Ezekieli 44
1 Ndipo yule mtu akanirudisha mpaka kwenye lango la nje la mahali patakatifu, lile linaloelekea upande wa mashariki, nalo lilikuwa limefungwa.
2 Mwenyezi Mungu akaniambia, “Lango hili litabaki limefungwa. Haliruhusiwi kufunguliwa, wala hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kuingilia kwenye lango hili. Litabaki limefungwa kwa sababu Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, ameingia kupitia lango hili.
3 Yeye aliye mkuu peke yake ndiye anayeweza kukaa penye njia ya hilo lango na kula chakula mbele za Mwenyezi Mungu. Itampasa aingie kwa njia hiyo ya lango la ukumbini na kutokea njia hiyo hiyo.”
4 Kisha yule mtu akanileta kwa njia ya lango la kaskazini mpaka mbele ya Hekalu. Nikatazama nami nikauona utukufu wa Mwenyezi Mungu ukilijaza Hekalu la Mwenyezi Mungu, nami nikaanguka kifudifudi.
5 Mwenyezi Mungu akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa uangalifu, usikilize kwa makini na uzingatie kila kitu ninachokuambia kuhusu masharti yote yanayohusu Hekalu la Mwenyezi Mungu. Uwe mwangalifu kuhusu wale wanaoruhusiwa hekaluni na wale wasioruhusiwa kuingia mahali patakatifu.
6 Iambie nyumba ya uasi ya Israeli, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Matendo yenu ya machukizo yatosha, ee nyumba ya Israeli!
7 Zaidi ya matendo yenu yote ya machukizo, mmewaleta wageni wasiotahiriwa mioyo na miili katika patakatifu pangu. Mmelinajisi Hekalu langu, huku mkinitolea chakula, mafuta ya wanyama na damu, nanyi mmevunja agano langu.
8 Badala ya kutimiza wajibu wenu kuhusiana na vitu vyangu vitakatifu, mmeweka watu wengine kuwa viongozi katika patakatifu pangu.
9 Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Hakuna mgeni asiyetahiriwa moyo na mwilini anayeruhusiwa kuingia patakatifu pangu, wala hata wageni wanaoishi miongoni mwa Waisraeli.
10 “ ‘Walawi walioniacha wakati Waisraeli walipopotoka wakatoka kwangu na kutangatanga kwa kufuata sanamu zao, sharti watachukua adhabu ya dhambi zao.
11 Wanaweza wakatumika katika mahali patakatifu pangu, wakiwa na uangalizi wa malango ya Hekalu; wanaweza kuchinja wanyama wa sadaka za kuteketezwa, na kutoa dhabihu kwa ajili ya watu, na kusimama mbele ya watu ili kuwahudumia.
12 Lakini kwa sababu walitumikia watu wakiwa mbele ya sanamu zao, na kuifanya nyumba ya Israeli ianguke kwenye dhambi, kwa hiyo nimeapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba ni lazima wachukue matokeo ya dhambi yao, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
13 Hawaruhusiwi kukaribia ili kunitumikia kama makuhani wala kukaribia chochote changu kilicho kitakatifu au sadaka iliyo takatifu kupita zote, bali watachukua aibu ya matendo yao ya kuchukiza.
14 Lakini nitawaweka katika uangalizi wa Hekalu na kazi zote zile zinazotakiwa kufanyika ndani yake.
15 “ ‘Lakini makuhani, ambao ni Walawi na wazao wa Sadoki, ambao walitimiza wajibu wao kwa uaminifu katika patakatifu pangu wakati Waisraeli walipopotoka, watakaribia ili kutumika mbele zangu. Itawapasa wasimame mbele zangu ili kutoa dhabihu za mafuta ya wanyama na damu, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
16 Wao peke yao ndio wenye ruhusa ya kuingia mahali patakatifu pangu. Wao peke yao ndio watakaokaribia meza yangu ili kuhudumu mbele zangu na kufanya utumishi wangu.
