Waamuzi 21
1 Wanaume wa Israeli walikuwa wameapa kiapo kule Mispa, wakasema: “Hapana mtu yeyote wetu atakayemwoza binti yake kwa Mbenyamini.”
2 Watu wakaenda Betheli, wakaketi mbele za Mungu hadi jioni, wakapaza sauti zao wakilia kwa uchungu.
3 Wakasema, “Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, kwa nini jambo hili limewapata Waisraeli? Kwa nini kabila moja la Israeli limekosekana?”
4 Kesho yake asubuhi na mapema watu wakajenga madhabahu na kuleta sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani.
5 Ndipo Waisraeli wakauliza, “Ni kabila lipi la Israeli ambalo halikukusanyika mbele za Mwenyezi Mungu?” Kwa kuwa walikuwa wameapa kiapo kikuu kuwa yeyote asiyefika mbele za Mwenyezi Mungu huko Mispa, kwa hakika angeuawa.
6 Basi Waisraeli wakahuzunika kwa ajili ya ndugu zao Wabenyamini, wakasema, “Leo kabila moja limekatiliwa mbali na Israeli.
7 Sasa tutawezaje kuwapa binti zetu kuwa wake zao, hao waliobaki, na tumeapa kwa Mwenyezi Mungu kuwa hatutawapa binti zetu kuwa wake zao?”
8 Ndipo wakasema, “Ni kabila lipi la Israeli ambalo halikukusanyika mbele za Mwenyezi Mungu huko Mispa?” Wakagundua kuwa hakuna hata mmoja kutoka Yabesh-Gileadi aliyefika kambini kwa kusanyiko.
9 Kwa kuwa walipohesabu waliona hapakuwa mtu yeyote wa Yabesh-Gileadi.
10 Ndipo mkutano wakatuma wapiganaji elfu kumi na mbili, wakawaamuru kwenda Yabesh-Gileadi na kuua kwa panga wale wote walioishi huko, wakiwemo wake na watoto.
11 Wakasema, “Hili ndilo mtakalofanya: Ueni kila mwanaume na kila mwanamke ambaye si bikira.”
12 Wakapata kati ya watu walioishi Yabesh-Gileadi wanawali mia nne, mabikira, nao wakawachukua kwenye kambi huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
13 Ndipo mkutano ukatuma ujumbe wa amani kwa Wabenyamini huko katika mwamba wa Rimoni.
14 Basi Wabenyamini wakarudi wakati ule, nao wakapewa wale wanawali wa Yabesh-Gileadi waliohifadhiwa. Lakini hawakuwatosha wanaume wote.
15 Waisraeli wakahuzunika kwa ajili ya Wabenyamini, kwa kuwa Mwenyezi Mungu alikuwa ameweka ufa katika makabila ya Israeli.
16 Viongozi wa kusanyiko wakasema, “Kwa kuwa wanawake wa Wabenyamini wameangamizwa, tufanyeje ili kuwapatia wake wale wanaume waliosalia?”
17 Wakaendelea kusema, “Lazima tuwape Wabenyamini waliopona wake ili wawe na warithi, nalo kabila lolote katika Israeli lisifutike.
18 Hatuwezi kuwapa binti zetu kuwa wake, kwa kuwa sisi Waisraeli tumeapa kiapo hiki: ‘Alaaniwe mtu yeyote ampaye Mbenyamini mke.’ ”
19 Ndipo waliposema, “Tazama iko sikukuu ya kila mwaka ya Mwenyezi Mungu katika Shilo, kaskazini mwa Betheli na mashariki mwa ile barabara inayotoka Betheli kwenda Shekemu, upande wa kusini wa Lebona.”
20 Hivyo wakawaelekeza Wabenyamini, wakisema, “Nendeni mkajifiche kwenye mashamba ya mizabibu,
21 na mkae macho. Wasichana wa Shilo watakapojiunga kwenye kucheza, tokeni kwenye hayo mashamba ya mizabibu, na kila mmoja ajinyakulie mke kutoka miongoni mwa hao wasichana wa Shilo, nanyi mwende nao katika nchi ya Benyamini.
