1 Wafalme 22
1 Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
2 Lakini katika mwaka wa tatu, Yehoshafati mfalme wa Yuda akateremka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu, na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
4 Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utaenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
5 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta ushauri wa Mwenyezi Mungu.”
6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii, wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
7 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Mwenyezi Mungu hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
8 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia kwake twaweza kuuliza ushauri wa Mwenyezi Mungu, lakini namchukia kwa sababu hatabiri jambo lolote jema kunihusu, ila hunitabiria mabaya kila mara. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
9 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
10 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, huku manabii wote wakitabiri mbele yao.
11 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma. Naye akatangaza, “Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi Mungu, ‘Kwa hizi pembe utawapiga Waaramu hadi waangamizwe.’ ”
12 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ataitia mkononi mwa mfalme.”
13 Mjumbe aliyekuwa ameenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
14 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Mwenyezi Mungu aishivyo, nitamwambia kile tu Mwenyezi Mungu atakachoniambia.”
15 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Mwenyezi Mungu atawatia mkononi mwa mfalme.”
16 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Mwenyezi Mungu?”
17 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Mwenyezi Mungu akasema, ‘Watu hawa hawana kiongozi. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’ ”
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, ila mabaya tu?”
19 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Mwenyezi Mungu: Nilimwona Mwenyezi Mungu ameketi kwenye kiti chake cha enzi, na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
20 Naye Mwenyezi Mungu akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
21 Hatimaye, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Mwenyezi Mungu na kusema, ‘Nitamshawishi.’
22 “Mwenyezi Mungu akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitaenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Mwenyezi Mungu akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
23 “Kwa hiyo sasa Mwenyezi Mungu ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Mwenyezi Mungu ameamuru maafa kwa ajili yako.”
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Mwenyezi Mungu alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
25 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapoenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
26 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni Mikaya, mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji, na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
27 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji hadi nitakaporudi salama.’ ”
28 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Mwenyezi Mungu hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
31 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
32 Wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati alipopiga kelele,
33 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, wakaacha kumfuatilia.
34 Lakini mtu mmoja akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake la vita, “Geuza gari na uniondoe katika mapigano, nimejeruhiwa.”
35 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari lake la vita kuelekea Waaramu. Damu kutoka jeraha lake ikatiririka ndani ya gari lake, na jioni yake akafa.
36 Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
37 Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
38 Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Mwenyezi Mungu lilivyokuwa limesema.
39 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea ngome, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
40 Ahabu akalala na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
41 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na tano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na tano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
43 Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakuenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Mwenyezi Mungu. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
44 Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
45 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
46 Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
47 Wakati ule, hakukuwa na mfalme katika Edomu; naibu ndiye alitawala.
48 Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu; lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjikia huko Esion-Geberi.
49 Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
50 Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Yehoramu mwanawe akawa mfalme baada yake.
51 Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda. Naye akatawala katika Israeli kwa miaka miwili.
