1 Timotheo 3
1 Hili ni neno la kuaminiwa, kwamba mtu akitamani kuwa mwangalizi wa kundi la waumini, atamani kazi nzuri.
2 Basi, imempasa mwangalizi awe mtu asiye na lawama, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, anayejitawala, anayeheshimika, mkarimu, ajuaye kufundisha,
3 asiwe mlevi, wala mkali bali awe mpole, asiwe mgomvi wala mpenda fedha.
4 Lazima aweze kuisimamia nyumba yake mwenyewe vizuri na kuhakikisha kwamba watoto wake wanamtii na kuwa na heshima kwa kila njia.
5 (Kwa maana kama mtu hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atawezaje kuliangalia kundi la waumini la Mungu?)
6 Asiwe mtu aliyeongoka karibuni asije akajivuna na kuangukia kwenye hukumu ile ile ya ibilisi.
7 Inampasa pia awe na sifa njema kwa watu walio nje, ili asije akalaumiwa na kuanguka kwenye mtego wa ibilisi.
8 Vivyo hivyo, mashemasi nao wawe watu wanaostahili heshima, wasiwe wenye kauli mbili au wenye kujifurahisha kwa mvinyo, wala wanaotamani faida isiyo halali.
9 Inawapasa kushikamana sana na ile siri ya imani kwa dhamiri safi.
10 Ni lazima wapimwe kwanza; kisha kama hakuna neno dhidi yao, basi na waruhusiwe kuhudumu kama mashemasi.
11 Vivyo hivyo, wake zao wawe wanawake wanaostahili heshima, wasio wasingiziaji, bali wawe na kiasi na waaminifu katika kila jambo.
12 Shemasi awe mume wa mke mmoja, na aweze kusimamia watoto wake na watu wa nyumbani mwake vyema.
13 Wale ambao wamehudumu vyema katika huduma ya ushemasi hujipatia msimamo bora na ujasiri mkubwa katika imani yao ndani ya Al-Masihi Isa.
14 Ingawa ninatarajia kuja kwako hivi karibuni, ninakuandikia maagizo haya sasa ili,
15 nikikawia, utajua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, ambayo ndiyo jumuiya ya waumini ya Mungu aliye hai, iliyo nguzo na msingi wa kweli.
16 Bila shaka yoyote, siri ya utauwa ni kubwa: Alidhihirishwa katika mwili, akathibitishwa kuwa na haki katika Roho wa Mungu, akaonekana na malaika, akahubiriwa miongoni mwa mataifa, akaaminiwa ulimwenguni, akachukuliwa juu katika utukufu.
Cross-references
118
- 1Tit 1:7, Act 20:28, 1Pe 5:2, 1Pe 2:25, Jas 5:19–20, 1Ti 1:15, Heb 12:15, 2Ti 2:11
- 2Tit 1:6–9, 2Ti 2:24, Rom 12:13, 1Ti 5:9, 1Pe 4:9, 1Ti 3:10–11, 1Pe 5:8, Tit 2:2
- 3Tit 1:7, Tit 3:2, 1Ti 3:8, Eph 5:18, Jas 4:1, Isa 28:7, 1Pe 5:2, Luk 21:34–36
- 4Tit 1:6, Gen 18:19, 1Ti 3:12, Tit 2:2, Act 10:2, Jos 24:15, Tit 2:7, Psa 101:2–8
- 51Sa 3:13, Eph 5:24, Act 20:28, Eph 5:32, 1Ti 3:15, Eph 1:22
- 61Ti 6:4, Heb 5:12–13, 1Pe 5:5, 1Pe 2:2, Isa 14:12–14, 2Co 12:7, 1Co 4:6–8, 1Co 3:1
- 72Co 8:21, 2Ti 2:26, Col 4:5, 1Co 10:32, 2Co 6:3, Act 6:3, 1Th 4:12, 1Ti 6:9
- 8Php 1:1, Act 6:3–6, 1Ti 3:3, 1Ti 5:23, Tit 2:3, Lev 10:9, Ezk 44:21, 1Ti 3:12
- 91Ti 1:19, 2Jn 1:9–10, 1Ti 1:5, 1Ti 3:16
- 101Ti 5:22, 1Ti 3:13, Tit 1:6–7, Act 6:1–2, 1Ti 3:2, 1Ti 3:6, 1Co 1:8, 1Jn 4:1
- 11Tit 2:3, Tit 3:2, 1Ti 3:2, 1Pe 5:8, 2Ti 3:3, Pro 10:18, 1Ti 6:2, Jer 9:4
- 121Ti 3:2, 1Ti 3:4–5, Php 1:1, 1Ti 3:8
- 13Mat 25:21, Heb 6:10, Php 1:14, Mat 20:28, Act 6:5, Rom 12:7–8, 2Ti 2:1, Luk 19:17
- 14Phm 1:22, 1Co 11:34, Heb 13:23, 3Jn 1:14, 2Jn 1:12, 2Co 1:15–17, 1Th 2:18, 1Ti 4:13
- 151Pe 2:5, Eph 2:21–22, 1Ch 22:13, Mat 16:18–19, 1Ki 2:4, 1Th 1:9, Jhn 14:6, Mat 16:16
- 16Jhn 1:14, Heb 1:3, Mrk 16:19, Rom 16:25, 1Jn 5:6–8, Php 2:6–8, 1Jn 1:2, Col 1:23
Topics in this chapter
37
Ambition, Angel (A Spirit), Avarice, Bishop, Children, Church, Commandments, Conscience, Covetousness, Deacon, Diligence, Family, Gentiles, Gospel, Hospitality, House, Integrity, Jesus, the Christ, Marriage, Meekness, Minister, Christian, Mysteries, Parents, Patience, Polygamy, Pride, Purity, Salvation, Satan, Slander, Sobriety, Strife, Temperance, Trinity, Truth, Wife, Women