Ayubu 28
1 Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu inaposafishwa.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huning’inia na kubembea.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba ya gumegume, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
12 Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
14 Kilindi husema, “Haiko ndani yangu”; bahari nayo husema, “Haiko pamoja nami.”
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa kwa vito vya dhahabu.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
20 Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
22 Uharibifu na Mauti husema, “Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.”
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
25 Alipoufanyia upepo nguvu zake na kuyapima maji,
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia ya mwali wa radi,
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, “Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.”
Referências cruzadas
141
- 11Pe 1:7, Pro 17:3, Mal 3:2–3, Isa 48:10, 1Ch 29:2–5, Zec 13:9, 1Ki 10:21, Pro 27:21
- 2Deu 8:9, Num 31:22, Gen 4:22, 1Ch 22:14
- 3Ecc 1:13, Pro 2:4, Hab 2:13, Mat 6:33, Job 10:21–22, Luk 16:8, Job 12:22, Job 38:16–17
- 5Isa 28:25–29, Psa 104:14–15, Gen 1:11–12, Gen 1:29, Ezk 28:13–14
- 6Exo 24:10, Job 28:16, Sng 5:14, Isa 54:11, Rev 21:19
- 7Job 11:6, Job 28:21–23, Job 38:24, Rom 11:33, Job 38:19
- 9Nam 1:4–6
- 10Hab 3:9, Pro 24:4, Pro 14:23
- 11Isa 45:2–3, 1Co 4:5, Job 26:8, Isa 44:27, Isa 37:25
- 12Job 28:20, Pro 2:4–6, Jas 1:5, Pro 3:19, 1Co 1:19–20, Col 2:3, Job 28:28, Jas 1:17
- 13Pro 8:18–19, Pro 8:11, Pro 3:14–15, Job 28:21–22, Psa 119:72, Pro 23:23, Pro 16:16, Mat 13:44–46
- 14Rom 11:33–34
- 15Pro 16:16, Pro 3:13–15, