Marko 11
1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage na Bethania katika Mlima wa Mizeituni. Isa akawatuma wawili wa wanafunzi wake,
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Na hapo mtakapoingia kijijini, mtampata mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
3 Mtu yeyote akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ mwambieni, ‘Bwana anamhitaji, na atamrudisha hapa baada ya muda mfupi.’ ”
4 Wakaenda, wakampata mwana-punda amefungwa kando ya barabara, karibu na mlango wa nyumba.
5 Walipokuwa wanamfungua, watu waliokuwa wamesimama karibu wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua huyo mwana-punda?”
6 Wakawajibu kama vile Isa alivyokuwa amewaagiza, nao wale watu wakawaruhusu.
7 Kisha wakamleta huyo mwana-punda kwa Isa na kutandika mavazi yao juu yake, naye akampanda.
8 Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakatandaza matawi waliyokuwa wamekata mashambani.
9 Kisha wale waliokuwa wametangulia mbele na wale waliokuwa wakifuata nyuma wakapaza sauti, wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Mwenyezi Mungu!”
10 “Umebarikiwa ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!” “Hosana kwake yeye aliye juu!”
11 Isa akaingia Yerusalemu na kwenda Hekaluni. Akaangalia kila kitu kilichokuwamo, lakini kwa kuwa ilishakuwa jioni, akaenda zake Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
12 Kesho yake walipokuwa wakitoka Bethania, Isa alikuwa na njaa.
13 Akauona mtini kwa mbali, naye akaenda ili aone kama ulikuwa na matunda. Alipoufikia, akakuta una majani tu, kwa kuwa hayakuwa majira ya tini.
14 Akauambia ule mti, “Tangu leo mtu yeyote asile kamwe matunda kutoka kwako.” Wanafunzi wake walimsikia akisema hayo.
15 Walipofika Yerusalemu, Isa akaingia katika eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakinunua na kuuza humo. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa,
16 wala hakumruhusu mtu yeyote kuchukua bidhaa kupitia ukumbi wa Hekalu.
17 Naye alipokuwa akiwafundisha, akasema, “Je, haikuandikwa kuwa: “ ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote’? Lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyang’anyi.’ ”
18 Viongozi wa makuhani na walimu wa Torati wakapata habari hizi, nao wakaanza kutafuta njia ya kumuua, kwa kuwa walikuwa wakimwogopa, kwa sababu umati wote walishangazwa na mafundisho yake.
19 Ilipofika jioni, Isa na wanafunzi wake wakatoka nje ya mji.
20 Kesho yake asubuhi walipokuwa wakipita, wakauona ule mtini umenyauka kutoka juu hadi kwenye mizizi yake.
21 Petro akakumbuka na kumwambia Isa, “Mwalimu, tazama! Ule mtini ulioulaani umenyauka!”
22 Isa akawajibu, “Mwaminini Mungu.
23 Amin, nawaambia, mtu yeyote atakayeuambia mlima huu, ‘Ng’oka ukatupwe baharini,’ wala asione shaka moyoni mwake, bali aamini kwamba hayo asemayo yametukia, atatimiziwa.
24 Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote mtakayoyaomba mkisali, aminini kwamba mmeyapokea, nayo yatakuwa yenu.
25 Nanyi kila msimamapo kusali, sameheni mkiwa na neno na mtu, ili naye Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu. [
26 Lakini kama ninyi msiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]”
27 Wakafika tena Yerusalemu, na Isa alipokuwa akitembea Hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa Torati pamoja na wazee wa watu wakamjia.
