Isaya 50
1 Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: “Iko wapi hati ya talaka ya mama yako ambayo kwayo niliachana naye? Au nimewauza ninyi kwa nani miongoni mwa watu wanaonidai? Kwa ajili ya dhambi zenu mliuzwa, kwa sababu ya makosa, mama yenu aliachwa.
2 Nilipokuja, kwa nini hapakuwa hata mtu mmoja? Nilipoita, kwa nini hapakuwa hata mtu mmoja wa kujibu? Je, mkono wangu ni mfupi mno hata nisiweze kuwakomboa? Je, mimi sina nguvu za kukuokoa? Kwa kukemea tu naikausha bahari, naigeuza mito ya maji kuwa jangwa; samaki wake wanaoza kwa kukosa maji na kufa kwa ajili ya kiu.
3 Ninalivika anga weusi na kufanya gunia kuwa kifuniko chake.”
4 Bwana Mungu Mwenyezi amenipa ulimi uliofundishwa, ili kujua neno limtegemezalo aliyechoka. Huniamsha asubuhi kwa asubuhi, huamsha sikio langu lisikie kama mtu afundishwaye.
5 Bwana Mungu Mwenyezi amezibua masikio yangu, nami sikuwa mwasi, wala sikurudi nyuma.
6 Niliwapa mgongo wangu wale wanipigao, mashavu yangu wale wang’oao ndevu zangu; sikuuficha uso wangu kutokana na fedheha na kutemewa mate.
7 Kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi ananisaidia, sitatahayarika. Kwa hiyo nimekaza uso wangu kama gumegume, nami ninajua sitaaibika.
8 Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu. Ni nani basi atakayeleta mashtaka dhidi yangu? Tukabiliane uso kwa uso! Mshtaki wangu ni nani? Ni nani aliye mshtaki wangu?
9 Ni Bwana Mungu Mwenyezi anisaidiaye mimi. Ni nani huyo atakayenihukumu? Wote watachakaa kama vazi, nondo watawala wawamalize.
10 Ni nani miongoni mwenu amchaye Mwenyezi Mungu, na kulitii neno la mtumishi wake? Yeye atembeaye gizani, yeye asiye na nuru, na alitumainie jina la Mwenyezi Mungu, na amtegemee Mungu wake.
11 Lakini sasa, ninyi nyote mnaowasha mioto, na kupeana mienge iwakayo ninyi kwa ninyi, nendeni, tembeeni katika nuru ya moto wenu na ya mienge mliyoiwasha. Hili ndilo mtakalolipokea kutoka mkononi mwangu: Mtalala chini kwa mateso makali.
Mga kaugnay na talata
82
- 1Deu 32:30, Jer 3:8, Mat 18:25, 2Ki 4:1, Neh 5:5, Isa 52:3, Deu 24:1–4, Hos 2:2–4
- 2Isa 59:1, Num 11:23, Isa 66:4, Jos 3:16, Gen 18:14, Pro 1:24, Exo 14:21, Isa 43:16
- 3Rev 6:12, Psa 18:11–12, Exo 10:21, Mat 27:45
- 4Luk 21:15, Jer 1:9, Pro 25:11, Exo 4:11–12, Jhn 7:15–17, Pro 15:23, Psa 143:8, Psa 119:147
- 5Jhn 14:31, Heb 5:8, Php 2:8, Isa 35:5, Jhn 8:29, Mat 26:39, Jhn 15:10, Isa 48:8
- 6Mat 26:67, Mrk 14:65, Mrk 15:19, Mat 27:30, Luk 22:63–64, Isa 53:5, Lam 3:30, Jhn 18:22
- 7Heb 13:6, Ezk 3:8–9, Jhn 16:33, Isa 42:1, Rom 1:16, Luk 9:51, Psa 89:21–27, 1Pe 4:16
- 8Rom 8:32–34, Isa 41:1, Rev 12:10, Isa 41:21, Isa 43:26, 1Ti 3:16, Deu 19:17, Exo 22:9
- 9Job 13:28, Psa 102:26, Isa 41:10, Heb 1:11–12, Psa 39:11, Isa 51:6–8
- 10Jhn 12:46, Isa 26:3–4, Mic 7:7–9, Psa 23:4, Jhn 8:12, Psa 27:13–14, Lam 3:25–26, Psa 25:14
- 11Jer 17:5–7, Rom 1:21–22, Rom 10:3, Jhn 8:24, Mat 15:6–8, Psa 20:7–8, Isa 28:15–20, Jon 2:8
Mga paksa sa kabanatang ito
24
Afflictions and Adversities, Assault and Battery, Backsliders, Colors, Darkness, Decision, Divorce, Doubting, Faith, Fear, Flint, God, Jesus, the Christ, Justification, Life, Meteorology and Celestial Phenomena, Moth, Persecution, Righteous, Salvation, Self-Righteousness, Sin, Wicked (People), Words