Kutoka 15
1 Ndipo Musa na Waisraeli wakamwimbia Mwenyezi Mungu wimbo huu: “Nitamwimbia Mwenyezi Mungu, kwa kuwa ametukuzwa sana. Farasi na mpanda farasi amewatosa baharini.
2 “Mwenyezi Mungu ni nguvu zangu na wimbo wangu; amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu, Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.
3 Mwenyezi Mungu ni shujaa wa vita; Mwenyezi Mungu ndilo jina lake.
4 Magari ya vita ya Farao na jeshi lake amewatosa baharini. Maafisa wa Farao walio bora sana wamezamishwa katika Bahari ya Shamu.
5 Maji yenye kina yamewafunika, wamezama vilindini kama jiwe.
6 Mkono wako wa kuume, Ee Mwenyezi Mungu ulitukuka kwa uweza. Mkono wako wa kuume, Ee Mwenyezi Mungu, ukamponda adui.
7 “Katika ukuu wa utukufu wako, ukawaangusha chini wale waliokupinga. Uliachia hasira yako kali, ikawateketeza kama kapi.
8 Kwa pumzi ya pua yako maji yalijilundika. Mawimbi ya maji yakasimama imara kama ukuta, vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari.
9 Adui alijivuna, ‘Nitawafuatia, nitawapata. Nitagawanya nyara; nitajishibisha kwao. Nitafuta upanga wangu na mkono wangu utawaangamiza.’
10 Lakini ulipuliza kwa pumzi yako, bahari ikawafunika. Wakazama kama risasi kwenye maji makuu.
11 Ni nani miongoni mwa miungu aliye kama wewe, Ee Mwenyezi Mungu? Ni nani kama Wewe: uliyetukuka katika utakatifu, utishaye katika utukufu, ukitenda maajabu?
12 “Uliunyoosha mkono wako wa kuume na nchi ikawameza.
13 Katika upendo wako usiokoma utawaongoza watu uliowakomboa. Katika nguvu zako utawaongoza hadi makao yako matakatifu.
14 Mataifa watasikia na kutetemeka, uchungu utawakamata Wafilisti.
15 Wakuu wa Edomu wataogopa, viongozi wa Moabu watatetemeka kwa hofu, Wakanaani watayeyuka,
16 vitisho na hofu vitawaangukia. Kwa nguvu ya mkono wako watatulia kama jiwe, hadi watu wako wapite, Ee Mwenyezi Mungu, hadi watu uliowanunua wapite.
17 Utawaingiza na kuwapandikiza juu ya mlima wa urithi wako: hapo mahali, Ee Mwenyezi Mungu, ulipopafanya kuwa makao yako, mahali patakatifu, Ee Mwenyezi Mungu, ulipopajenga kwa mikono yako.
18 “Mwenyezi Mungu atatawala milele na milele.”
19 Farasi wa Farao, magari yake ya vita na wapanda farasi wake walipoingia baharini, Mwenyezi Mungu aliyarudisha maji ya bahari yakawafunika, lakini Waisraeli walipita baharini mahali pakavu.
20 Kisha Miriamu yule nabii mke, ndugu yake Haruni, akachukua matari mkononi mwake na wanawake wote wakamfuata na matari yao wakicheza.
21 Miriamu akawaimbia: “Mwimbieni Mwenyezi Mungu, kwa maana ametukuka sana. Farasi na mpanda farasi amewatosa baharini.”
22 Kisha Musa akawaongoza Israeli kutoka Bahari ya Shamu na kuingia katika Jangwa la Shuri. Kwa siku tatu walisafiri jangwani bila kupata maji.
23 Walipofika Mara, hawakuweza kunywa maji yake kwa sababu yalikuwa machungu. (Ndiyo sababu mahali hapo panaitwa Mara.)
24 Kwa hiyo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, “Tunywe nini?”
25 Ndipo Musa akamlilia Mwenyezi Mungu, naye Mwenyezi Mungu akamwonesha kipande cha mti. Akakitupa ndani ya maji, nayo maji yakawa matamu. Huko Mwenyezi Mungu akawapa amri na sheria na huko akawajaribu.
26 Mungu akasema, “Mkisikiliza kwa makini sauti ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, na kuyafanya yaliyo mema machoni pake, na mkiyatii maagizo yake na kuzishika amri zake zote, sitaleta juu yenu ugonjwa wowote niliowaletea Wamisri, kwa kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, niwaponyaye.”
27 Kisha wakafika Elimu, mahali palipokuwa na chemchemi kumi na mbili, na miti sabini ya mitende, wakapiga kambi huko karibu na maji.
