Ayubu 22
1 Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
2 “Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu? Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?
3 Je, Mwenyezi angefurahia nini kama ungekuwa mwadilifu? Au je, yeye angepata faida gani kama njia zako zingekuwa kamilifu?
4 “Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea na kuleta mashtaka dhidi yako?
5 Je, uovu wako si mkuu? Dhambi zako si hazina mwisho?
6 Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
7 Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
8 ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
9 Umewafukuza wajane mikono mitupu na kuzivunja nguvu za yatima.
10 Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, hatari ya ghafula inakutia hofu,
11 ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
12 “Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
13 Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
14 Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi atembeapo juu ya anga la dunia.
15 Je, utaifuata njia ya zamani, ambayo watu waovu waliikanyaga?
16 Waliondolewa kabla ya wakati wao, misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
17 Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
18 Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
19 “Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
20 ‘Hakika adui zetu wameangamizwa, nao moto umeteketeza mali yao.’
21 “Mjue sana Mungu ili uwe na amani, ndipo mema yatakapokujia.
22 Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake, na maneno yake uyaweke moyoni mwako.
23 Ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: Ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,
24 kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi, dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,
25 ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako, naye atakuwa fedha yako iliyo bora.
26 Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi, nawe utamwinulia Mungu uso wako.
27 Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.
28 Utakusudia jambo nalo litatendeka, nao mwanga utaangazia njia zako.
29 Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.
30 Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia, ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”
Referencias cruzadas
226
- 2Luk 17:10, Gal 6:7–8, Job 35:6–8, Pro 3:13–18, Psa 16:2, Job 21:15, Pro 9:12, Mat 5:29
- 3Pro 15:8, 2Co 7:1, Psa 147:10–11, Pro 12:22, Pro 11:1, Psa 119:3–6, Mal 2:17, Psa 119:59
- 4Job 14:3, Psa 143:2, Rev 3:19, Isa 3:14–15, Job 16:21, Job 34:23, Job 19:29, Job 9:19
- 5Psa 40:12, Job 15:5–6, Job 11:14, Job 21:27, Job 15:31–34, Job 32:3, Psa 19:12, Job 4:7–11
- 6Exo 22:26, Ezk 18:12, Ezk 18:16, Deu 24:10–18, Job 24:3, Job 31:19–20, Job 24:9–10, Deu 24:6
- 7Job 31:17, Mat 25:42, Isa 58:7, Ezk 18:7, Ezk 18:16, Rom 12:20, Job 31:31, Psa 112:9
- 8Isa 9:15, Mic 7:3, Job 31:34, Job 29:7–17, Isa 3:3, 1Ki 21:11–15, Psa 12:8, Job 13:8
- 9Job 24:21, Ezk 22:7, Job 24:3, Isa 10:2, Job 31:21, Exo 22:21–24, Isa 1:23, Psa 10:15
- 10Job 13:21, Job 6:4, Job 18:8–10, Job 19:6, Psa 11:6, 1Th 5:3, Pro 1:27, Pro 3:25–26
- 11Lam 3:54, Psa 69:1–2, Jon 2:3, Psa 124:4–5, Job 19:8, Isa 8:22, Job 5:14, Mat 8:12
- 12Job 11:8, Psa 8:3–4, Isa 66:1, Ecc 5:2, Psa 115:3, Isa 57:15, Psa 115:16
- 13Ezk 8:12, Psa 10:11, Ezk 9:9, Psa 73:11, Isa 29:15, Psa 59:7, Psa 94:7–9, Psa 64:5
- 14Psa 97:2, Psa 139:11–12, Psa 33:14, Job 26:9, Job 34:22, Jer 23:24, Psa 139:1–2, Luk 12:2–3
- 15Luk 17:26–27, Gen 6:11–13, Gen 6:5
- 16Job 15:32, Gen 7:17–24, Mat 24:37–39, 2Pe 2:5, 1Pe 3:19–20, Psa 55:23, Gen 7:11, Psa 102:24
- 17Job 21:14–15, Rom 1:28, Psa 4:6, Mat 8:29, Job 21:10, Isa 30:11, Mal 3:14, Mat 8:34
- 18Job 21:16, Job 12:6, Act 14:17, 1Sa 2:7, Psa 17:14, Jer 12:2, Psa 1:1, Act 15:16
- 19Psa 58:10, Psa 52:6, Psa 107:42, Rev 19:1–3, Job 9:23, Rev 18:20, Psa 97:8, Psa 48:11
- 20Gen 19:24, Job 20:26, 2Pe 2:6–7, Job 1:16, Luk 13:1–5, Job 21:27–28, Job 15:5–6, Luk 17:29–30
- 211Ch 28:9, Isa 27:5, Psa 34:10, Php 4:7, Eph 2:14–17, 2Co 5:20, Act 10:36, Jhn 17:3
- 22Psa 119:11, Job 23:12, Deu 4:1–2, Deu 6:6–9, Jer 15:16, Pro 4:21, Pro 4:4, Luk 2:19
- 23Zec 1:3, Job 11:13–14, Job 8:5–6, Isa 55:6–7, Hos 14:1–2, Zec 5:3–4, Jos 7:13–16, 2Ti 2:19
- 24Isa 13:12, 1Ki 9:28, 2Ch 9:27, 2Ch 9:10, 1Ki 22:48, 2Ch 1:5, Psa 45:9, Job 31:25
- 25Psa 16:5–6, Isa 33:6, Psa 18:2, Gen 15:1, Psa 84:11, Isa 41:10, Jas 2:5, Rom 8:31
- 26Psa 37:4, Isa 58:14, Job 27:10, Job 11:15, Rom 7:22, Psa 86:4, Sng 2:3, Psa 143:8
- 27Isa 58:9, 1Jn 5:14–15, Psa 116:1, Psa 50:14–15, Psa 91:15, Job 33:26, Psa 66:17–20, Job 34:28
- 28Mat 21:22, Psa 90:17, Psa 20:4, Isa 30:21, Pro 4:18, Jhn 8:12, Lam 3:37, Mal 4:2
- 29Job 5:19–27, Jas 4:6, 1Pe 5:5, Luk 1:52, Mat 23:12, Psa 91:14–16, Psa 92:9–11, Luk 18:9–14
- 30Job 42:7–8, Jas 5:15–16, Gen 18:26–32, Psa 18:20, Act 27:24, Mal 1:9, Psa 24:4, Mat 17:19–20
Temas en este capítulo
39
Afflicted, Antediluvians, Anthropomorphisms, Backsliders, Blasphemy, Blessing, Blindness, Creditor, Debt, Eliphaz, Flood, God, Gold, Grace of God, Heaven, Humility, Infidelity, Job, Joy, Man, Ophir, Orphan, Peace, Penitent, Poor, Prayer, Prosperity, Repentance, Righteous, Self-Righteousness, Sin, Skepticism, Sympathy, Uncharitableness, Vows, Wicked (People), Widow, Wisdom, Word of God