Waamuzi 10
1 Baada ya Abimeleki, Tola mwana wa Pua mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, aliyeishi huko Shamiri, katika nchi ya vilima ya Efraimu, akainuka kuokoa Israeli.
2 Akawa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini na tatu. Ndipo akafa, naye akazikwa huko Shamiri.
3 Baada yake akafuatiwa na Yairi, Mgileadi, aliyekuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini na mbili.
4 Alikuwa na wana thelathini waliopanda punda thelathini. Nao walikuwa na miji thelathini huko Gileadi, inayoitwa Hawoth-Yairi hadi leo.
5 Yairi akafa, naye akazikwa huko Kamoni.
6 Tena Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Mwenyezi Mungu. Wakaabudu Mabaali na Maashtorethi, na miungu ya Aramu, miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu, miungu ya Waamoni, na miungu ya Wafilisti. Na kwa kuwa Waisraeli walimwacha Mwenyezi Mungu wala hawakuendelea kumtumikia,
7 hivyo hasira ya Mwenyezi Mungu ikawaka dhidi ya Waisraeli. Naye akawatia mikononi mwa Wafilisti na Waamoni,
8 ambao waliowaonea na kuwatesa mwaka huo. Kwa miaka kumi na nane wakawatesa Waisraeli wote upande wa mashariki mwa Mto Yordani huko Gileadi, katika nchi ya Waamori.
9 Waamoni nao wakavuka Yordani ili kupigana na Yuda, Benyamini na nyumba ya Efraimu, nayo nyumba ya Israeli ikawa katika taabu kubwa.
10 Ndipo Waisraeli wakamlilia Mwenyezi Mungu wakasema, “Tumetenda dhambi dhidi yako, kumwacha Mungu wetu na kutumikia Mabaali.”
11 Mwenyezi Mungu akawaambia, “Wamisri, Waamori, Waamoni, Wafilisti,
12 Wasidoni, Waamaleki na Wamaoni walipowadhulumu ninyi, nanyi mkanililia na kuomba msaada, je, sikuwaokoa mikononi mwao?
13 Lakini ninyi mmeniacha na kuitumikia miungu mingine, kwa hiyo sitawaokoa tena.
14 Nendeni mkaililie ile miungu mlioichagua. Hiyo miungu na iwaokoe mnapokuwa katika taabu!”
15 Lakini Waisraeli wakamwambia Mwenyezi Mungu, “Tumetenda dhambi. Ututendee lile unaloona kuwa jema kwako, lakini twakusihi utuokoe sasa.”
16 Nao wakaiondoa hiyo miungu migeni kati yao nao wakamtumikia Mwenyezi Mungu. Naye akahuzunika kwa sababu ya taabu ya Israeli.
17 Waamoni walipoitwa vitani na kupiga kambi kule Gileadi, Waisraeli walikusanyika na kupiga kambi huko Mispa.
18 Viongozi wa watu wa Gileadi wakaambiana wao kwa wao, “Yeyote atakayeanzisha mashambulizi dhidi ya Waamoni atakuwa kiongozi wa wote wanaoishi Gileadi.”
Cross-references
91
- 1Jdg 2:16, Jos 15:48, Jdg 3:9
- 3Num 32:29, Gen 31:48
- 4Num 32:41, Deu 3:14, Jdg 5:10, Jdg 12:14
- 62Ki 23:13, 1Ki 11:5, Psa 106:36, 1Ki 11:33, 1Ki 11:7, Jer 2:13, 2Ki 17:16, Jdg 16:23
- 7Jdg 2:14, Deu 32:16–22, 1Sa 12:9–10, Nam 1:2, Deu 31:16–18, Psa 74:1, Isa 50:1, Nam 1:6
- 8Isa 30:13, 1Th 5:3, Jdg 10:5
- 92Ch 15:5, 1Sa 28:15, 2Ch 20:1–2, Jdg 6:3–5, 2Ch 14:9, Jdg 3:12–13, Deu 28:65
- 101Sa 12:10, Psa 107:28, Psa 107:19, Psa 107:13, Psa 106:43–44, Jdg 3:9
- 11Exo 14:30, Num 21:21–25, Jdg 3:31, Jdg 2:1–3, 1Sa 12:8, Neh 9:9–11, Num 21:35, Psa 135:10–11
- 12Jdg 6:3, Jdg 5:19–31, Psa 106:42–43, 2Ch 26:6–7
- 13Jer 2:13, 1Ch 28:9, Jdg 2:12, Jon 2:8, Deu 32:15
- 14Deu 32:37–38, Jer 2:28, Pro 1:25–27, Isa 10:3, Deu 32:26–28, 1Ki 18:27–28, 2Ki 3:13
- 151Sa 3:18, 2Sa 15:26, 1Jn 1:8–10, 2Sa 24:14, Pro 28:13, Jos 9:25, Jon 3:9, 2Sa 10:12
- 16Isa 63:9, Psa 106:44–45, Hos 11:8, Jer 31:20, Deu 32:36, Luk 19:41, Eph 4:32, Ezk 18:30–32
- 17Jdg 11:29, Gen 31:49, Jdg 11:11
- 18Jdg 11:11, Isa 3:1–8, Jdg 1:1, Jdg 11:5–8, Isa 34:12, 1Sa 17:25, Jdg 12:7