Hosea 6
1 “Njooni, tumrudie Mwenyezi Mungu. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
2 Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
3 Tumkubali Mwenyezi Mungu, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
4 “Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
5 Kwa hiyo nimewakata ninyi vipande vipande nikitumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
6 Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, na kumkubali Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
7 Wamevunja agano kama Adamu: hawakuwa waaminifu kwangu huko.
8 Gileadi ni mji wa watenda maovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
9 Kama wanyang’anyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
10 Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
11 “Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,
Cross-references
87
- 1Job 5:18, Deu 32:39, 1Sa 2:6, Lam 3:40–41, Hos 14:4, Isa 55:7, Job 34:29, Isa 2:3
- 22Ki 20:5, 1Co 15:4, Isa 26:19, Ezk 37:11–13, Hos 13:14, Psa 30:4–5, Jhn 14:19, Gen 17:18
- 3Jer 24:7, Hos 14:5, Pro 2:1–5, Psa 72:6, Php 3:13–15, Mat 13:11, Rev 22:16, Zec 10:1
- 4Hos 13:3, Psa 78:34–37, Hos 11:8, Psa 106:12–13, Mat 13:21, Luk 13:7–9, 2Pe 2:20–22, Luk 19:41–42
- 5Jer 23:29, Jer 1:10, Jer 5:14, Heb 4:12, Psa 119:120, Isa 11:4, Rev 2:16, Rom 2:5
- 6Mat 9:13, Mat 12:7, Pro 21:3, 1Sa 15:22, Amo 5:21, Ecc 5:1, Isa 1:11, Mat 5:7
- 7Gen 3:11, Hos 8:1, Hos 5:7, Job 31:33, Jer 9:6, Gen 3:6, Ezk 16:59–61, 2Ki 17:15
- 8Hos 12:11, Act 25:3, Mat 26:15–16, Isa 59:6, Hos 5:1, 2Sa 3:27, Jos 21:38, 1Ki 2:5
- 9Luk 22:2–6, Hos 7:1, Zep 3:3, Hos 5:1, Pro 1:11–19, Ezk 22:9, Jer 7:9–10, Jer 11:9
- 10Hos 5:3, Ezk 23:5, Jer 5:30–31, Jer 23:14, Jer 2:12–13, 2Ki 17:7, Jer 18:13, Jer 3:6
- 11Jol 3:13, Rev 14:15, Jer 51:33, Job 42:10, Psa 126:1, Zep 2:7, Mic 4:12
Topics in this chapter
29
Adam, Afflictions and Adversities, Backsliders, Blessing, Character, Church, Cloud, Depravity of Man, Dew, Ephraim, Fall of Man, Formalism, Gilead, Hypocrisy, Instability, Knowledge, Lukewarmness, Meteorology and Celestial Phenomena, Minister, Christian, Offerings, Quotations and Allusions, Repentance, Righteous, Robbers, Sin, Symbols and Similitudes, Wisdom, Word of God, Worship