Waamuzi 19
1 Katika siku hizo, Waisraeli hawakuwa na mfalme. Basi Mlawi mmoja aliyeishi sehemu za mbali katika nchi ya vilima ya Efraimu, akamchukua suria mmoja kutoka Bethlehemu ya Yuda.
2 Lakini suria wake akafanya ukahaba, akamwacha na kurudi nyumbani mwa baba yake huko Bethlehemu ya Yuda. Baada ya kukaa huko kwa muda wa miezi minne,
3 mume wake akaenda kumsihi arudi. Alienda na mtumishi wake na punda wawili. Yule mwanamke akamkaribisha nyumbani mwa baba yake, naye baba yake alipomwona akamkaribisha kwa furaha.
4 Baba mkwe wake, yaani baba yake yule msichana, akamsihi akae. Hivyo akakaa na huyo baba mkwe wake kwa siku tatu, wakila na kunywa, na kulala huko.
5 Siku ya nne wakaamka mapema naye akajiandaa kuondoka, lakini baba wa yule msichana akamwambia mkwewe, “Ujiburudishe kwa kitu cha kula, ndipo uweze kwenda.”
6 Basi wakaketi wote wawili ili kula na kunywa pamoja. Baadaye baba wa msichana akamwambia, “Tafadhali ubakie usiku huu upate kujifurahisha.”
7 Basi yule mtu alipotaka kuondoka, baba mkwe wake akamsihi, hivyo akabaki usiku ule.
8 Asubuhi ya siku ya tano, alipoamka ili aondoke, baba wa yule msichana akamwambia, “Jiburudishe nafsi yako. Ngoja hadi alasiri!” Kwa hiyo wote wawili wakala chakula pamoja.
9 Kisha yule mtu alipoinuka aende zake pamoja na suria wake na mtumishi wake, baba mkwe wake, yaani baba wa yule msichana, akamwambia, “Tazama sasa jioni inakaribia. Ulale hapa, usiku unakaribia. Ukae, ukajifurahishe nafsi yako. Kesho unaweza kuamka asubuhi na mapema uende nyumbani kwako.”
10 Lakini akakataa kulala tena, akaondoka na kuelekea Yebusi (ndio Yerusalemu), akiwa na punda wake wawili waliotandikwa, pamoja na suria wake.
11 Alipokaribia Yebusi na usiku ukiwa umekaribia, mtumishi akamwambia bwana wake, “Haya sasa natuingie katika mji huu wa Wayebusi tulale humo.”
12 Lakini bwana wake akamjibu, “Hapana. Hatutaingia kwenye mji wa kigeni, ambao watu wake si Waisraeli. Tutaendelea hadi Gibea.”
13 Tena akasema, “Haya, tujitahidi tufike Gibea au Rama, nasi tutalala katika mji huo.”
14 Hivyo wakaendelea na safari, nalo jua likazama walipokaribia Gibea ya Benyamini.
15 Wakageuka ili kuingia na kulala Gibea. Wakaingia humo, wakaketi kwenye uwanja wa mji, wala hakuna mtu yeyote aliyewakaribisha kwake ili wapate kulala.
16 Jioni ile, mzee mmoja toka nchi ya vilima ya Efraimu, aliyekuwa anaishi huko Gibea (watu wa sehemu ile walikuwa Wabenyamini), akarudi kutoka kwenye kazi zake za shamba.
17 Alipotazama na kuwaona hao wasafiri katika uwanja wa mji, yule mzee akawauliza, “Ninyi mnaenda wapi? Nanyi mmetoka wapi?”
18 Akamwambia, “Tumepita kutoka Bethlehemu ya Yuda, tunaelekea katika nchi ya vilima ya Efraimu ninakoishi. Nilienda Bethlehemu ya Yuda na sasa ninaenda katika nyumba ya Mwenyezi Mungu. Hakuna mtu yeyote aliyenikaribisha katika nyumba yake.
19 Tunazo nyasi na chakula cha punda wetu, pia mkate na divai kwa ajili yetu sisi watumishi wako: mimi, mtumishi wako mwanamke, pamoja na huyu kijana tuliye naye. Hatuhitaji kitu zaidi.”
20 Yule mzee akawaambia, “Amani iwe kwenu! Karibuni nyumbani mwangu. Nitawapa mahitaji yenu yote, ila tu msilale katika uwanja huu.”
21 Hivyo akamwingiza nyumbani mwake na kuwalisha punda wake. Baada ya kunawa miguu yao, wakala na kunywa.
22 Walipokuwa wakijiburudisha, wanaume waovu wa mji huo wakaizingira ile nyumba. Wakagonga mlango na kusema kwa sauti kuu kwa yule mzee mwenye nyumba, “Mtoe nje yule mwanaume aliyeingia kwako, tupate kumlawiti.”
23 Yule mwenye nyumba akatoka nje na kuwaambia, “Hapana, ndugu zangu, msiwe waovu namna hii, ninawasihi. Kwa kuwa huyu mwanaume ni mgeni wangu, msifanye jambo hili la aibu.