52 Akafanya maovu machoni pa Mwenyezi Mungu kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
53 Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
Cross-references
320
- 11Ki 20:34
- 21Ki 15:24, 1Ki 22:1, Mat 16:21, 1Ki 22:41, 2Ki 8:18, Mat 12:40, 2Ch 18:1–27, 1Ki 22:44
- 3Deu 4:43, 1Ki 4:13, Jos 21:38, Jdg 16:2, 2Sa 19:10
- 42Ki 3:7, Eph 5:11, 2Ch 19:2, 2Ch 18:3, 2Jn 1:11, 1Co 15:33, Psa 139:21–22, Rev 2:26
- 5Pro 3:5–6, 2Ch 18:4–5, 2Ki 3:11, Jer 21:2, Jer 42:2–6, Ezk 20:1–3, Num 27:21, Jos 9:14
- 61Ki 18:19, Jer 23:14–17, Ezk 13:22, Ezk 13:7–16, 2Ch 18:14, 2Ti 4:3, Jer 8:10–11, Mat 7:15
- 72Ch 18:6–7, 2Ki 3:11–13
- 8Jhn 7:7, Jhn 3:19–21, Amo 5:10, Jhn 17:14, Gal 4:16, Jer 38:4, Jhn 15:18–19, Mic 2:7
- 92Ch 18:8, 1Ki 22:26–27, 2Ki 9:32, Dan 1:18, Isa 39:7
- 10Est 5:1, 2Ch 18:9–11, Ezk 13:1–9, 1Ki 18:29, 1Ki 22:30, Act 25:23, Act 12:21, Jer 27:14–16
- 11Zec 1:18–21, Deu 33:17, Jer 27:2, Jer 23:25, Jer 28:2–3, Jer 29:21, Jer 28:10–14, Act 19:13–16
- 121Ki 22:32–36, 2Ch 35:22, 1Ki 22:6–15
- 13Hos 7:3, Amo 7:13–17, 1Co 2:14–16, Isa 30:10–11, Psa 10:11, Psa 11:1, Mic 2:6–7, Psa 14:1
- 14Num 24:13, Jer 26:2–3, Num 22:18, Ezk 3:17–19, Num 22:38, 2Ch 18:12–13, 2Co 2:17, 1Ki 18:15
- 15Jdg 10:14, Ecc 11:9, 1Ki 18:27, Mat 26:45, 2Ki 3:13, 2Ch 18:14
- 16Jos 6:26, Mat 26:63, 1Sa 14:24, 2Ch 18:15, Mat 22:16–17, Mrk 5:7, Jer 42:3–6, Act 19:13
- 17Num 27:17, Mat 9:36, 1Ki 22:34–36, 2Ch 18:16–17, Jer 50:17, Zec 13:7, Act 10:11–17, Ezk 34:4–6
- 181Ki 22:8, Luk 11:45, Pro 29:1, Pro 10:24, Pro 27:22
- 19Job 2:1, Job 1:6, Dan 7:9–10, Isa 6:1–3, Psa 103:20–21, Mat 18:10, 2Ch 18:18–22, Rev 4:2–3
- 20Ezk 14:9, Job 12:16, Jer 4:10
- 21Job 2:1, Job 1:6–7, 1Ki 22:23
- 22Jdg 9:23, 1Sa 16:14, 1Sa 19:9, Job 1:8–11, 1Ki 22:20, Ezk 14:9, 2Th 2:9–12, Job 12:16
- 23Ezk 14:9, Mat 24:24–25, Isa 6:9–10, Isa 44:20, 2Ch 25:16, Isa 3:11, Deu 2:30, 1Ki 20:42
- 24Act 23:2, Mic 5:1, Lam 3:30, 1Ki 22:11, 2Ch 18:23–24, Jer 29:26–27, Mat 26:68, Jhn 15:18
- 251Ki 20:30, 2Pe 2:1, Rev 19:20, Jer 29:32, Jer 23:15, Jer 29:21–22, Isa 9:14–16, Jer 28:16–17
- 272Ch 16:10, 2Ch 18:25–27, Rev 2:10, Psa 102:9, Isa 30:20, Act 5:18, Jer 37:15, Eph 3:1
- 28Mic 1:2, Num 16:29, Mrk 12:37, Act 13:10–11, Deu 18:20–22, 1Ki 18:21–24, Isa 44:26, Amo 3:1
- 292Ch 18:28, 1Ki 22:2–9
- 302Ch 35:22, Jer 23:24, 1Sa 28:8, 1Ki 20:38, Psa 12:2, 1Ki 14:2, Pro 21:30, 2Sa 14:2
