Obadia 1
1 Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Mwenyezi Mungu: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
2 “Tazama, nitakufanya mdogo miongoni mwa mataifa, utadharauliwa kabisa.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika mapango ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
4 Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Mwenyezi Mungu.
5 “Ikiwa wezi wangekuja kwako, ikiwa wanyang’anyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
6 Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
7 Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
8 “Katika siku hiyo,” asema Mwenyezi Mungu, “je, sitaangamiza wenye hekima wa Edomu, hao wenye ufahamu katika milima ya Esau?
9 Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
10 Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
11 Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake, na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
12 Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
13 Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyang’anya mali yao katika siku ya maafa yao.
14 Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
15 “Siku ya Mwenyezi Mungu iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyotenda, nawe utatendewa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
16 Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo; watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwa na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Mwenyezi Mungu amesema.
19 Watu kutoka nchi ya Negebu wataimiliki milima ya Esau, na watu kutoka Shefela wataimiliki nchi ya Wafilisti. Watayamiliki mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
20 Kundi la Waisraeli walio uhamishoni Kanaani watarudi na kuimiliki nchi hadi Sarepta. Walio uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu wataimiliki miji ya Negebu.
21 Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Mwenyezi Mungu.
Referencias cruzadas
159
- 1Amo 1:11–12, Jol 3:19, Isa 63:1–6, Ezk 35:3–15, Psa 137:7, Mal 1:3–4, Ezk 25:12–14, Jer 6:4–5
- 2Isa 23:9, Num 24:18, Luk 1:51–52, Mic 7:10, Job 34:25–29, Psa 107:39–40, Ezk 29:15, 1Sa 2:7–8
- 3Isa 14:13–15, Pro 29:23, Jer 49:16, Isa 16:6, 2Ki 14:7, Mal 1:4, Isa 47:7–8, Pro 16:18
- 4Hab 2:9, Amo 9:2, Isa 14:12–15, Job 20:6–7, Jer 49:16, Jer 51:53, Job 39:27–28
- 5Jer 49:9, Deu 24:21, Lam 1:1, Isa 17:6, 2Sa 1:19, Isa 24:13, Jer 50:23, Isa 14:12
- 6Jer 49:10, Psa 139:1, Dan 2:22, Mat 6:19–20, Jer 50:37, Isa 10:13–14, Isa 45:3
- 7Psa 41:9, Jhn 13:18, Jer 49:7, Jer 30:14, Jer 4:30, Isa 19:11–14, Lam 1:19, Ezk 23:22–25
- 8Isa 29:14, Job 5:12–14, Psa 33:10, Isa 19:13–14, Isa 19:3, 1Co 3:19–20
- 9Ezk 25:13, Isa 63:1–3, Amo 1:12, Jer 49:22, Isa 34:5–8, Gen 36:11, Job 2:11, Jer 49:7
- 10Amo 1:11, Gen 27:41, Mal 1:3–4, Psa 89:45, Ezk 35:9, Psa 137:7, Ezk 35:5–7, Gen 27:11
- 11Psa 137:7, Nam 3:10, Jol 3:3, Psa 50:18, 2Ki 25:11, Jer 52:28–30, 2Ki 24:10–16
- 12Pro 17:5, Ezk 35:15, Mic 4:11, Pro 24:17–18, 1Sa 2:3, Mat 27:40–43, 2Pe 2:18, Mic 7:8–10
- 13Ezk 35:5, Zec 1:15, Psa 22:17, Ezk 35:10, 2Sa 16:12
- 14Isa 37:3, Amo 1:6, Oba 1:12, Gen 35:3, Jer 30:7, Psa 31:8, Amo 1:9
- 15Jas 2:13, Hab 2:8, Mat 7:2, Ezk 30:3, Jer 49:12, Jer 50:29, Jol 3:7–8, Psa 137:8
- 16Jol 3:17, Jer 49:12, Jer 25:15–16, Isa 51:22–23, 1Pe 4:17, Psa 75:8–9, Jer 25:27–29, Isa 49:25–26
- 17Rev 21:27, Amo 9:11–15, Isa 14:1–2, Jol 3:19–21, Amo 9:8, Jol 2:32, Isa 60:21, Jol 3:17
- 18Zec 12:6, Isa 10:17, Ezk 37:19, Mic 5:8, Isa 5:24, Isa 31:9, 1Co 3:12, Oba 1:16
- 19Amo 9:12, Zep 2:4–7, Jer 32:44, Ezk 37:21–25, Jer 31:4–6, Mal 1:4–5, Ezk 36:28, Jos 18:21–28
- 201Ki 17:9–10, Luk 4:26, Jer 33:13, Jer 32:44, Jer 3:18, Ezk 34:12–13, Hos 1:10–11, Amo 9:14–15
- 21Zec 14:9, Jas 5:20, Rev 11:15, Dan 7:27, Psa 22:28, Isa 19:20, 1Ti 4:16, Dan 2:44