Ayubu 4
1 Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
2 “Kama mtu akithubutu kuzungumza nawe, kutakukasirisha? Lakini ni nani awezaye kujizuia asiseme?
3 Fikiri jinsi umewafundisha watu wengi, jinsi umeitia nguvu mikono iliyokuwa dhaifu.
4 Maneno yako yamewategemeza wale waliojikwaa; umeyatia nguvu magoti yaliyokuwa dhaifu.
5 Lakini sasa hii taabu imekujia wewe, nawe unashuka moyo; imekupiga wewe, nawe unafadhaika.
6 Je, kumcha Mungu kwako hakupaswi kuwa ndiyo matumaini yako na njia zako kutokuwa na lawama ndilo taraja lako?
7 “Fikiri sasa: Ni mtu yupi asiye na hatia ambaye aliwahi kuangamia? Ni wapi wanyofu waliwahi kuangamizwa?
8 Kwa jinsi mimi nimechunguza, wale walimao ubaya na wale hupanda uovu, huvuna hayo hayo.
9 Kwa pumzi ya Mungu huangamizwa; kwa mshindo wa hasira zake huangamia.
10 Simba anaweza kunguruma na kukoroma, lakini bado meno ya simba mkubwa huvunjika.
11 Simba anaweza kuangamia kwa kukosa mawindo, nao wana wa simba jike hutawanyika.
12 “Neno lililetwa kwangu kwa siri, masikio yangu yakasikia mnong’ono wake.
13 Katikati ya ndoto za kutia wasiwasi wakati wa usiku, hapo usingizi mzito uwapatapo wanadamu,
14 hofu na kutetemeka kulinishika na kufanya mifupa yangu yote itetemeke.
15 Kuna roho aliyepita mbele ya uso wangu, nazo nywele za mwili wangu zikasimama.
16 Yule roho akasimama, lakini sikuweza kutambua kilikuwa kitu gani. Umbo fulani lilisimama mbele ya macho yangu, kukawa na ukimya kisha nikasikia sauti:
17 ‘Je, binadamu aweza kuwa mwadilifu kuliko Mungu? Je, mtu aweza kuwa safi kuliko Muumba wake?
18 Ikiwa Mungu hawaamini watumishi wake, ikiwa yeye huwalaumu malaika wake kwa kukosea,
19 ni mara ngapi zaidi wale wanaoishi katika nyumba za udongo wa mfinyanzi, ambazo misingi yake ipo mavumbini, ambao wamepondwa kama nondo!
20 Kati ya mawio na machweo huvunjwa vipande vipande; bila yeyote kutambua, huangamia milele.
21 Je, kamba za hema lao hazikung’olewa, hivyo hufa bila hekima?’
Перехресні посилання
149
- 1Job 2:11, Job 6:1, Job 42:9, Job 15:1, Job 3:1–2, Job 22:1, Job 8:1
- 2Job 32:18–20, Act 4:20, Jer 6:11, 2Co 7:8–10, 2Co 2:4–6, Jer 20:9
- 3Isa 35:3, Luk 22:32, Heb 12:12, Job 16:5, Pro 10:21, Luk 22:43, Eph 4:29, Deu 3:28
- 4Psa 145:14, 1Th 5:14, Heb 12:12, Pro 12:18, Pro 16:23–24, 2Co 7:6, Isa 35:3–4, Dan 5:6
- 5Job 19:21, 2Co 4:16, Heb 12:3, Pro 24:10, 2Co 4:1, Job 3:25–26, Heb 12:5, Job 6:14
- 6Pro 3:26, Pro 14:26, Job 1:1, Job 17:15, Job 23:11–12, Job 13:15, Job 16:17, 2Ki 20:3
- 7Psa 37:25, Job 36:7, 2Pe 2:9, Act 28:4, Job 8:20, Ecc 9:1–2, Job 9:22–23, Ecc 7:15
- 8Gal 6:7–8, Pro 22:8, Hos 8:7, Job 15:35, 2Co 9:6, Jer 4:18, Hos 10:12–13, Psa 7:14–16
- 9Job 15:30, Isa 11:4, 2Th 2:8, Isa 30:33, Rev 2:16, Psa 18:15, Exo 15:8, Exo 15:10
- 10Psa 58:6, Psa 3:7, Psa 57:4, Pro 30:14, Job 29:17, Job 5:15
- 11Psa 34:10, Psa 7:2, Job 8:3–4, Job 27:14–15, Num 23:24, 2Ti 4:17, Job 1:19, Num 24:9
- 12Job 26:14, 1Co 13:12, Psa 62:11
- 13Job 33:14–16, Gen 2:21, Gen 46:2, Dan 4:5, Dan 2:28–29, Gen 31:24, Dan 2:19, Num 12:6
- 14Job 33:19, Rev 1:17, Psa 119:120, Luk 1:12, Luk 1:29, Job 7:14, Hab 3:16, Isa 6:5
- 15Heb 1:7, Luk 24:37–39, Dan 5:6, Psa 104:4, Isa 21:3–4, Isa 13:8, Mat 14:26, Heb 1:14
- 161Ki 19:12
- 17Job 9:2, Job 25:4, Ecc 7:20, Psa 143:2, Rom 11:33, Jer 17:9, Job 40:8, Job 15:14
- 182Pe 2:4, Job 25:5–6, Jud 1:6, Job 15:15–16, Psa 104:4, Psa 103:20–21
- 19Job 10:9, Gen 2:7, Gen 3:19, Job 33:6, 2Co 4:7, 2Co 5:1, Job 13:28, Job 13:12
- 20Job 20:7, Isa 38:12–13, Psa 39:13, 2Ch 15:6, Psa 92:7, Pro 10:7, Job 14:20, Job 16:22
- 21Job 36:12, Luk 16:22–23, Psa 39:11, Job 8:22, Jas 1:11, Isa 14:16, Psa 146:3–4, Psa 39:5
Теми в цьому розділі
26
Afflictions and Adversities, Angel (A Spirit), Blasting, Body, Breath, Clay, Death, Depravity of Man, Doubting, Dream, Eliphaz, Faith, God, Ground, Heathen, Immortality, Job, Life, Lion, Man, Moth, Presumption, Sin, Vision, Wicked (People), Wisdom