Ayubu 3
1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 Kisha akasema:
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, na usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Giza na kivuli kikuu viikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 Usiku ule na ushikwe na giza nene; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Wale wanaozilaani siku na wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiione miali ya mapambazuko,
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 Wadogo kwa wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale wanaotafuta kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wanapofika kaburini?
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzingira?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 Lile nililokuwa nikiogopa limenijia; lile nililokuwa nikihofia limenipata.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
Перехресні посилання
146
- 1Jer 20:14–15, Psa 106:33, Psa 39:2–3, Job 35:16, Job 3:3, Job 2:5, Job 1:22, Job 2:9–10
- 3Jer 15:10, Jer 20:14–18, Job 10:18–19
- 4Jol 2:2, Exo 10:22–23, Rev 16:10, Amo 5:18, Mat 27:45, Act 27:20, Deu 11:12
- 5Job 10:21–22, Job 28:3, Psa 23:4, Jer 2:6, Psa 107:10, Jer 4:28, Psa 107:14, Jer 13:16
- 7Isa 13:20–22, Isa 24:8, Jer 7:34, Rev 18:22–23
- 8Job 41:1, Job 41:10, Mrk 5:38, Mat 11:17, 2Ch 35:25, Jer 9:17–18, Job 41:25, Amo 5:16
- 9Job 41:18, Job 30:26, Jer 8:15, Jer 13:16
- 10Ecc 6:3–5, Gen 20:18, Jer 20:17, Job 23:2, 1Sa 1:5, Ecc 11:10, Job 6:2–3, Job 10:1
- 11Job 10:18–19, Isa 46:3, Psa 58:8, Psa 22:9–10, Hos 9:14, Psa 139:13–16, Psa 71:6, Jer 15:10
- 12Isa 66:12, Gen 30:3, Gen 50:23, Ezk 16:4–5
- 13Job 21:13, Job 14:10–12, Ecc 9:10, Job 10:22, Job 7:21, Ecc 6:3–5, Job 7:8–10, Job 19:27
- 14Job 15:28, Isa 14:10–16, Psa 89:48, Psa 49:14, Job 12:17, Ezk 27:18–32, Ezk 26:20, Psa 49:6–10
- 15Job 22:25, 1Ki 10:27, Zep 1:18, Num 22:18, Zec 9:3, Isa 2:7, Job 12:21, Job 27:16–17
- 16Psa 58:8, Ecc 6:3, 1Co 15:8
- 17Rev 14:13, Job 17:16, Isa 57:1–2, Heb 4:11, Heb 4:9, Job 14:13, Mat 10:28, 2Th 1:6–7
- 18Job 39:7, Jdg 4:3, Exo 5:15–19, Isa 14:3–4, Exo 5:6–8
- 19Job 30:23, Ecc 12:7, Ecc 8:8, Psa 49:2, Heb 9:27, Psa 49:14–20, Ecc 12:5, Luk 16:22–23
- 20Jer 20:18, Job 7:15–16, Pro 31:6, 1Sa 1:10, Job 33:30, 2Ki 4:27, Job 3:16, Job 6:9
- 21Rev 9:6, Pro 2:4, Jon 4:3, Num 11:15, Jon 4:8, 1Ki 19:4
- 23Job 19:8, Lam 3:7, Isa 40:27, Hos 2:6, Job 19:12, Job 12:14, Psa 31:8, Lam 3:9
- 24Psa 102:9, Psa 42:3–4, Psa 80:5, Psa 38:8, Psa 32:3, Job 33:20, Job 7:19, Isa 59:11
- 25Job 1:5, Job 30:15, Job 31:23
- 26Job 7:14, Psa 143:11, Job 27:9