Amosi 8
1 Hili ndilo alilonionesha Bwana Mungu Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
2 Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Mwenyezi Mungu akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
3 Bwana Mungu Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
6 mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
7 Mwenyezi Mungu ameapa kwake mwenyewe, aliye Fahari ya Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote wanaoishi ndani yake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Mto Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana Mungu Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae magunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mungu Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Mwenyezi Mungu.
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Mwenyezi Mungu, lakini hawatalipata.
13 “Katika siku ile “wasichana wazuri na wavulana wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”
Cross-references
105
- 1Amo 7:1, Amo 7:4, Amo 7:7
- 2Amo 7:8, Lam 4:18, Mic 7:1, Jer 1:11–14, Jer 24:1–3, Ezk 7:6, Ezk 3:7, Ezk 3:10
- 3Amo 6:9–10, Amo 5:23, Jer 9:21–22, Lev 10:3, Amo 5:16, Jer 22:18, Nam 3:3, Jol 1:5
- 4Pro 30:14, Amo 5:11, Psa 14:4, Isa 32:6–7, Psa 12:5, Psa 140:12, Amo 2:6–7, Jas 5:6
- 5Neh 13:15–21, Hos 12:7, Mic 6:10–11, Deu 25:13–16, Lev 19:36, Pro 16:11, Pro 11:1, Exo 20:8–10
- 6Amo 2:6, Jol 3:3, Amo 8:4, Jol 3:6, Neh 5:8, Lev 25:39–42, Neh 5:1–5
- 7Amo 6:8, Hos 9:9, Hos 8:13, Hos 7:2, Psa 10:11, Deu 33:26–29, Jer 31:34, Isa 43:25
- 8Amo 9:5, Jer 46:8, Hos 4:3, Psa 18:7, Isa 5:25, Jer 12:4, Mat 24:30, Psa 114:3–7
- 9Mrk 15:33, Mat 27:45, Luk 23:44, Jer 15:9, Mat 24:29, Mic 3:6, Amo 5:8, Isa 59:9–10
- 10Jer 6:26, Zec 12:10, Job 20:23, Jer 48:37, Ezk 7:18, Luk 7:12–13, Hos 2:11, Isa 15:2–3
- 111Sa 3:1, Psa 74:9, 2Ch 15:3, 1Sa 28:6, Ezk 7:26, Mat 9:36, Mic 3:6, 1Sa 28:15
- 12Rom 11:7–10, 2Ti 3:6–7, Mat 12:30, Pro 14:6, Mat 24:23–26, Dan 12:4, Rom 9:31–33
- 13Hos 2:3, Lam 2:21, Lam 1:18, Deu 32:25, Psa 63:1, Isa 41:17–20, Jer 48:18, Zec 9:17
- 14Amo 5:5, 1Ki 12:28–29, Deu 9:21, Act 9:2, Jer 25:27, Hos 8:5–6, Hos 10:5, 2Ch 36:16
Topics in this chapter
36
Amos, Balances, Baldness, Beer-Sheba, Dan, Darkness, Dishonesty, Eclipse, Egypt, Famine, God, Hunger, Israel, Prophecies Concerning, Measure, Money, Moon, Music, New Moon, Nile, Oppression, Poor, Sabbath, Seekers, Servant, Shekel, Shoe, Silver, Summer, Sun, Symbols and Similitudes, Thirst, Vision, War, Wicked (People), Word of God, Worldliness