Ayubu 30
1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuliko mimi wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wezi.
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea wanavyopenda.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 “Ee Mwenyezi Mungu, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusharusha kwenye dhoruba.
23 Ninajua utanileta hadi kifoni, mahali wenye uhai wote wamewekewa.
24 “Hakika hakuna mtu anayemshambulia mhitaji anapoomba msaada katika shida yake.
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Referencias cruzadas
180
- 1Job 12:4, Luk 23:35, Psa 69:12, Psa 35:15–16, 2Ki 2:23, Luk 23:18, Act 17:5, Tit 1:12
- 3Job 24:5, Job 24:13–16, Heb 11:38
- 4Luk 15:16, Amo 7:14, 2Ki 4:38–39
- 5Dan 4:25, Psa 109:10, Gen 4:12–14, Dan 4:32–33
- 61Sa 22:1–2, Jdg 6:2, Rev 6:15, Isa 2:19
- 7Job 11:12, Job 6:5, Gen 16:12
- 8Pro 16:22, Isa 32:6, Pro 1:22, Mrk 6:24, Job 40:4, Jer 7:18, Pro 1:7, Psa 15:4
- 9Job 17:6, Lam 3:63, Lam 3:14, Psa 69:11–12, Psa 35:15–16, Job 12:4, Psa 44:14
- 10Isa 50:6, Mat 26:67, Psa 88:8, Num 12:14, Deu 25:9, Mat 27:30, Job 17:6, Pro 19:7
- 11Job 12:21, Job 12:18, Rut 1:21, 2Sa 16:5–8, Psa 32:9, Psa 35:21, Mat 26:67–68, Jas 1:26
- 12Job 19:12, Job 19:18, Psa 140:4–5, Isa 3:5
- 13Isa 3:12, Psa 69:26, Zec 1:15
- 14Psa 69:14–15, Isa 8:7–8, Psa 18:4, Job 22:16
- 15Hos 13:3, Job 6:4, Isa 44:22, Psa 88:15, Job 31:23, Psa 55:4–5, Job 10:16, Job 7:14
- 16Psa 42:4, Psa 22:14, Job 3:24, Isa 53:12, Psa 40:12, 1Sa 1:15
- 17Job 7:4, Psa 6:2–6, Psa 22:2, Job 33:19–21, Isa 38:13, Psa 38:2–8
- 18Job 19:20, Job 7:5, Job 2:7, Isa 1:5–6, Psa 38:5
- 19Job 9:31, Gen 18:27, Psa 69:14, Job 42:6, Psa 69:1–2, Jer 38:6, Job 2:8
- 20Job 19:7, Psa 22:2, Lam 3:8, Psa 80:4–5, Job 27:9, Mat 15:23, Lam 3:44
- 21Job 16:9–14, Job 10:14–17, 1Pe 5:6, Job 19:6–9, Job 10:3, Psa 77:7–9, Psa 89:13, Job 19:22
- 22Job 27:21, Psa 1:4, Hos 13:3, Hos 4:19, Job 9:17, Psa 104:3, Isa 17:13, Psa 18:10
- 23Ecc 12:5–7, Ecc 8:8, Ecc 9:5, Heb 9:27, Gen 3:19, Job 3:19, 2Sa 14:14, Job 21:33
- 24Job 19:7, Mat 27:39–44, Psa 35:25, Jdg 5:31
- 25Rom 12:15, Psa 35:13–14, Jer 13:17, Luk 19:41, Pro 19:17, Pro 17:5, Job 24:4, 2Co 9:9
- 26Jer 8:15, Job 3:25–26, Jer 14:19, Job 18:6, Job 23:17, Job 19:8, Isa 50:10, Mic 1:12
- 27Lam 2:11, Jer 4:19, Jer 31:20, Lam 1:20, Psa 22:4
- 28Psa 38:6, Psa 43:2, Psa 42:9, Isa 53:3–4, Lam 3:1–3, Job 19:7
- 29Mic 1:8, Psa 102:6, Job 17:14, Mal 1:3, Psa 44:19, Isa 13:21–22, Isa 38:14
- 30Lam 4:8, Psa 102:3, Psa 119:83, Lam 3:4, Lam 5:10
- 31Lam 5:15, Isa 21:4, Psa 137:1–4, Isa 22:12, Dan 6:18, Isa 24:7–9, Ecc 3:4