2 Wafalme 15
1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na mbili. Mama yake aliitwa Yekolia, kutoka Yerusalemu.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Mwenyezi Mungu, kama Amazia baba yake alivyofanya.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
5 Mwenyezi Mungu akampiga mfalme kwa ukoma hadi siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
6 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
7 Azaria akalala na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi. Naye Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
9 Akafanya maovu machoni pa Mwenyezi Mungu, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akapanga njama dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua, na akawa mfalme baada yake.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
12 Kwa hiyo neno la Mwenyezi Mungu lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi kwenye kiti cha utawala cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa hadi Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua, na akawa mfalme baada yake.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na njama alizozipanga, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua tumbo wanawake wote wenye mimba.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
18 Akatenda maovu machoni pa Mwenyezi Mungu. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
21 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
22 Menahemu akalala na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Mwenyezi Mungu. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akapanga njama dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akawa mfalme baada yake.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
28 Akafanya maovu machoni pa Mwenyezi Mungu. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akapanga njama dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Hoshea akamshambulia Peka na kumuua, kisha akawa mfalme baada yake katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
31 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
33 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Mwenyezi Mungu, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Mwenyezi Mungu.
36 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
37 (Katika siku hizo, Mwenyezi Mungu akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Cross-references
171
- 12Ki 15:13, 2Ki 14:21, 2Ch 26:1, 2Ch 26:3–4, 2Ki 15:8, 2Ki 14:16–17, 2Ki 15:30–38
- 22Ch 26:3–4
- 32Ki 14:3–4, 2Ki 12:2–3, 2Ch 26:4
- 42Ch 32:12, 2Ki 18:4, 1Ki 22:43, 2Ch 17:6, 2Ki 12:3, 2Ki 15:35, 2Ch 34:3, 2Ki 14:4
- 5Lev 13:46, Num 12:14, 2Ki 7:3, 2Sa 15:2–4, 2Ch 26:16–23, 2Sa 8:15, Deu 24:8, 2Sa 3:29
- 62Ki 14:18, 2Ch 26:5–15
- 72Ch 26:23, Isa 6:1
- 82Ki 14:16–17, 2Ki 14:29–15:1, 2Ki 14:21
- 92Ki 13:2, 2Ki 14:24, 2Ki 10:31, 2Ki 10:29, 2Ki 13:11
- 102Ki 9:31, 1Ki 16:9–10, 2Ki 15:14, 1Ki 15:28, 2Ki 15:25, Amo 7:9, 2Ki 9:24, Hos 1:4–5
- 112Ki 14:28
- 122Ki 10:30, Zec 1:6, 2Ki 13:13, Jhn 19:24, Mrk 13:31, Act 1:16, 2Ki 13:10, Jhn 10:35
- 132Ki 15:1, Pro 28:17, Pro 28:2, Mat 1:8–9, Job 20:15, Psa 55:23, 1Ki 16:15, 1Ki 16:24
- 141Ki 14:17, 1Ki 16:15, 1Ki 15:21, 1Ki 16:8–9, 1Ki 16:17, 1Ki 15:33
- 151Ki 14:19, 1Ki 14:29, 1Ki 22:39, 2Ki 15:11
- 162Ki 8:12, 1Ki 4:24, Hos 13:16, Amo 1:13
- 192Ki 14:5, 2Ki 18:16, 1Ch 5:25–26, 2Ki 12:18, Hos 10:6, Jer 17:5, 2Ki 16:8, Isa 9:1
- 20Job 1:3, 2Sa 19:32, 2Ki 18:14–17, 2Ki 23:35, Rut 2:1, 2Ki 15:29, 2Ki 17:3–4
- 232Ki 21:19, 1Ki 16:8, Job 20:5, 1Ki 22:51, 1Ki 15:25
- 242Ki 15:9, 2Ki 15:18
- 252Ch 28:6, 1Ki 16:9, 2Ki 9:5, 2Ki 15:27, 2Ki 15:10, 2Ki 9:14
- 272Ki 15:23, Isa 7:4, Isa 7:1, Isa 7:9, 2Ch 28:6, 2Ki 15:2, 2Ki 15:8, 2Ki 15:25
- 282Ki 21:2, 2Ki 13:6, 2Ki 15:9, 2Ki 13:2, 2Ki 15:18
- 291Ch 5:26, 2Ki 17:6, 1Ki 15:20, Jos 20:7, 2Ki 16:7, Jos 11:1, 1Ch 5:6, Jos 19:37
- 302Ki 17:1, Hos 10:15, 2Ki 15:32–33, 2Ki 15:25, 2Ki 15:10, Isa 8:6, Hos 10:3, 2Ch 28:4–6
- 322Ki 15:7, 1Ch 3:12, 2Ki 15:27, Mat 1:9, 2Ki 15:1, 2Ki 14:21, 2Ki 15:13, 2Ki 15:23
- 332Ch 27:1
- 342Ch 26:4–5, 2Ki 15:3–4, 2Ch 27:2
- 352Ki 12:3, 2Ch 23:20, 2Ch 32:12, 2Ki 18:4, 2Ch 27:3–9, 2Ki 15:4
- 362Ki 15:6–7, 2Ch 27:4–9
- 372Ki 16:5, Isa 7:1, Hos 5:12–13, 2Ki 10:32, Jer 43:10, Isa 7:8, 2Ch 28:6, Isa 38:1–22
- 381Ki 14:31, 1Ki 1:2, 1Ki 14:20, 2Sa 7:12, 1Ch 3:13, 2Ch 28:1, 2Ki 16:1, Mat 1:9
Topics in this chapter
57
Abel-Beth-Maachah, Afflictions and Adversities, Ahaz, Argob, Arieh, Assyria, Beth-Maachah, Captive, Citizens, Conspiracy, Elah, Gadi, Galilee, Gilead, Hazor, Homicide, Hoshea, Ijon, Influence, Israel, Prophecies Concerning, Janoah, Jecholiah, Jehu, Jerusha, Jotham, Kedesh, Leprosy, Massacre, Menahem, Money, Naphtali, Palace, Pekah, Pekahiah, Prophecy, Pul, Regency, Regicide, Remaliah, Reubenites, Rezin, Rulers, Samaria, Sanitation, Shallum, Tax, Temple, Tiglath-Pileser, Tiphsah, Tirzah, Tribute (Taxes), Usurpation, Uzziah, War, Zachariah, Zadok, Zebulun