Références croisées
186
- 1Rev 15:3, Exo 15:21, Psa 106:12, Isa 12:1–6, Isa 51:10–11, Psa 107:8, Psa 107:21–22, Exo 18:11
- 2Isa 12:2, Psa 118:14, Psa 18:46, Psa 59:17, Isa 25:1, Psa 140:7, Psa 18:1–2, Psa 99:9
- 3Psa 24:8, Exo 14:14, Rev 19:11–21, Isa 42:8, Psa 83:18, Exo 6:6–8, Psa 45:3, Exo 3:15
- 4Exo 14:13–28, Exo 14:6–7
- 5Neh 9:11, Exo 14:28, Exo 15:10, Jer 51:63–64, Ezk 27:34, Mat 18:6, Mic 7:19, Jon 2:2
- 6Psa 118:15–16, Isa 51:9, Psa 2:9, 1Ch 29:11–12, Psa 60:5, Rev 2:27, Isa 52:10, Mat 6:13
- 7Mal 4:1, Isa 5:24, Isa 47:14, Isa 5:16, Psa 83:13, Isa 37:29, Deu 33:26, Psa 148:13
- 8Job 4:9, Psa 78:13, Exo 14:21–22, Hab 3:10, Isa 11:4, 2Sa 22:16, Isa 37:7, 2Th 2:8
- 9Jdg 5:30, Exo 14:5, Isa 53:12, Luk 11:22, Hab 3:14, Gen 49:27, Isa 36:20, 1Ki 20:10
- 10Deu 11:4, Exo 15:5, Exo 14:21, Mat 8:27, Isa 11:15, Exo 14:27–28, Amo 4:13, Psa 135:7
- 111Ki 8:23, Psa 89:5–8, 1Sa 2:2, 2Sa 7:22, Rev 4:8, Isa 6:3, Jer 10:6–7, Deu 3:24
- 12Exo 15:6
- 13Psa 77:20, 1Pe 1:5, Psa 77:14–15, Psa 78:52–54, Psa 106:9, Jer 2:6, Isa 63:12–13, Eph 2:4
- 14Deu 2:25, Jos 2:9–10, Psa 48:6, Num 14:14, Jos 9:24, Isa 14:31, Isa 14:29, Deu 2:4–5
- 15Jos 5:1, Jos 2:9, Jos 2:11, Psa 68:2, Gen 36:40, Deu 2:4, Deu 20:8, 1Ch 1:51–54
- 16Psa 74:2, Deu 2:25, 1Sa 25:37, Jos 2:9, Isa 43:1–3, 1Pe 2:9, Jer 31:11, Tit 2:14
- 17Psa 44:2, Psa 80:8, Psa 78:54–55, Jer 32:41, Psa 78:68–69, Isa 5:1–4, Psa 132:13–14, Jer 2:21
- 18Psa 29:10, Psa 10:16, Isa 57:15, Dan 2:44, Psa 146:10, Rev 11:15–17, Dan 7:27, Dan 4:3
- 19Exo 14:28–29, Heb 11:29, Exo 14:22–23, Pro 21:31
- 20Psa 150:4, 1Sa 18:6, Psa 68:25, Psa 149:3, Jdg 11:34, Jdg 4:4, Mic 6:4, Psa 81:2
- 21Exo 15:1, Rev 15:3, Rev 7:10–12, Rev 5:9, Rev 19:1–6, Psa 134:1–3, 2Ch 5:13, Isa 5:1–30
- 22Gen 16:7, Gen 25:18, Exo 3:18, 1Sa 15:7
- 23Num 33:8, Rut 1:20
- 24Exo 16:2, Exo 14:11, Num 20:2–5, Psa 78:19–20, Num 14:1–4, Num 11:1–6, Exo 17:3–4, Num 16:11
- 25Deu 8:2, Psa 66:10, Jdg 3:1, Jdg 3:4, Jdg 2:22, Deu 8:16, 2Ki 2:21, Exo 16:4
- 26Psa 103:3, Deu 7:15, Exo 23:25, Psa 41:3–4, Psa 147:3, Jer 33:6, Deu 28:1–15, Hos 6:1
- 27Rev 22:2, Rev 7:17, Num 33:9, Isa 12:3, Ezk 47:12
Thèmes dans ce chapitre
48
Arm, Bitter Water, Blasting, Blessing, Canaan, Children, Dancing, Diligence, Disease, Duke, Edomites, Elim, Epic, Evil for Good, Faith, Glory, God, Horse, Israel, Joy, Lead, Marah, Meekness, Miracles, Miriam, Moses, Murmuring, Music, Ordinance, Panic, Poetry, Power, Praise, Prayer, Prophetesses, Psalms, Readings, Select, Red Sea, Salvation, Shur, Song, Stubble, Thankfulness, Timbrel, Trouble, War, Women, Worship