Ezekieli 46
1 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
2 Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa hadi jioni.
3 Siku za Sabato na za Mwezi Mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Mwenyezi Mungu penye lile ingilio la ile njia.
4 Sadaka za kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Mwenyezi Mungu siku ya Sabato zitakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
5 Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja, na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
6 Siku ya Mwezi Mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
7 Atatoa sadaka ya nafaka ya: efa moja kwa huyo fahali, na efa moja kwa huyo kondoo dume; na kwa wana-kondoo atatoa nafaka nyingi kama atakavyo kutoa; atatoa hini ya mafuta kwa kila efa.
8 Mkuu anayetawala atakapoingia, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
9 “ ‘Watu wa nchi wanapokuja mbele za Mwenyezi Mungu katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini; na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
10 Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, na akitoka nao nje wanapotoka.
11 “ ‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
12 Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Mwenyezi Mungu, iwe ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, atafunguliwa lango linaloelekea mashariki. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje. Baada yake kutoka nje, lango litafungwa.
13 “ ‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Mwenyezi Mungu, utaitoa kila siku asubuhi.
14 Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Mwenyezi Mungu ni agizo la kudumu.
15 Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
16 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Ikiwa mkuu anayetawala atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake; itakuwa mali yao kwa urithi.
17 Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka hadi mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
18 Mkuu anayetawala hafai kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali yao. Mkuu huyo atawapa wanawe urithi wao katika mali yake mwenyewe, ili pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’ ”
19 Kisha mtu yule akanileta kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango hadi kwenye vyumba vitakatifu vilivyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
20 Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi, na kuoka sadaka ya nafaka, ili kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
21 Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
22 Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
23 Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
24 Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”
Mga kaugnay na talata
110
- 1Isa 66:23, Ezk 44:1–2, Ezk 45:17–19, Exo 20:9, Ezk 8:16, Ezk 46:6, Heb 4:9–10, Gen 3:19
- 2Ezk 44:3, Ezk 46:8, 2Ch 23:13, Col 1:28, 1Ch 17:16, Mat 26:39, Ezk 45:19, 2Ch 29:29
- 3Luk 1:10, Jhn 10:9, Heb 10:19–22
- 4Ezk 45:17, Num 28:9–10
- 5Ezk 45:24, Ezk 46:7, Deu 16:17, Num 28:12, Ezk 46:11–12, Lev 14:21, Num 6:21
- 6Ezk 46:1
- 7Ezk 46:5
- 8Ezk 46:2, Col 1:18, Ezk 44:1–3
- 9Deu 16:16, Exo 23:14–17, Exo 34:23, 2Pe 2:20–21, Psa 84:7, Mal 4:4, Ezk 1:17, Heb 10:38
- 10Psa 42:4, 1Ch 29:20, 1Ch 29:22, 2Ch 6:2–4, 2Ch 20:27–28, Heb 4:14–16, Rev 2:1, Neh 8:8–9
- 11Ezk 46:5, Ezk 46:7, Num 28:1–29, Deu 16:1–22, Lev 23:1–44, Num 15:1–41
- 12Ezk 45:17, Ezk 46:1–2, Lev 23:38, Ezk 46:8, 2Ch 29:31, Ezk 44:3, Ezr 6:17, Eph 5:2
- 13Isa 50:4, Exo 12:5, Dan 8:11–13, Psa 92:2, Num 28:3–8, Exo 29:38–42, Rev 13:8, Lev 12:6
- 14Num 28:5
- 15Heb 10:1–10, Heb 9:26, Heb 7:27, Num 28:6, Exo 29:42
- 162Ch 21:3, Gal 4:7, Jhn 8:35–36, Mat 25:34, Luk 10:42, Psa 37:18, Gen 25:5–6, Rom 8:29–32
- 17Lev 25:10, Gal 4:30–31, Mat 25:14–29, Luk 19:25–26
- 18Ezk 45:8, 1Ki 21:19, Ezk 22:27, Psa 72:2–4, Jer 23:5–6, Isa 32:1–2, Eph 4:8, Isa 11:3–4
- 19Ezk 42:9, Ezk 44:4–5, Ezk 40:44–46
- 202Ch 35:13, Ezk 44:19, Lev 2:4–7, Ezk 44:29, Lev 7:1–38, 1Sa 2:13–15
- 24Ezk 46:20, Jhn 21:15–17, 1Pe 5:2, Mat 24:45