Amosi 7
1 Hili ndilo alilonionesha Bwana Mungu Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
2 Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mungu Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
3 Kwa hiyo Mwenyezi Mungu akaghairi. Kisha Mwenyezi Mungu akasema, “Hili halitatokea.”
4 Hili ndilo Bwana Mungu Mwenyezi alilonionesha katika maono: Bwana Mungu Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
5 Ndipo nikalia, “Bwana Mungu Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
6 Kwa hiyo Mwenyezi Mungu akaghairi. Bwana Mungu Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
7 Hili ndilo alilonionesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
8 Naye Mwenyezi Mungu akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
9 “Mahali pa Isaka pa juu pa kuabudia pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
10 Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
11 Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “ ‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli wataenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’ ”
12 Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
13 Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
14 Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
15 Lakini Mwenyezi Mungu akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
16 Sasa basi, sikieni neno la Mwenyezi Mungu. Ninyi mnasema, “ ‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaka.’
17 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: “ ‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako wa kiume na wa kike watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itaenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’ ”
Cross-references
132
- 1Jol 1:4, Amo 8:1, Jol 2:25, Nam 3:15–17, Isa 33:4, Amo 4:9, Jer 24:1, Jer 1:11–16
- 2Isa 37:4, Ezk 11:13, Jer 14:7, Ezk 9:8, Jer 42:2, Jer 14:20–21, Exo 10:15, Dan 9:19
- 3Deu 32:36, Jon 3:10, Hos 11:8, Psa 106:45, Jol 2:14, Amo 7:6, Jer 26:19, Jas 5:16
- 4Amo 7:1, Isa 66:15–16, Exo 9:23–24, Heb 1:7, Jer 21:12, Amo 4:11, Isa 27:4, Amo 1:4
- 5Psa 85:4, Jol 2:17, Amo 7:2–3, Isa 1:9, Jer 30:19, Isa 10:25
- 6Jon 4:2, Psa 135:14, Jon 3:10, Jdg 10:16, Amo 7:3, Jer 26:19, Jdg 2:18, Psa 90:13
- 72Ki 21:13, Isa 28:17, Rev 21:15, Zec 2:1–2, Isa 34:11, Rev 11:1, 2Sa 8:2, Lam 2:8
- 8Amo 8:2, Lam 2:8, Jer 15:6, Ezk 7:2–9, Isa 28:17, 2Ki 21:13, Mic 7:18, Nam 1:8–9
- 92Ki 15:8–10, Gen 46:1, Amo 3:14, Gen 26:23–25, Lev 26:30–31, Hos 10:8, Amo 5:5, Amo 8:14
- 10Jer 38:4, 1Ki 12:31–32, Mat 21:23, Act 24:5, Jer 26:8–11, Luk 23:2, 1Ki 13:33, Act 5:28
- 112Ki 17:6, Amo 6:7–8, Psa 56:5, Amo 7:9, Mat 26:61, Jer 28:10–11, Act 6:14
- 12Mat 8:34, 1Co 2:14, Rom 16:18, Isa 30:10, 1Sa 9:9, Ezk 13:19, 2Ch 16:10, Act 16:39
- 13Amo 2:12, 1Ki 12:32, 1Ki 12:29, 1Ki 13:1, Act 5:28, Act 5:40, Act 4:17–18
- 14Amo 1:1, Zec 13:5, 2Ki 2:5, 1Co 1:27, 2Ki 4:38, 2Ki 2:3, 2Ch 19:2, 2Ki 6:1
- 152Sa 7:8, Ezk 2:3–4, Act 1:8, Jer 1:7, Act 5:20, Psa 78:70–72, Mat 4:18–19, Mat 9:9
- 16Ezk 20:46, Mic 2:6, Ezk 21:2, Amo 7:13, Deu 32:2, Jer 28:15–17, 1Ki 22:19, 1Sa 15:16
- 17Hos 9:3, 2Ki 17:6, Jer 28:16, Ezk 4:13, Hos 4:13–14, Jer 29:21, Jer 29:31–32, Isa 13:16