Ayubu 29
1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 wakati taa yake ilinimulika kichwani, na kwa mwanga wa Mungu nikapita katikati ya giza!
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 wakati Mwenyezi bado alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu wakawa wamenizunguka,
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyeshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 “Wakati nilienda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 vijana waliniona, wakakaa kando, nao wazee walioketi, wakasimama;
9 wakuu wakaacha kuzungumza, na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 Mizizi yangu itafika hata kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Walipokata tamaa niliwaonesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
Referencias cruzadas
152
- 1Job 27:1, Job 13:12, Num 23:7
- 2Job 1:1–5, Job 1:10, Jer 31:28, Jud 1:1, Job 7:3, Psa 37:28
- 3Psa 18:28, Jhn 8:12, Jhn 12:46, Eph 5:8, Job 18:6, Job 22:28, Job 11:17, Pro 24:20
- 4Psa 25:14, Pro 3:32, Job 1:10, Psa 27:5, Job 15:8, Psa 91:1, Col 3:3
- 5Psa 128:3, Psa 127:3–5, Sng 3:1–2, Sng 2:4, Psa 30:7, Deu 33:27–29, Jos 1:9, Job 23:8–10
- 6Psa 81:16, Job 20:17, Deu 32:13–14, Deu 33:24, Gen 49:11
- 7Rut 4:1–2, Deu 16:18, Zec 8:16, Rut 4:11, Deu 21:19, Job 31:21
- 8Lev 19:32, Tit 3:1, Pro 16:31, Rom 13:7, 1Pe 5:5, Pro 20:8, 1Pe 2:17, Rom 13:3–4
- 9Job 21:5, Job 40:4, Pro 10:19, Jas 1:19, Pro 30:32, Job 7:11, Jdg 18:19, Job 4:2
- 10Psa 137:6, Ezk 3:26
- 11Luk 4:22, Job 31:20, Pro 29:2, Luk 11:27
- 12Psa 72:12, Pro 21:13, Jas 1:27, Exo 22:22–24, Psa 82:2–4, Psa 68:5, Pro 24:11–12, Deu 10:18
- 13Phm 1:7, 2Ti 1:16–18, Job 31:19–20, Job 22:9, Isa 27:13, Deu 24:13, Psa 67:4, 2Co 9:12–14
- 14Isa 61:10, Isa 59:17, Psa 132:9, Eph 6:14, Rev 19:8, Job 27:6, 2Co 6:7, Isa 62:3
- 15Num 10:31, Mat 11:5, 1Co 12:12–31
- 16Pro 29:7, Psa 68:5, Est 2:7, Job 31:18, Pro 25:2, Job 24:4, Eph 5:1, Deu 17:8–10
- 17Psa 3:7, Pro 30:14, Psa 58:8, Psa 124:6, 1Sa 17:35, Psa 124:3
- 18Psa 30:6–7, Job 42:16–17, Gen 32:12, Job 5:26, Jer 49:16, Psa 91:16, Oba 1:4, Hab 2:9
- 19Jer 17:8, Psa 1:3, Hos 14:5–7, Job 18:16
- 20Gen 49:24, Isa 40:31, Psa 18:34, 2Co 4:16, Gen 45:13, Psa 3:3, Psa 103:5, Job 29:14
- 21Job 32:11–12, Job 29:9–10
- 22Deu 32:2, Isa 52:15, Sng 4:11, Ezk 20:46, Mat 22:46, Mic 2:6, Job 33:31–33, Amo 7:16
- 23Hos 6:3, Psa 72:6, Zec 10:1
- 24Psa 126:1, Psa 89:15, Psa 4:6, Gen 45:26, Luk 24:41
- 252Co 1:3–4, Jdg 11:8, Isa 61:1–3, Isa 35:3–4, 1Th 3:2–3, Gen 41:40, Gen 14:14–17, 2Co 7:5–7