- 311Ki 20:24, 2Ch 18:30, Jer 16:6, 1Ki 20:1, Gen 19:11, 1Sa 30:2, 1Ki 20:16, 1Ki 20:33–42
- 32Jon 2:1–2, Pro 13:20, Exo 14:10, Psa 116:1–2, Psa 130:1–4, 2Ch 18:31, Psa 91:15, Psa 50:15
- 33Psa 76:10, 1Ki 22:31
- 342Ch 35:23, Mic 6:13, 1Sa 17:49, Rev 9:9, 2Ki 9:24, 2Sa 15:11, 2Ch 18:30
- 351Ki 22:28, 1Ki 20:42
- 362Ki 14:12, 1Ki 12:24, 1Ki 22:31, Jdg 7:7–8, 1Sa 4:10, 1Ki 22:17, Jdg 21:24, 2Sa 19:8
- 381Ki 21:19, Mat 24:35, Jos 23:14–15, Isa 48:3–5, Jer 44:21–23, Isa 44:25–26, Zec 1:4–6
- 39Amo 3:15, Psa 45:8, 1Ki 16:20, Amo 6:4, Ezk 27:15, 1Ki 15:31, 1Ki 10:22, Ezk 27:6
- 402Ki 1:2, Deu 31:16, 2Sa 7:12, 2Ch 20:35, 1Ki 2:10, 1Ki 22:51, 1Ki 11:21, 2Ki 1:17
- 412Ch 20:31, 2Ch 17:1, 1Ch 3:10, 1Ki 22:2
- 421Ki 15:10, 1Ki 14:21, 1Ki 15:2, 2Ki 8:16, 2Ki 1:17
- 431Ki 15:14, 2Ki 12:3, Pro 4:27, 1Ki 14:23, 2Ch 20:3–30, 2Ch 19:3–4, 1Ki 15:11, Exo 32:8
- 442Ki 8:18, 2Ch 19:2, 1Ki 22:2, 2Co 6:14, 2Ch 21:6
- 452Ch 20:34, 1Ki 14:29, 1Ki 11:41
- 461Ki 15:12, 1Ki 14:24, Deu 23:17, Jud 1:7, Gen 19:5, 1Ti 1:10, Jdg 19:22, Rom 1:26–27
- 472Ki 3:9, 2Sa 8:14, 2Ki 8:20, Gen 27:40, Gen 36:31–43, Gen 25:23, Psa 108:9–10
- 481Ki 9:26, 1Ki 10:22, 1Ki 9:28, 2Ch 9:21, Psa 48:7, 2Ch 20:21, Isa 60:9, 2Ch 20:35–37
- 502Ch 21:1, 1Ki 2:10, 2Ch 21:5–7, 1Ki 15:24, 1Ki 22:40, 1Ki 11:43, 2Ki 8:16–18, 1Ki 14:31
- 511Ki 15:25, 2Ki 1:17, 1Ki 22:40
- 521Ki 15:26, 1Ki 21:25, 1Ki 16:30–33, 2Ki 9:22, 1Ki 15:34, 2Ki 8:27, Rev 3:20, Mrk 6:24
- 531Ki 16:30–32, 1Ki 21:29, 2Ki 3:2, 1Ki 16:7, Isa 65:3, Jdg 2:1–11, Ezk 18:14–18, Psa 106:29
Parallel passages
1
- Micaiah and the Death of Ahab1Ki 22:1–40, 2Ch 18:1–34
Topics in this chapter
64
Ahab, Ahaziah, Alliances, Amon, Archery, Armies, Arrow, Azubah, Bread, Chariot, Chenaanah, Children, Coat of Mail, Commerce, Decision, Demons, Deputy, Dog (Sodomite?), Edomites, Exports, Ezion-Gaber (Ezion-Geber), Flattery, Gates, Gold, High Places, Horn, Horse, House, Infidelity, Influence, Iron, Irony, Israel, Prophecies Concerning, Ivory, Jehoram, Jehoshaphat, Joash, Lying, Micaiah, Minister, Christian, Mocking, Ophir, Persecution, Pool, Presumption, Prisoners, Prophecy, Prophets, Ramoth-Gilead, Regency, Reproof, Revenge, Rulers, Samaria, Satan, Shilhi, Ship, Sodomites, Sodomy, Tarshish, Vision, Wicked (People), Zeal, Religious, Zedekiah