17 “ ‘Watakapoingia kwenye malango ya ukumbi wa ndani, watavaa nguo za kitani safi, hawaruhusiwi kamwe kuvaa mavazi ya sufu wakati wanapokuwa wakihudumu kwenye malango ya ukumbi wa ndani wala ndani ya Hekalu.
18 Watavaa vilemba vya kitani safi vichwani mwao na nguo za ndani za kitani safi viunoni mwao. Hawatavaa chochote kitakachowafanya kutoa jasho.
19 Watakapotoka ili kuingia katika ukumbi wa nje mahali watu walipo, watavua nguo walizokuwa wakihudumu nazo na wataziacha katika vyumba vitakatifu nao watavaa nguo nyingine, ili wasije wakaambukiza watu utakatifu kupitia mavazi yao.
20 “ ‘Hawatanyoa nywele za vichwa vyao wala kuziacha ziwe ndefu, bali watazipunguza.
21 Kuhani yeyote asinywe mvinyo aingiapo katika ukumbi wa ndani.
22 Wasioe wanawake wajane wala walioachika, inawapasa kuoa wanawake bikira wenye heshima wa Israeli au wajane wa makuhani.
23 Watawafundisha watu wangu tofauti kati ya vitu vitakatifu na vitu vya kawaida na kuwaonesha jinsi ya kupambanua kati ya vitu najisi na vitu safi.
24 “ ‘Katika magombano yoyote, makuhani watatumika kama mahakimu na kuamua hilo jambo kufuatana na sheria zangu. Watazishika sheria zangu na maagizo yangu katika sikukuu zangu zote zilizoamriwa, nao watatakasa Sabato zangu.
25 “ ‘Kuhani asijitie unajisi kwa kukaribia maiti; lakini, ikiwa mtu aliyekufa alikuwa baba yake au mama yake, mwana au binti yake, ndugu yake au dada ambaye hakuolewa, basi anaweza kujitia unajisi kwa hao.
26 Baada ya kujitakasa, atakaa hali hiyo kwa muda wa siku saba.
27 Siku atakapoingia katika ukumbi wa ndani wa mahali patakatifu ili kuhudumu, atatoa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
28 “ ‘Mimi ndio nitakuwa urithi pekee wa makuhani katika Israeli. Msiwape wao milki, mimi nitakuwa milki yao.
29 Wao watakula sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia na kila kitu kitakachotolewa kwa Mwenyezi Mungu katika Israeli kitakuwa chao.
30 Yote yaliyo bora ya malimbuko ya vitu vyote na matoleo yenu maalum vitakuwa vya makuhani. Inawapasa kuwapa malimbuko ya kwanza ya unga wenu ili baraka ipate kuwa katika nyumba zenu.
