Hosea 11
1 “Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda; nilimwita mwanangu kutoka Misri.
2 Lakini kadiri nilivyomwita Israeli, ndivyo walivyoenda mbali nami. Walitoa dhabihu kwa Mabaali na kufukiza uvumba kwa vinyago.
3 Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea, nikiwashika mikono; lakini hawakutambua kuwa ni mimi niliyewaponya.
4 Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu, kwa vifungo vya upendo; niliondoa nira shingoni mwao nami nikainama kuwalisha.
5 “Je, hawatarudi Misri, nayo Ashuru haitawatawala kwa sababu wamekataa kutubu?
6 Upanga utavurumishwa katika miji yao, nao utaharibu makomeo ya malango yao na kukomesha mipango yao.
7 Watu wangu wamedhamiria kuniacha. Hata wakimwita Yeye Aliye Juu Sana, kwa vyovyote hatawainua.
8 “Efraimu, ninawezaje kukuacha? Ee Israeli, ninawezaje kukutoa? Nitawezaje kukutendea kama Adma? Nitawezaje kukufanya kama Seboimu? Moyo wangu umegeuka ndani yangu, huruma zangu zote zimeamshwa.
9 Sitatimiza hasira yangu kali, wala sitageuka na kumharibu Efraimu. Kwa kuwa mimi ndimi Mungu, wala si mwanadamu, Aliye Mtakatifu miongoni mwenu. Sitakuja kwa ghadhabu.
10 Watamfuata Mwenyezi Mungu; atanguruma kama simba. Anaponguruma, watoto wake watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.
11 Watakuja wakitetemeka kama ndege wakitoka Misri, kama hua wakitoka Ashuru. Nitawafanya waishi katika nyumba zao,” asema Mwenyezi Mungu.
12 Efraimu amenizunguka kwa uongo, nyumba ya Israeli kwa udanganyifu. Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu, hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.
Références croisées
96
- 1Mat 2:15, Exo 4:22, Hos 13:4, Hos 2:15, Jer 2:2, Hos 12:13, Ezk 16:6, Mal 1:2
- 2Jer 18:15, Hos 2:13, Isa 65:7, Hos 11:7, Jhn 3:19, Act 7:51, 2Ki 17:13–16, Hos 13:1–2
- 3Jer 30:17, Deu 1:31, Exo 15:26, Hos 7:15, Hos 14:4, Exo 23:25, Act 13:18, Deu 8:2
- 4Jhn 12:32, Lev 26:13, 2Co 5:14, Psa 78:23–25, Jer 31:2–3, Hos 2:8, 2Sa 7:14, Isa 63:9
- 5Hos 7:16, Hos 8:13, Hos 10:6, 2Ki 17:13–14, Hos 9:3, Amo 4:6, Hos 9:6, Jer 8:4–6
- 6Hos 13:16, Hos 10:6, Hos 10:14, Psa 106:43, Isa 30:1, Lev 26:33, Psa 106:39, Isa 18:5
- 7Jer 8:5, Amo 5:4–6, Amo 5:14–15, Jer 3:11, Pro 14:14, Hos 7:16, Hos 11:2, Jer 3:6–8
- 8Jer 31:20, Mat 23:37, Hos 6:4, Deu 32:36, Deu 29:23, Jud 1:7, Amo 4:11, 2Sa 24:16
- 9Num 23:19, Isa 55:8–9, Mic 7:18–20, Isa 12:6, Jer 30:11, Mal 3:6, Ezk 37:27–28, Hos 14:4
- 10Jol 3:16, Isa 31:4, Amo 1:2, Jer 25:30, Isa 64:2, Jer 31:9, Zec 8:7, 2Pe 2:10
- 11Isa 11:11, Isa 60:8, Zec 10:10, Hos 7:11, Amo 9:14–15, Ezk 37:25, Ezk 37:21, Ezk 28:25–26
- 121Co 6:2, Isa 44:20, Rev 1:6, 2Ch 29:1–32, Hos 12:7, Isa 29:13, Rev 3:21, Mic 6:12