1 Wafalme 17
1 Basi Ilya Mtishbi, kutoka Tishbi katika Gileadi, akamwambia Ahabu, “Kama Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli ninayemtumikia, aishivyo, hapatakuwa na umande wala mvua katika miaka kadhaa ijayo, isipokuwa kwa neno langu.”
2 Kisha neno la Mwenyezi Mungu likamjia Ilya, kusema,
3 “Ondoka hapa, elekea upande wa mashariki ukajifiche karibu na Kijito cha Kerithi, mashariki mwa Yordani.
4 Utakunywa maji kutoka kile kijito, nami nimeagiza kunguru wakulishe huko.”
5 Naye akafanya kama alivyoambiwa na Mwenyezi Mungu. Akaenda katika Kijito cha Kerithi, mashariki mwa Yordani na akakaa huko.
6 Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi, na mkate na nyama jioni, naye akanywa maji kutoka kile kijito.
7 Baada ya muda, kile kijito kikakauka kwa sababu mvua haikuwa imenyesha katika nchi.
8 Kisha neno la Mwenyezi Mungu likamjia Ilya, kusema,
9 “Ondoka, uende Sarepta ya Sidoni, ukae huko. Nimemwagiza mjane wa huko ili akuhudumie.”
10 Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, alimkuta mjane akiokota kuni pale. Akamwita na kumwambia, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.”
11 Alipokuwa anaenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.”
12 Akamjibu, “Hakika kama Mwenyezi Mungu, Mungu wako, aishivyo, sina mkate wowote, isipokuwa konzi moja ya unga kwenye chungu, na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili tule, kiishe, tukafe.”
13 Ilya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unitengenezee mkate mdogo kutoka vile ulivyo navyo kisha uniletee na ndipo utayarishe chochote kwa ajili yako na mwanao.
14 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli: ‘Kile chungu cha unga hakitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile Mwenyezi Mungu atakapoleta mvua juu ya nchi.’ ”
15 Akaondoka na kufanya kama Ilya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Ilya, yule mwanamke na jamaa yake.
16 Kwa kuwa kile chungu hakikuisha unga na ile chupa ya mafuta haikukauka sawasawa na lile neno la Mwenyezi Mungu lililonenwa na Ilya.
17 Baada ya muda, mwana wa yule mwanamke mwenye nyumba akaugua. Hali yake ikaendelea kuwa mbaya sana, na hatimaye akaacha kupumua.
18 Yule mjane akamwambia Ilya, “Una nini dhidi yangu, ewe mtu wa Mungu? Umekuja ili kunikumbusha dhambi yangu, na kusababisha kifo cha mwanangu?”
19 Ilya akamjibu, “Nipe mwanao.” Ilya akampokea kutoka kifuani mwake, akambeba hadi chumba cha juu alipokuwa anaishi, akamlaza kitandani pake.
20 Kisha akamlilia Mwenyezi Mungu, akasema “Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wangu, je, pia umeleta msiba juu ya mjane huyu ninayeishi kwake, kwa kusababisha mwanawe kufa?”
21 Kisha akajinyoosha juu ya kijana mara tatu na kumlilia Mwenyezi Mungu, akisema, “Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wangu, nakuomba roho ya huyu kijana imrudie!”
22 Mwenyezi Mungu akasikia kilio cha Ilya, na roho ya kijana ikamrudia, naye akafufuka.
23 Ilya akamtwaa kijana na kumbeba kutoka chumba chake cha juu, akamshusha, akampa mama yake na kusema, “Tazama, mwanao yu hai!”
24 Ndipo yule mwanamke akamwambia Ilya, “Sasa ninajua kwamba wewe ni mtu wa Mungu, na kwamba neno la Mwenyezi Mungu kutoka kinywani mwako ni kweli.”
