Ayubu 32
1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu, kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kuliko yeye.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
8 Lakini ni Roho iliyo ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo ufahamu.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni; mimi nami nitawaambia ninalolijua.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyo ndani yangu inanisukuma;
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho karibu kupasuka.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Referencias cruzadas
116
- 1Job 10:7, Job 33:9, Job 13:15, Job 10:2, Job 27:4–6, Job 23:7, Job 31:1–40, Job 29:11–17
- 2Gen 22:21, Job 40:8, Job 27:2, Eph 4:26, Job 35:2, Job 27:5, Job 30:21, Job 10:3
- 3Job 8:6, Job 22:5–30, Job 24:25, Job 32:1, Job 15:34, Act 24:13, Job 26:2–4, Job 25:2–6
- 4Job 32:11–12, Pro 18:13
- 5Exo 32:19, Job 32:2
- 6Job 15:10, 1Ti 5:1, Tit 2:6, 1Pe 5:5, Lev 19:32, Job 15:7, 1Sa 17:28–30, Rom 13:7
- 7Pro 16:31, Job 12:12, Heb 5:12, Pro 1:1–4, Psa 34:11–12, Job 8:8–10, 1Ki 12:6–8
- 8Job 38:36, Job 33:4, 2Ti 3:16, Pro 2:6, Jas 1:5, Ecc 2:26, 1Co 2:10–12, 1Ki 3:12
- 9Mat 11:25, Ecc 4:13, Job 12:20, 1Co 1:26–27, 1Co 2:7–8, Jas 2:6–7, Jhn 7:48, Jer 5:5
- 101Co 7:25, 1Co 7:40
- 11Job 32:4, Job 5:27, Pro 28:11, Job 29:23, Ecc 12:9–10, Pro 18:17, Job 29:21
- 12Job 32:3, 1Ti 1:7
- 13Jer 9:23, 1Co 3:18, Isa 5:21, 1Co 1:27–29, Job 12:2, Isa 48:5, 1Co 1:19–21, Jdg 7:2
- 15Job 29:22, Mat 22:26, Mat 22:22, Mat 22:34, Job 6:24–25, Mat 7:23, Mat 22:46
- 16Job 13:5, Jas 1:19, Pro 17:28, Amo 5:13
- 17Job 33:12, Job 35:3–4, Job 32:10
- 18Psa 39:3, Act 4:20, Ezk 3:14–27, Jer 20:9, 2Co 5:13–14
- 19Mat 9:17
- 20Job 21:3, Job 13:13, Job 20:2, Pro 8:6–7, Job 13:19
- 21Lev 19:15, Job 13:8, Pro 24:23, 2Sa 14:17, 2Sa 14:20, Job 13:10, Deu 1:17, Act 12:22–23
- 22Psa 12:2–3, 1Th 2:5, Pro 29:5, Job 17:5, Gal 1:10