1 Samweli 26
1 Hao Wazifu wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hakujificha katika kilima cha Hakila, kinachotazamana na Yeshimoni?”
2 Hivyo Sauli akashuka kwenda katika Jangwa la Zifu, akiwa na wapiganaji wake elfu tatu wa Israeli waliochaguliwa, ili kumtafuta Daudi huko.
3 Sauli akapiga kambi yake kando ya barabara juu ya kilima cha Hakila kinachotazamana na Yeshimoni, lakini Daudi alikuwa anaishi huko jangwani. Alipoona kuwa Sauli amemfuata huko,
4 Daudi akatuma wapelelezi na akapata habari kwa hakika kwamba Sauli alikuwa amewasili.
5 Ndipo Daudi akaondoka, akaenda hadi mahali ambapo Sauli alikuwa amepiga kambi. Akaona mahali Sauli na Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi, walipokuwa wamelala. Sauli alikuwa amelala ndani ya kambi, jeshi likiwa limemzunguka.
6 Basi Daudi akamuuliza Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, nduguye Yoabu, akisema, “Ni nani atakayeshuka pamoja nami kambini kwa Sauli?” Abishai akajibu, “Nitaenda pamoja nawe.”
7 Hivyo Daudi na Abishai wakaenda kwenye jeshi wakati wa usiku, tazama Sauli, alikuwa amelala ndani ya kambi na mkuki wake umekitwa ardhini karibu na kichwa chake. Abneri na askari walikuwa wamelala kumzunguka Sauli.
8 Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemtia adui yako mikononi mwako. Sasa niruhusu nimchome hadi ardhini kwa pigo moja la mkuki wangu; sitamchoma mara mbili.”
9 Lakini Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize! Ni nani awezaye kutia mkono juu ya mpakwa mafuta wa Mwenyezi Mungu na asiwe na hatia?”
10 Daudi akasema, “Hakika kama Mwenyezi Mungu aishivyo, Mwenyezi Mungu mwenyewe atampiga; au wakati wake utafika, naye atakufa, au ataenda vitani na kuangamia.
11 Lakini Mungu na apishie mbali nisije nikainua mkono juu ya mpakwa mafuta wa Mwenyezi Mungu. Sasa chukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyo karibu na kichwa chake, tuondoke.”
12 Hivyo Daudi akachukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyokuwa karibu na kichwa cha Sauli, nao wakaondoka. Hakuna yeyote aliyeona au kufahamu habari hii, wala hakuna hata mmoja aliyeamka usingizini. Wote walikuwa wamelala, kwa sababu Mwenyezi Mungu alikuwa amewatia kwenye usingizi mzito.
13 Kisha Daudi akavuka upande mwingine na kusimama juu ya kilima, mahali palipokuwa na nafasi pana kati yao.
14 Daudi akapaza sauti kwa jeshi na kwa Abneri mwana wa Neri, akisema, “Je, Abneri, hutanijibu?” Abneri akajibu, “Nani wewe unayemwita mfalme?”
15 Daudi akasema, “Wewe si ni mtu shujaa? Ni nani aliye kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukumlinda mfalme bwana wako? Mtu mmoja alikuja kumwangamiza mfalme, bwana wako.
16 Ulichokifanya si kizuri. Kwa hakika kama Mwenyezi Mungu aishivyo, wewe na watu wako mnastahili kufa, kwa sababu hamkumlinda bwana wenu, mpakwa mafuta wa Mwenyezi Mungu. Tazameni hapo mlipo. Uko wapi mkuki wa mfalme na gudulia la maji ambavyo vilikuwa karibu na kichwa chake?”
17 Sauli akatambua sauti ya Daudi, na kusema, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akajibu, “Naam, hiyo ndiyo, bwana wangu mfalme.”
18 Pia akaongeza, “Kwa nini bwana wangu anamfuatia mtumishi wake? Nimefanya nini, nalo kosa langu ni lipi nililolifanya niwe na hatia?
19 Sasa mfalme bwana wangu na asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama Mwenyezi Mungu amekuchochea dhidi yangu, basi yeye na aipokee sadaka yangu. Lakini kama ni wanadamu waliofanya hivyo, walaaniwe mbele za Mwenyezi Mungu! Wao sasa wamenifukuza kutoka sehemu yangu katika urithi wa Mwenyezi Mungu wangu wakisema, ‘Nenda ukatumikie miungu mingine.’