31 Makuhani hawaruhusiwi kula chochote, ikiwa ni ndege au mnyama, aliyekutwa amekufa au aliyeraruliwa na wanyama pori.
Mga kaugnay na talata
207
- 1Ezk 43:1, Ezk 40:6, Ezk 40:17, Ezk 42:14, Ezk 46:1, Ezk 43:4, 2Ch 4:9, Act 21:28–30
- 2Ezk 43:2–4, Exo 24:10, Isa 6:1–5
- 3Ezk 46:2, Ezk 37:25, Ezk 34:24, 1Co 10:18–33, Gen 31:54, Ezk 46:8–10, Ezk 40:9, 2Ch 34:31
- 4Ezk 1:28, Ezk 3:23, Rev 1:17, Ezk 40:20, Ezk 43:3–5, Hag 2:7, Ezk 40:40, Isa 6:3–4
- 5Ezk 40:4, Ezk 43:10–11, Deu 12:32, Deu 32:46, Mat 28:20, Pro 24:32, Psa 119:4, Exo 9:21
- 6Ezk 45:9, Ezk 3:9, 1Pe 4:3, Ezk 3:26–27, Ezk 2:5–8
- 7Lev 22:25, Jer 9:26, Jer 4:4, Lev 26:41, Gen 17:14, Ezk 44:9, Act 7:51, Mal 1:12–14
- 8Lev 22:2–33, Num 18:7, Ezr 8:24–30, Act 7:53, Ezk 44:16, 2Ti 4:1, 1Ti 6:13, Ezk 40:45–46
- 9Jol 3:17, Zec 14:21, Ezk 44:7, Jhn 3:3–5, Mrk 16:16, Psa 93:5, Tit 1:5–9, Psa 50:16
- 10Ezk 48:11, Ezk 22:26, 1Ti 5:22, 2Ki 23:8–9, Ezk 44:15, Neh 9:34, Lev 19:8, Zep 3:4
- 11Num 16:9, 2Ch 29:34, 2Ch 30:17, Ezk 40:45, Num 18:6, 1Ch 26:1–19, Ezk 44:14, 2Ch 35:10–11
- 12Psa 106:26, 2Ki 16:10–16, Ezk 14:3–4, Ezk 20:23, Ezk 44:10, Ezk 20:15, Isa 9:16, 1Sa 2:29–30
- 13Num 18:3, 2Ki 23:9, Ezk 32:20, Ezk 36:7, Ezk 16:61
- 141Ch 23:28–32, Num 18:4
- 15Deu 10:8, Ezk 48:11, Ezk 43:19, Ezk 44:7, Ezk 40:46, Zec 3:1–7, 2Ti 2:2, Lev 3:16–17
- 16Ezk 41:22, Mal 1:7, Num 18:7–8, Mal 1:12, Deu 33:8–10, Num 18:5, Rev 1:6
- 17Rev 19:8, Exo 28:43, Exo 39:27–29, Rev 4:4, Lev 16:4, Exo 28:39–40
- 18Exo 39:28, Exo 28:40–43, 1Co 14:40, Isa 3:20, Lev 16:4, 1Co 11:4–10
- 19Lev 6:27, Ezk 46:20, Lev 6:10–11, Exo 29:37, Exo 30:29, Mat 23:17–19, Ezk 42:13–14, 1Co 3:5–6
- 201Co 11:14, Lev 21:5–24, Num 6:5, Deu 14:1
- 21Lev 10:9, Tit 1:7–8, 1Ti 3:8, Luk 1:15, 1Ti 5:23
- 22Lev 21:7, Lev 21:13–14, 1Ti 3:2, 1Ti 3:11–12, 1Ti 3:4–5, Tit 1:6, Deu 24:1–4
- 23Ezk 22:26, Lev 10:10–11, 2Ti 2:24–25, Hos 4:6, Mal 2:6–9, Zep 3:4, Deu 33:10, Tit 1:9–11
- 241Ch 23:4, Ezk 22:26, 2Ch 19:8–10, Deu 17:8–13, Lev 23:1–44, Ezr 2:63, 1Ti 3:15, Num 28:1–29
- 25Lev 22:4, Luk 9:59–60, Mat 8:21–22, Lev 21:1–6, 1Th 4:13–15, 2Co 5:16
- 26Num 6:10–21, Heb 9:13–14, Num 19:11–14
- 27Num 6:9–11, Lev 8:14–36, Lev 4:3–35, Heb 7:26–28, Ezk 44:17
- 28Jos 13:33, Num 18:20, Deu 18:1–2, Deu 10:9, Ezk 45:4, Jos 13:14, 1Pe 5:2–4, Ezk 48:9–11
- 29Num 18:14, Lev 27:21, Lev 27:28, Lev 7:6, Lev 6:29, Lev 6:26, Lev 6:14–18, Heb 13:10
- 30Neh 10:35–37, Num 18:12–18, 2Ch 31:10, Deu 18:4, Num 15:19–21, Exo 23:19, Exo 22:29, Exo 13:12
- 31Lev 22:8, Exo 22:31, Deu 14:21, Rom 14:20, 1Co 8:13, Ezk 4:14, Lev 17:15