Hosea 12
1 Efraimu anajilisha upepo; hufukuzia upepo wa mashariki kutwa nzima na kuzidisha uongo na jeuri. Anafanya mkataba na Ashuru na kutuma mafuta ya zeituni Misri.
2 Mwenyezi Mungu analo shtaka dhidi ya Yuda, atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake na kumlipa kwa kadiri ya matendo yake.
3 Yakobo akiwa tumboni alishika kisigino cha kaka yake; kama mwanadamu, alishindana na Mungu.
4 Alishindana na malaika na kumshinda; alilia na kuomba upendeleo wake. Alimkuta huko Betheli na kuzungumza naye huko:
5 Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, Mwenyezi Mungu ndilo jina lake!
6 Lakini ni lazima urudi kwa Mungu wako; dumisha upendo na haki, nawe umngojee Mungu wako siku zote.
7 Mfanyabiashara hutumia vipimo vya udanganyifu; hupenda kupunja.
8 Efraimu hujisifu akisema, “Mimi ni tajiri sana; nimetajirika. Pamoja na utajiri wangu wote hawatakuta ndani yangu uovu wowote au dhambi.”
9 “Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, niliyewaleta kutoka Misri; nitawafanya mkae tena kwenye mahema, kama vile katika siku za sikukuu zenu zilizoamriwa.
10 Niliongea na manabii, nikawapa maono mengi na kusema mifano kupitia wao.”
11 Je, Gileadi si mwovu? Watu wake hawafai kitu! Je, hawatoi dhabihu za mafahali huko Gilgali? Madhabahu zao zitakuwa kama malundo ya mawe katika shamba lililolimwa.
12 Yakobo alikimbilia katika nchi ya Aramu; Israeli alitumika ili apate mke, ili aweze kulipa kwa ajili yake alichunga kondoo.
13 Mwenyezi Mungu alimtumia nabii kumpandisha Israeli kutoka Misri, kupitia kwa nabii alimtunza.
14 Lakini Efraimu amemchochea sana hasira; Bwana wake ataleta juu yake hatia yake ya kumwaga damu naye atamlipiza kwa ajili ya dharau yake.
Références croisées
103
- 1Hos 11:12, Ezk 17:10, Hos 8:7, Jer 22:22, Hos 5:13, 2Ki 15:19, Job 15:2, 2Ki 17:4–6
- 2Mic 6:2, Isa 10:6, Hos 4:1, Jer 3:8–11, Isa 3:11, Jer 25:31, Hos 2:13, Isa 8:7–8
- 3Gen 25:26, Rom 9:11, Gen 32:24–28, Jas 5:16–18
- 4Gen 35:15, 1Th 4:17, Mal 3:1, Gen 48:15, Exo 3:2–5, Heb 6:13–18, Heb 5:7, Act 7:30–35
- 5Exo 3:15, Psa 135:13, Isa 42:8, Gen 28:16, Gen 32:30
- 6Mic 6:8, Mic 7:7, Lam 3:25–26, Hos 14:1, Act 2:38, Zec 7:9, Hos 6:1–3, Psa 37:7
- 7Pro 11:1, Mic 6:10–11, Amo 8:5–6, 1Sa 12:3, Mal 3:5, Jas 5:4, Amo 4:1, Zec 14:21
- 8Rev 3:17, Psa 62:10, Deu 8:17, Psa 49:6, Psa 52:7, Job 31:24–25, 1Ti 6:5, Pro 30:20
- 9Lev 23:40–43, Neh 8:15–17, Psa 81:10, 2Sa 7:2, Hos 13:4, Jer 35:7, Ezr 3:4, Lev 26:13
- 102Ki 17:13, Ezk 20:49, Jer 19:1, Isa 20:2–5, Jer 7:25, Jol 2:28, Amo 7:14, 1Ki 19:10
- 11Hos 6:8, Hos 4:15, Hos 8:11, Hos 9:15, Hos 10:1, Jon 2:8, Jer 10:8, Jer 10:15
- 12Gen 29:18–28, Gen 31:41, Gen 28:1–22, Gen 27:43, Deu 26:5, Gen 32:27–28
- 13Act 3:22–23, Psa 77:20, Exo 12:50–51, Isa 63:11–14, Act 7:35–37, Exo 13:3, Amo 2:11–12, Mic 6:4
- 14Ezk 18:13, Dan 11:18, 2Ki 17:7–18, Ezk 23:2–10, Deu 28:37, Hos 7:16, 1Ki 2:33–34, 1Sa 2:30
Thèmes dans ce chapitre
33
Alliances, Balances, Beth-El, Commerce, Confidence, Dishonesty, Ephraim, Gilead, Gilgal, Idolatry, Israel, Israel, Prophecies Concerning, Jacob, Jesus, the Christ, Judgment, Marriage, Measure, Merchant, Mercy, Moses, Oil, Perseverance, Prayer, Prophets, Repentance, Riches, Self-Delusion, Self-Righteousness, Similitude, Sin, Vision, Waiting, Wicked (People)