Перекрёстные ссылки
160
- 1Luk 4:25–26, Jas 5:17, Luk 1:17, 1Ki 22:14, 2Ki 3:14, Rom 11:2, Deu 10:8, Rev 11:6
- 2Jer 11:1, Jer 18:1, 1Ki 12:22, Hos 1:1–2, Jer 7:1, 1Ch 17:3
- 3Psa 83:3, Rev 12:6, Rev 12:14, Jer 36:26, Jer 36:19, Jhn 8:59, 1Ki 22:25, Heb 11:38
- 41Ki 17:9, Psa 147:9, Mat 4:4, Job 38:41, 1Ki 19:5–8, Psa 33:8–9, Mat 4:11, Job 34:29
- 5Jhn 15:14, Pro 3:5, Mat 16:24, 1Ki 19:9
- 6Psa 78:23–24, Mat 6:31–33, Psa 78:15–16, Jer 37:21, Mat 14:19–21, Luk 22:35, Mat 19:26, Psa 34:9–10
- 7Isa 54:10, Isa 40:30–31
- 8Gen 22:14, Isa 41:17, 1Ki 17:2, Heb 13:6
- 9Luk 4:26, Oba 1:20, 2Co 4:7, Mat 15:21–22, 1Ki 17:4, Rom 4:17–21, Jdg 7:4, Jdg 7:2
- 10Gen 24:17, Jhn 4:7, 2Co 11:27, Gen 21:15, Heb 11:37
- 11Mat 10:42, 1Ki 17:9, Mat 25:35–40, 1Ki 18:4, Heb 13:2, Gen 24:18–19, Gen 18:5
- 12Mat 15:33–34, 1Ki 17:1, Gen 21:16, 2Ki 4:2–7, Ezk 12:18–19, Lam 4:9, Jer 5:2, 1Sa 25:26
- 13Mal 3:10, Mat 6:33, Exo 14:13, Pro 3:9, Isa 41:13, Act 27:24, 2Ki 6:16, 1Pe 1:7
- 14Mat 15:36–38, Mat 14:17–20, 2Ki 4:42–44, 2Ki 3:16, 2Ki 7:1, 2Ki 9:6, 1Ki 17:4, 2Ki 4:2–7
- 15Mat 15:28, Gen 6:22, Mrk 12:43, Heb 11:17, Rom 4:19–20, 2Ch 20:20, Gen 22:3, Jhn 11:40
- 16Mat 9:28–30, Jhn 4:50–51, Luk 1:37, Luk 1:45, 1Ki 16:12, 1Ki 13:5, Mat 19:26
- 17Jas 1:2–4, 2Ki 4:18–20, Zec 12:10, Jhn 11:14, Jas 1:12, Dan 5:23, Psa 104:29, 1Pe 4:12
- 18Luk 5:8, Jhn 2:4, Luk 4:34, 2Ki 3:13, 2Sa 16:10, Gen 42:21–22, 2Sa 19:22, Job 13:26
- 192Ki 4:32, 2Ki 4:10, Act 9:37, 2Ki 4:21
- 20Jas 5:15–18, Mat 21:22, 2Ki 19:15, Exo 17:4, 1Sa 7:8–9, 1Ki 18:36–37, Gen 18:23–25, Psa 99:6
- 21Act 20:10, Act 9:40, 2Ki 4:33–35, Heb 11:19, Act 10:10
- 22Rev 11:11, Deu 32:39, Rom 14:9, Jhn 5:28–29, Heb 11:35, Jhn 11:43, 2Ki 13:21, 1Sa 2:6
- 232Ki 4:36–37, Act 9:41, Luk 7:15, Heb 11:35
- 24Jhn 16:30, Jhn 3:2, Jhn 2:11, Jhn 4:42–48, 1Th 2:13, 1Jn 2:21, Ecc 12:10, Jhn 15:24
Темы в этой главе
34
Barrel, Blessing, Bread, Canaan, Cherith, Children, Conviction, Dead (People), Dew, Drought, Elijah, Faith, Famine, Frugality, Gilead, God, Hospitality, House, Intercession, Israel, Prophecies Concerning, Minister, Christian, Miracles, Oil, Poor, Prayer, Prophecy, Prophets, Raven, Readings, Select, Self-Denial, Shield, Widow, Women, Zarephath