28 Wakamuuliza, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka ya kufanya hayo?”
29 Isa akawajibu, “Nitawauliza swali moja. Nijibuni, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
30 Je, ubatizo wa Yahya ulitoka mbinguni au kwa wanadamu? Niambieni!”
31 Wakahojiana wao kwa wao na kusema, “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
32 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu’ ” (waliwaogopa watu, kwa sababu kila mtu aliamini kwamba Yahya alikuwa nabii wa kweli);
33 kwa hiyo wakamjibu Isa, “Hatujui.” Naye Isa akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
Cross-references
183
- 1Luk 19:29–40, Mat 21:1–11, Jhn 12:14–19, Jhn 8:1, Act 1:12, Mrk 14:13, Mat 21:17, Zec 14:4
- 2Mat 21:2–3, Luk 19:30–31
- 3Mrk 14:15, 2Co 8:9, Act 17:25, Heb 2:7–9, Act 10:36, 1Ch 29:12–18, Psa 24:1, Act 1:24
- 4Luk 19:32–34, Mat 26:19, Heb 11:8, Mat 21:6–7, Jhn 2:5
- 7Zec 9:9, Luk 19:35–36, Mat 21:4–5, Mat 21:7–8, Jhn 12:12–16, 2Ki 9:13
- 8Lev 23:40
- 9Psa 118:25–26, Mat 21:9, Luk 19:37–38, Mat 23:39, Jhn 19:15, Jhn 12:13
- 10Ezk 37:24–25, Luk 2:14, Luk 19:38–40, Ezk 34:23–24, Amo 9:11–12, Psa 148:1, Isa 9:6–7, Jer 33:15–17
- 11Zep 1:12, Jhn 8:1–2, Mat 21:10–17, Luk 19:41–45, Luk 21:37–38, Ezk 8:9, Mal 3:1
- 12Mat 21:18–22, Mat 4:2, Jhn 19:28, Luk 4:2, Jhn 4:31–33, Heb 2:17, Jhn 4:6–7
- 13Luk 13:6–9, Mat 21:19, Isa 5:7, Luk 12:6–7
- 14Mat 21:19, Mat 3:10, Mat 7:19, Jhn 15:6, Mrk 11:20–21, Isa 5:5–6, Mat 12:33–35, Mat 21:44
- 15Jhn 2:13–17, Mat 21:12–16, Luk 19:45–47
- 17Isa 56:7, Jer 7:11, Luk 19:46, Jhn 2:16, 1Ki 8:41–48, Isa 60:7, Hos 12:7
- 18Mat 7:28, Mrk 12:12, Mat 21:45–46, Mat 21:38–39, 1Ki 21:20, Jhn 11:53–57, Mrk 3:6, Mat 21:15
- 19Luk 21:37, Mrk 11:11, Jhn 12:36
- 20Mat 15:13, Mat 21:19–22, Jhn 15:6, Mrk 11:14, Mat 13:6, Isa 40:24, Isa 5:4, Job 18:16–17
- 21Pro 3:33, 1Co 16:22, Mat 25:41, Zec 5:3–4, Mat 23:7
- 22Psa 62:8, Jhn 14:1, Mrk 9:23, 2Ch 20:20, Isa 7:9, Tit 1:1, Col 2:12
- 23Mat 17:20, Jhn 15:7, Mat 21:21, Psa 37:4, Jhn 14:13, Luk 17:6, Jas 1:5–6, Heb 11:17–19
- 24Mat 21:22, 1Jn 5:14–15, 1Jn 3:22, Jas 1:5–6, Jhn 15:7, Mat 18:19, Jhn 14:13, Mat 7:7–11
- 25Mat 6:14–15, Col 3:13, Eph 4:32, Luk 6:37, Mat 6:12, Jas 2:13, Mat 5:23, Mat 18:23–35
- 27Luk 20:1–8, Mat 21:23–27, Act 4:27–28, Psa 2:1–5, Jhn 10:23, Act 4:5–8, Mrk 14:1, Jhn 18:20
- 28Exo 2:14, Num 16:13, Num 16:3, Act 7:27–28, Act 7:51, Act 7:38–39
- 29Luk 20:3–8, Isa 52:13, Mat 21:24
- 30Jhn 1:6–8, Jhn 3:25–36, Jhn 1:15–36, Mrk 9:13, Luk 3:1–20, Mat 3:1–17, Mrk 1:1–11
- 31Jhn 1:34, Jhn 1:36, Mat 21:31–32, Jhn 1:29, Mat 21:25–27, Jhn 1:15, Mat 11:7–14, Jhn 3:29–36
- 32Mat 21:46, Mat 14:5, Mrk 12:12, Mat 3:5–6, Act 5:26, Mat 21:31–32, Mrk 6:20, Jhn 10:41
- 33Isa 6:9–10, 2Th 2:10–12, 2Co 4:3–4, Isa 29:9–14, Rom 1:28, 2Co 3:15, Mat 16:4, Luk 10:21–22
Parallel passages
3
- The Triumphal EntryMat 21:1–11, Mrk 11:1–11, Luk 19:28–40, Jhn 12:12–19
- Cleansing the TempleMat 21:12–17, Mrk 11:15–19, Luk 19:45–48
- The Cursing of the Fig TreeMat 21:18–22, Mrk 11:12–14
Topics in this chapter
35
Baptism, Bethany, Bethphage, Colt, Commandments, Contingencies, Faith, Forgiveness, God, Heaven, Hosanna, House of God, Hunger, Jesus, the Christ, John, Joy, Miracles, Money Changers, Mountain, Olives, Mount of, Opinion, Public, Persecution, Peter, Prayer, Prophecy, Quotations and Allusions, Rabbi, Reproof, Righteous, Sin, Temple, Theft and Thieves, Unfaithfulness, Unfruitfulness, Wicked (People)