ezk 26:17, Ezk 32:2, Jer 7:20, Amo 5:1
- 3Ezk 27:4, Psa 50:2, Ezk 27:10–36, Rev 18:11–15, Ezk 26:17, Isa 23:2–3, Isa 23:8–9, Isa 23:11
- 4Ezk 26:5
- 5Deu 3:9, Sng 4:8, Isa 14:8, Psa 104:16, Psa 92:12, 1Ki 5:6, Psa 29:5, 1Ki 5:1
- 6Gen 10:4, Isa 2:13, Zec 11:2, Jer 2:10, Num 24:24, Num 21:33, Jer 22:20, Isa 23:12
- 7Jer 10:9, Exo 25:4, Isa 19:9, Gen 10:4, 1Ch 1:7, 1Ki 10:28, Pro 7:16
- 8Gen 10:18, 1Ki 9:27, Ezk 27:11, Gen 49:13, Ezk 27:28, Jer 49:23, Jos 11:8, 1Ki 5:6
- 91Ki 5:18, Jos 13:5, Psa 83:7
- 10Ezk 38:5, Ezk 30:5, Isa 66:19, Sng 4:4, Jer 46:9, 1Ch 1:11, Nam 3:9, Dan 5:28
- 11Ezk 27:3–4
- 12Ezk 38:13, Gen 10:4, 1Ki 10:22, Isa 23:10, 2Ch 20:36–37, Ezk 27:16, Isa 23:14, Isa 60:9
- 13Gen 10:2, Isa 66:19, Rev 18:13, Ezk 39:1, 1Ch 1:5, Ezk 32:26, Jol 3:3, Ezk 27:19
- 14Ezk 38:6, Gen 10:3, 1Ch 1:6
- 151Ki 10:22, Rev 18:12, Gen 10:7, Jer 25:23, Ezk 27:20, Jer 49:8, Ezk 25:13, 1Ch 1:32
- 16Jdg 10:6, Ezk 28:13, 2Sa 15:8, Gen 28:5, Gen 10:22, 2Sa 8:5, 2Sa 10:6, Isa 7:1–8
- 17Jdg 11:33, 1Ki 5:9, Deu 8:8, 2Ch 2:10, Gen 43:11, Ezr 3:7, Jer 8:22, Act 12:20
- 18Isa 7:8, Gen 14:15, Ezk 47:16–18, Act 9:2, 1Ki 11:24–25, Gen 15:2
- 19Exo 30:23–24, Jdg 18:29, Psa 45:8, Sng 4:13–14
- 20Gen 25:3, Ezk 27:15
- 21Isa 60:7, Gen 25:13, Jer 25:24, 1Ki 10:15, Isa 21:16, Act 2:11, Sng 1:5, Gal 4:25
- 22Gen 10:7, Isa 60:6, 2Ch 9:1–12, 1Ki 10:1–13, Ezk 38:13, 1Ch 1:9, Gen 43:11, Psa 72:10
- 232Ki 19:12, Isa 37:12, Amo 1:5, Gen 10:22, Gen 10:10, Isa 10:9, Num 24:22, Gen 2:8
- 242Ki 2:8
- 25Isa 2:16, Psa 48:7, Isa 23:14, 1Ki 10:22, Isa 60:9
- 26Psa 48:7, Jer 18:17, Ezk 26:19, Act 27:14, Psa 93:3–4, Rev 17:15, Isa 33:23, Ezk 27:34
- 27Pro 11:4, Ezk 26:12, Ezk 27:7–9, Ezk 26:21, Ezk 27:24, Ezk 26:14, Ezk 27:34, Ezk 27:22
- 28Ezk 26:10, Ezk 31:16, Ezk 26:15–18, Nam 2:3, Ezk 27:35, Exo 15:14
- 29Rev 18:17–24, Ezk 26:16, Ezk 32:10
- 30Jer 6:26, 2Sa 1:2, Lam 2:10, 1Sa 4:12, Jon 3:6, Ezk 26:17, Isa 23:1–6, Mic 1:10
- 31Isa 22:12, Ezk 7:18, Isa 16:9, Isa 15:2, Isa 22:4, Jer 47:5, Jer 16:6, Amo 8:10
- 32Ezk 26:17, Rev 18:18, Ezk 27:2, Lam 1:12, Ezk 27:26, Ezk 26:4–5, Lam 2:13
- 33Rev 18:19, Ezk 28:4–5, Ezk 27:3, Ezk 28:16, Isa 23:3–8, Rev 18:12–15, Ezk 27:12–36, Rev 18:3
- 34Ezk 27:26–27, Zec 9:3–4, Ezk 26:12–15, Ezk 26:19–21
- 35Ezk 32:10, Isa 23:6, Ezk 26:15–18, Rev 18:9–10, Ezk 28:17–19
- 36Jer 18:16, Jer 19:8, Zep 2:15, Ezk 26:21, Psa 37:10, Psa 37:36, Jer 50:13, Ezk 26:2
Temas en este capítulo
79
Agate, Arabia, Arabians, Art, Arvad, Arvadites, Ashurites, Assyria, Baldness, Balm, Bashan, Bench, Brass, Calamus, Calkers (Caulkers), Calneh, Canaan, Cassia, Cedar, Chilmad, Chittim, Cities, Coffer, Commerce, Coral, Corn, Countenance, Dan, Dedan, Ebony, Eden, Egypt, Elishah, Emerald, Exports, Fir Tree, Gammadim, Gebal, Haran, Helbon, Honey, Imports, Iron, Ivory, Javan, Kedar, Lead, Lebanon, Linen, Lubims, Ludim, Mariners (Sailors), Market, Merchant, Meshech, Minnith, Mourning, Mule, Oar, Persia, Phut, Pilot, Prophecy, Raamah, Servant, Sheba, Sheep, Shenir, Ship, Sidon, Silver, Spices, Stones, Tarshish, Tin, Togarmah, Tubal, Tyre, Vedan