20 Basi usiache damu yangu imwagike kwenye ardhi mbali na uso wa Mwenyezi Mungu. Mfalme wa Israeli ametoka kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware katika milima.”
21 Ndipo Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Rudi, Daudi mwanangu. Kwa kuwa uliyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani leo, sitajaribu kukudhuru tena. Hakika nimetenda kama mpumbavu na nimekosa sana.”
22 Daudi akajibu, “Mkuki wa mfalme uko hapa. Mmoja wa vijana wako na avuke kuuchukua.
23 Mwenyezi Mungu humlipa kila mtu kwa ajili ya haki yake na uaminifu wake. Mwenyezi Mungu alikutia katika mikono yangu leo, lakini sikuinua mkono wangu juu ya mpakwa mafuta wa Mwenyezi Mungu.
24 Kwa hakika kama vile maisha yako yalivyokuwa ya thamani kwangu leo, vivyo hivyo maisha yangu na yawe na thamani kwa Mwenyezi Mungu na kuniokoa kutoka taabu zote.”
25 Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Mwanangu Daudi na ubarikiwe; utafanya mambo makubwa na hakika utashinda.” Basi Daudi akaenda zake, naye Sauli akarudi nyumbani.
Cross-references
127
- 11Sa 23:19, Psa 54:1–7, 1Sa 26:3, Jos 15:55, Jos 15:24
- 21Sa 24:2, 1Sa 13:2, 1Sa 24:17, Psa 140:4–9, 1Sa 23:23–25, Psa 38:12
- 31Sa 26:1, 1Sa 23:19
- 4Mat 10:16, Jos 2:1
- 51Sa 17:55, 1Sa 17:20, 1Sa 14:50–51, 2Sa 2:8–12, 2Sa 3:7–8, 1Ch 9:39, 2Sa 3:33–38, 1Sa 9:1
- 6Jdg 7:10–11, 2Sa 2:18, 2Sa 11:6, 2Sa 11:21, 2Sa 23:39, 2Sa 23:18, 1Sa 14:6–7, 2Sa 16:9–10
- 71Th 5:2–3
- 81Sa 24:4, 1Sa 26:23, 1Sa 24:18–19, Jos 21:44, 1Sa 23:14, Jdg 1:4, Deu 32:30, Nam 1:9
- 92Sa 1:14, Psa 105:15, 2Sa 1:16, 1Sa 24:6–7
- 10Deu 31:14, Gen 47:29, Rom 12:19, 1Sa 31:6, 1Sa 25:38, Psa 37:13, 1Sa 25:26, Deu 32:35
- 111Sa 24:6, 1Sa 24:12, 2Sa 1:16, 2Sa 1:14
- 12Gen 2:21, Gen 15:12, Isa 29:10, Est 6:1, 1Sa 26:7, 1Sa 24:4
- 13Jdg 9:7, 1Sa 24:8
- 161Sa 20:31, 2Sa 19:28, Psa 79:11, Eph 2:3, Psa 102:20, 2Sa 12:5, 1Sa 26:9, 1Sa 26:11
- 171Sa 24:16, 1Sa 24:8
- 181Sa 24:9, 1Sa 24:11–14, Jhn 18:23, Psa 69:4, Psa 7:3–5, Psa 35:7, Jhn 10:32, Jhn 8:46
- 192Sa 14:16, 2Sa 16:11, 2Sa 20:19, Gen 8:21, 1Ch 21:1, Gal 1:8–9, 1Sa 18:10, Jos 22:25–27
- 201Sa 24:14, Mat 26:55, 1Sa 2:9, Mat 26:47, 1Sa 25:29
- 211Sa 24:17, 1Sa 15:24, Exo 9:27, 1Sa 15:30, Mat 27:4, Psa 49:8, 1Sa 26:24, 1Sa 18:30
- 23Psa 62:12, 1Sa 24:6–7, Psa 18:20–26, Psa 7:8–9, Neh 13:14, 1Sa 26:11, 1Ki 8:32, 1Sa 26:9
- 24Psa 54:7, Mat 5:7, Psa 34:17–18, 2Co 1:9–10, Psa 18:25, Psa 18:1, Rev 7:14, Gen 48:16
- 25Num 24:9–10, Isa 54:17, 1Sa 24:19, Rom 8:37, Pro 26:25, Gen 32:28, 1Sa 24:22, Rom 8:35