Ezekieli 45
1 “ ‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Mwenyezi Mungu kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa elfu ishirini na tano, na upana wake dhiraa elfu ishirini; eneo hili lote litakuwa takatifu.
2 Katika eneo hilo patakuwa na sehemu mraba ambayo ni ya mahali patakatifu; kila upande utakuwa dhiraa mia tano, ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa elfu ishirini na tano, na upana wa dhiraa elfu kumi. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, ndipo Patakatifu pa Patakatifu.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Mwenyezi Mungu. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
5 Eneo la urefu wa dhiraa elfu ishirini na tano, na upana wa dhiraa elfu kumi litakuwa la Walawi, wanaohudumu hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
6 “ ‘Utatoa mji kama mali yao, wenye upana wa dhiraa elfu tano, na urefu wa dhiraa elfu ishirini na tano karibu na sehemu takatifu; itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
7 “ ‘Mkuu anayetawala atakuwa na eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu kwa upande moja, na eneo la mji upande mwingine. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi, na kuenea mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki, sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawatawadhulumu tena watu wangu, bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
9 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
13 “ ‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: sehemu ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano, na sehemu ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja, kwa kuwa bathi kumi ni homeri moja).
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kila kundi la kondoo mia mbili katika malisho yenye maji mengi ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja katika kutoa sadaka hii maalum ya kutumiwa na mkuu anayetawala Israeli.
17 Utakuwa wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
18 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua; ndivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
21 “ ‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Mwenyezi Mungu na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali, na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
25 “ ‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
Mga kaugnay na talata
126
- 1Ezk 48:29, Num 34:13, Zec 14:20–21, Lev 25:23, Pro 3:9, Psa 16:5–6, Jos 14:2, Ezk 47:21–22
- 2Ezk 42:16–20, Ezk 27:28
- 3Ezk 48:10
- 4Ezk 40:45, Ezk 43:19, Num 16:5, Ezk 44:13–14, Ezk 48:10–11, Ezk 45:1, Ezk 44:28
- 5Ezk 48:13, 1Co 9:13–14, Ezk 48:10, Ezk 48:20, Ezk 40:17, 1Ch 9:26–33, Neh 10:38–39
- 6Ezk 48:15–18, Ezk 48:30–35
- 7Ezk 48:21, Ezk 46:16–18, Ezk 34:24, Ezk 37:24, Isa 9:5–6, Psa 2:8–9, Luk 1:32–33
- 8Isa 11:3–5, Ezk 46:18, Jer 23:5, Jos 11:23, Ezk 22:27, Isa 32:1–2, Zep 3:13, Isa 60:17–18
- 9Zec 8:16, Jer 22:3, Ezk 44:6, Isa 1:17, 1Pe 4:3, Job 24:2–12, Ezk 43:14–16, Luk 3:14
- 10Lev 19:35–36, Pro 20:10, Mic 6:10–11, Deu 25:15, Pro 11:1, Amo 8:4–6, Pro 16:11, Pro 21:3
- 11Isa 5:10
- 12Exo 30:13, Num 3:47, Lev 27:25
- 15Lev 1:4, Lev 6:30, Eph 2:16, Dan 9:24, Rom 5:10, Mal 1:14, Col 1:21, Heb 2:17
- 16Isa 16:1, Exo 30:14–15
- 172Ch 31:3, Isa 66:23, Ezk 46:4–12, Num 28:1–29, 1Ki 8:63–64, Lev 23:1–44, 2Ch 30:24, Ezk 43:27
- 18Lev 16:16, Lev 22:20, Exo 12:2, Heb 9:14, Ezk 43:22, Lev 16:33, Ezk 43:26, 1Pe 1:19
- 19Ezk 43:20, Lev 16:18–20, Ezk 43:14, Ezk 43:17
- 20Psa 19:12, Ezk 45:18, Ezk 45:15, Lev 16:20, Lev 4:27–35, Heb 5:2, Rom 16:18–19
- 21Lev 23:5–8, Num 9:2–14, 1Co 5:7–8, Exo 12:1–51, Num 28:16–25, Deu 16:1–8
- 22Lev 4:14, Mat 26:26–28, 2Co 5:21, Mat 20:28
- 23Job 42:8, Lev 23:8, Num 23:1–2, Num 28:15–31, Heb 10:8–12, Num 29:5, Num 29:11–38
- 24Ezk 46:5–7, Num 28:12–15
- 25Lev 23:33–43, Num 29:12–38, 2Ch 5:3, Jhn 7:37–39, Neh 8:14–18, Deu 16:13–15, Jhn 7:2, 2Ch 7:8–10