Amosi 6
1 Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
2 Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
3 Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
4 Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
5 Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
6 Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yusufu.
7 Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
8 Bwana Mungu Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilicho ndani yake.”
9 Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
10 Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza! Haturuhusiwi kutaja jina la Mwenyezi Mungu.”
11 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
12 Je, farasi wanaweza kukimbia kwenye miamba iliyochongoka? Je, mtu aweza kulima kwa maksai huko? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
13 ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
14 Maana Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”
Marejeleo mtambuka
112
- 1Isa 32:9–11, Jas 5:5, Luk 12:17–20, Amo 4:1, Exo 19:5–6, Jdg 18:7, Zep 1:12, Jas 1:18
- 2Nam 3:8, 2Ki 18:34, Gen 10:10, 2Ch 26:6, 1Sa 17:4, Isa 10:9–11, 2Ki 17:30, Isa 37:12–13
- 3Amo 9:10, Isa 56:12, Ezk 12:27, Amo 3:10, 2Pe 3:4, 1Th 5:3, Mat 24:48, Ezk 12:22
- 4Amo 3:12, Jas 5:5, Ezk 34:2–3, Psa 73:7, Isa 22:13, 1Sa 25:36–38, Isa 5:11–12, Luk 16:19
- 5Isa 5:12, Amo 5:23, Amo 8:3, 1Pe 4:3, Job 21:11–12, 1Ch 15:16, Rev 18:22, Gen 31:27
- 6Gen 49:22, 2Ki 15:29, Jhn 12:3, Ezk 9:4, Jer 30:7, Hos 3:1, Gen 42:21–22, Amo 2:8
- 7Amo 7:11, Amo 5:5, 1Ki 20:16–20, Dan 5:4–6, Est 7:1–2, Amo 5:27, Est 5:12–14, Amo 7:17
- 8Jer 51:14, Amo 4:2, Jer 22:5, Amo 8:7, Psa 47:4, Amo 3:11, Psa 106:40, Psa 50:12
- 9Amo 5:3, Job 1:19, 1Sa 2:33, Est 5:11, Job 1:2, Isa 14:21, Job 20:28, Est 9:10
- 101Sa 31:12, Amo 8:3, Ezk 20:39, Amo 5:13, Jer 44:26, Jer 16:6, Ezk 24:21, Num 17:12
- 11Amo 3:15, Isa 55:11, 2Ki 25:9, Zec 14:2, Amo 9:9, Nam 1:14, Amo 6:8, Luk 19:44
- 12Amo 5:7, Hos 10:4, Isa 59:13–14, Amo 5:11–12, Psa 94:20–21, 1Ki 21:7–13, Isa 48:4, Jer 6:29–30
- 13Isa 28:14–15, Luk 12:19–20, 2Ki 14:25, Jas 4:16, Job 8:15, Hab 1:15–16, Isa 7:4, 2Ch 28:6–8
- 142Ki 14:25, 1Ki 8:65, Jer 5:15–17, 2Ki 15:29, Hos 10:5, Isa 7:20, 2Ki 17:6, Num 34:7–8
Mada katika sura hii
32
Amusements and Worldly Pleasures, Anointing, Bed, Calneh, Church, Confidence, Conscience, Cremation, David, Drunkenness, Eating, Feasts, Gath, Gluttony, Hamath, Happiness, Hemath, Hemlock, Horn, Invention, Israel, Prophecies Concerning, Ivory, Music, Ointment, Pleasure, Rich, the, Rulers, Security, Self-Righteousness, War, Wine, Worldliness