Waamuzi 17
1 Palikuwa na mtu aliyeitwa Mika kutoka nchi ya vilima ya Efraimu.
2 Akamwambia mama yake, “Zile shekeli elfu moja na mia moja za fedha zilizochukuliwa kwako, ambazo nilisikia ukizinenea maneno ya laana, hizi hapa; mimi ndiye niliyezichukua.” Ndipo mama yake akamwambia, “Mwenyezi Mungu na akubariki, mwanangu.”
3 Alipozirudisha zile shekeli elfu moja na mia moja za fedha kwa mama yake, mama yake akamwambia, “Mimi nimeiweka fedha hii wakfu kwa Mwenyezi Mungu ili mwanangu atengeneze sanamu ya kuchonga, na sanamu ya kusubu. Mimi nitakurudishia wewe.”
4 Hivyo akamrudishia mama yake ile fedha, naye mama yake akachukua shekeli mia mbili za hiyo fedha na kumpa mfua fedha, ambaye aliifanyiza kinyago na sanamu. Navyo vikawekwa ndani ya nyumba ya Mika.
5 Basi Mika alikuwa na mahali pa ibada za sanamu. Akatengeneza kizibau, pamoja na miungu ya nyumbani, na kumweka mmoja wa wanawe kuwa kuhani wake.
6 Katika siku hizo, Waisraeli hawakuwa na mfalme; kila mtu alifanya alivyoona ni vyema machoni pake.
7 Palikuwa na kijana Mlawi kutoka Bethlehemu ya Yuda, aliyekuwa akiishi miongoni mwa watu wa kabila la Yuda.
8 Huyu kijana akatoka mji huo wa Bethlehemu ya Yuda na kutafuta mahali pengine pa kuishi. Alipokuwa akisafiri, akafika nyumbani kwa Mika katika nchi ya vilima ya Efraimu.
9 Mika akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Mimi ni Mlawi kutoka Bethlehemu ya Yuda, ninatafuta mahali pa kuishi.”
10 Ndipo Mika akamwambia, “Ishi pamoja nami, uwe baba yangu na kuhani wangu, nami nitakupa shekeli kumi za fedha kila mwaka, pamoja na nguo na chakula.”
11 Hivyo yule Mlawi akakubali kuishi pamoja na Mika, naye akawa kama mmoja wa wanawe.
12 Basi Mika akamweka wakfu huyo kijana Mlawi, naye huyo akawa kuhani wake na kuishi nyumbani mwake.
13 Mika akasema, “Sasa najua Mwenyezi Mungu atanitendea mema, kwa kuwa Mlawi huyu amekuwa kuhani wangu.”
Cross-references
69
- 1Jdg 10:1, Jdg 18:2, Jos 15:9, Jos 17:14–18
- 2Neh 13:25, Rut 3:10, 1Sa 23:21, Mat 26:74, 2Jn 1:11, Deu 27:16, 1Sa 26:19, Jer 48:10
- 3Lev 19:4, Exo 20:4, Exo 20:23, Jdg 18:5, Jhn 16:2, Jdg 17:13, Hab 2:18–19, Isa 40:18–25
- 4Isa 46:6–7, Jer 10:9–10
- 5Jdg 8:27, Jdg 18:14, Gen 31:30, Gen 31:19, Jdg 18:24, Hos 3:4, Exo 28:15, Exo 29:9
- 6Deu 12:8, Pro 14:12, Pro 12:15, Jdg 21:25, Jdg 18:1, Jdg 19:1, Pro 16:2, Psa 12:4
- 7Mat 2:1, Rut 1:1–2, Mic 5:2, Mat 2:5–6, Jdg 19:1–2, Jos 19:15, Gen 35:19
- 8Jos 24:33, Jdg 17:11, Neh 13:10–11
- 101Pe 5:2, Jhn 12:6, Jdg 17:11, Ezk 13:19, 1Sa 2:36, 1Ti 6:10, Job 29:16, Isa 22:21
- 12Jdg 18:30, 1Ki 12:31, 1Ki 13:33–34, Num 16:5, Num 16:8–10
- 13Rom 10:2–3, Act 26:9, Jhn 16:2, Mat 15:13, Isa 44:20, Pro 14:12, Isa 66:3–4, Mat 15:9