22 Baba zao au ndugu zao watakapotulalamikia, tutawaambia, ‘Kuweni wakarimu kwetu, nanyi mturuhusu tuwe nao kwa kuwa hatukuweza kumpa kila mtu mke tulipopigana. Lakini ninyi pia hamna hatia, kwa kuwa hamkuwapa wao binti zenu kuwa wake.’ ”
23 Basi hivyo ndivyo Wabenyamini walivyofanya. Wasichana walipokuwa wakicheza, kila mtu akanyakua msichana mmoja, akaenda naye ili awe mke wake. Kisha wakarudi katika urithi wao na kuijenga upya miji na kuishi humo.
24 Wakati huo Waisraeli wakaondoka sehemu ile na kwenda nyumbani kwao, kwa makabila yao na kwa jamaa zao, kila mmoja kwenye urithi wake mwenyewe.
25 Katika siku hizo, Waisraeli hawakuwa na mfalme; kila mtu alifanya alivyoona ni vyema machoni pake.
Cross-references
115
- 1Jdg 20:1, Act 23:12, Jdg 21:18, Jdg 20:8, Ecc 5:2, Mrk 6:23, Deu 7:2–3, Jer 4:2
- 2Jdg 20:26, Jdg 20:18, 1Sa 30:4, Jdg 2:4, Jdg 21:12, Jos 18:1, Jdg 20:23, Gen 27:38
- 3Psa 80:12, Jer 12:1, Deu 29:24, Pro 19:3, Jos 7:7–9, Isa 63:17, Psa 74:1
- 42Sa 24:25, Heb 13:10, Psa 78:34–35, 2Sa 24:18, 1Ki 8:64, Jdg 6:26, Hos 5:15, Exo 20:24–25
- 5Jdg 5:23, Jer 48:10, Lev 27:28–29, Jdg 21:18, 1Sa 11:7, Jdg 21:1
- 6Jdg 21:15, Jdg 20:23, Luk 19:41–42, Jdg 11:35, Hos 11:8, 2Sa 2:26
- 7Jdg 21:1, Jdg 21:18, 1Sa 14:28–29, 1Sa 14:45
- 81Sa 31:11–13, 1Sa 11:1–3, 2Sa 2:5–6
- 10Jdg 5:23, Jdg 21:5, 1Sa 11:7, 1Sa 15:3, Deu 13:15, Jos 7:24
- 11Num 31:17–18, Deu 2:34
- 12Jos 18:1, Psa 78:60, Jdg 20:23, Jdg 20:18, Jer 7:12
- 13Deu 20:10, Jdg 20:47, Isa 57:19, Luk 10:5, Jos 15:32, Eph 2:17
- 141Co 7:2, Jdg 21:12, Jdg 20:47
- 15Jdg 21:6, 1Ch 15:13, 1Ch 13:11, Isa 30:13, Isa 58:12, Jdg 21:17
- 17Num 26:55, Num 36:7
- 18Jdg 21:1, Jdg 11:35
- 19Exo 23:14–16, Psa 81:3, Jhn 5:1, 1Sa 1:3, Num 10:10, Jhn 7:2, Jdg 18:31, Lev 23:6
- 21Exo 15:20, Jdg 11:34, Jer 31:13, 2Sa 6:21, Psa 150:4, Psa 149:3, Luk 17:25, 1Sa 18:6
- 22Jdg 21:1, Jdg 21:18, Mrk 10:6–8, Gen 1:27, Jdg 21:7, Gen 7:13, Pro 20:25, Phm 1:9–12
- 23Jdg 20:48
- 25Deu 12:8, Pro 3:5, Jdg 17:6, Ecc 11:9, Pro 14:12, Jdg 19:1, Jdg 18:1, Mic 2:1–2