24 Tazameni, hapa yupo binti yangu ambaye ni bikira, na suria wa mtu huyu. Nitawatoleeni hawa sasa, mkawatwae kwa nguvu na kuwafanyia lolote mtakalo. Lakini kwa mwanaume huyu msimfanyie jambo ovu hivyo.”
25 Lakini wale wanaume hawakumsikiliza. Hivyo yule mwanaume akamtoa yule suria wake nje kwa wale watu, nao wakambaka na kumnajisi usiku kucha hadi asubuhi. Kulipoanza kupambazuka, wakamwachia aende.
26 Alfajiri yule mwanamke akarudi kwenye ile nyumba bwana wake alikokuwa, akaanguka chini mlangoni, akalala pale hata kulipopambazuka.
27 Bwana wake alipoamka asubuhi na kufungua mlango wa nyumba na kutoka nje ili kuendelea na safari yake, tazama, yule suria wake alikuwa ameangukia penye ingilio la nyumba, mikono yake ikiwa penye kizingiti.
28 Akamwambia yule suria, “Inuka, twende.” Lakini hakujibu. Yule bwana akamwinua, akampandisha juu ya punda wake, na wakaondoka kwenda nyumbani.
29 Alipofika nyumbani, akachukua kisu na kumkatakata yule suria kiungo kwa kiungo, vipande kumi na mbili, na kuvipeleka katika sehemu zote za Israeli.
30 Kila mtu aliyeona akasema, “Jambo la namna hii halijaonekana wala kutendeka, tangu Waisraeli walipopanda kutoka Misri. Fikirini juu ya jambo hili! Tafakarini juu ya jambo hili! Tuambieni tufanye nini!”
Cross-references
135
- 1Jdg 18:1, Mat 2:6, Jdg 17:8, Jdg 21:25, Jos 24:30, Jos 24:33, Mal 2:15, Jdg 17:6
- 2Ezk 16:28, Lev 21:9, Deu 22:21
- 3Gen 50:21, Jhn 8:11, Gen 34:3, Jhn 8:4–5, Lev 19:17, Mat 1:19, Hos 2:14, Jdg 15:1
- 5Gen 18:5, Jdg 19:8, Jhn 4:34, 1Ki 13:7, 1Sa 14:27–29, 1Sa 30:12, Act 9:19, Psa 104:15
- 6Rut 3:7, Jdg 19:9, Jdg 16:25, Est 1:10, 1Sa 25:36, Jdg 19:21–22, Psa 104:15, Rev 11:10
- 9Jas 4:13–14, Pro 27:1, Luk 24:29
- 10Jos 15:8, Jos 15:63, 1Ch 11:4–5, Jdg 1:8, 2Sa 5:6, Jos 18:28
- 11Jos 15:63, 2Sa 5:6, Gen 10:16, Jdg 19:10, Jdg 1:21
- 13Jos 18:28, Hos 5:8, Isa 10:29, 1Sa 10:26, Jos 18:25–26
- 15Mat 25:43, Heb 13:2, Jdg 19:18, Gen 19:2–3, Gen 18:2–8, Mat 25:35
- 16Pro 14:23, Psa 104:23, Jdg 19:1, Psa 128:2, Pro 24:27, Jdg 19:14, Ecc 5:12, 1Th 4:11–12
- 17Gen 16:8, Gen 32:17
- 18Jdg 18:31, Jhn 15:6, Psa 26:9, Jos 18:1, Jdg 20:18, 1Sa 1:7, Jdg 19:5, 1Sa 1:3
- 20Jdg 6:23, Gen 43:23–24, Jas 2:15–16, 1Co 1:3, 1Ch 12:18, 1Pe 4:9, Jhn 14:27, Rom 12:13
- 21Luk 7:44, Gen 43:24, Jhn 13:14–15, Gen 18:4, 2Sa 11:8, 1Ti 5:10, 1Sa 25:41, Gen 24:32–33
- 22Gen 19:4–5, 1Co 6:9, Jdg 20:5, Deu 13:13, Rom 1:26–27, Jud 1:7, 2Co 6:15, Jdg 16:25
- 232Sa 13:12, Jdg 20:6, Gen 34:7, Jos 7:15, Gen 19:6–7, Deu 22:21
- 24Gen 19:8, Deu 21:14, Gen 34:2, Rom 3:8
- 25Eph 4:19, Hos 10:9, Jer 5:7–8, Gen 4:1, Hos 9:9, Hos 7:4–7
- 261Pe 3:6, Gen 18:12, Jdg 19:27, Jdg 19:3
- 28Jdg 20:5, 1Ki 18:29
- 29Jdg 20:6–7, 1Sa 11:7, Deu 21:22–23, Rom 10:2
- 30Jdg 20:7, Pro 13:10, Pro 11:14, Pro 15:22, Pro 24:6, Hos 9:9, Pro 20:18