Ezekieli 9
1 Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
2 Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu linalotazama kaskazini, kila mmoja akiwa na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Kati yao palikuwa na mtu aliyevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi kiunoni mwake. Wakaingia ndani ya Hekalu na kusimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
3 Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Mwenyezi Mungu akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi na mwenye vifaa vya mwandishi kiunoni mwake,
4 akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama kwenye paji za nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
5 Nikiwa ninasikiliza, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
6 Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wamama na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
7 Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze ua zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda, wakaanza kuua watu mjini kote.
8 Walipokuwa wakiwaua watu, nami nikaachwa peke yangu, nilisujudu, nikapaza sauti na kusema, “Ee Bwana Mungu Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
9 Mwenyezi Mungu akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Mwenyezi Mungu ameiacha nchi; Mwenyezi Mungu haoni.’
10 Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwarehemu, lakini nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyoyatenda.”
11 Ndipo mtu yule aliyevaa nguo ya kitani na mwenye vifaa vya mwandishi kiunoni mwake akarudi na kutoa taarifa, akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”
Перекрёстные ссылки
80
- 1Isa 6:8, Rev 1:10–11, Ezk 43:6–7, 1Ch 21:15, 2Ki 10:24, Amo 3:7–8, Rev 14:7, Exo 12:23
- 2Ezk 10:2, Lev 16:4, Rev 15:6, 2Ki 15:35, Ezk 10:6–7, Jer 8:16–17, Jer 26:10, Exo 27:1–7
- 3Ezk 10:4, Ezk 11:22–23, Ezk 3:23, Ezk 43:2–4, Ezk 8:4
- 4Rev 9:4, 2Co 1:22, Rev 14:1, Rev 7:2–3, Rev 20:4, 2Ti 2:19, Eph 4:30, Psa 119:136
- 5Ezk 5:11, Ezk 9:10, Deu 32:39–42, 1Sa 9:15, Num 25:7–8, Ezk 24:14, Isa 22:14, 1Ki 18:40
- 6Rev 9:4, Exo 12:23, Jer 25:29, 2Ti 2:19, 1Pe 4:17–18, Rev 7:3, 2Ch 36:17, Luk 12:47
- 72Ch 36:17, Ezk 7:20–22, Psa 79:1–3, Luk 13:1, Lam 2:4–7
- 8Ezk 11:13, Num 14:5, Ezk 4:14, 1Ch 21:16, Jos 7:6, Num 16:45, Jer 4:10, Num 16:4
- 9Ezk 8:12, Job 22:13, Ezk 7:23, 2Ch 36:14–16, 2Ki 21:16, Psa 10:11, Psa 94:7, Mic 3:1–3
- 10Ezk 7:4, Isa 65:6, Ezk 8:18, Ezk 11:21, Ezk 5:11, Hos 9:7, Ezk 7:8–9, Jol 3:4
- 11Rev 16:17, Zec 1:10–11, Isa 46:10–11, Psa 103:20, Zec 6:7–8, Rev 16:2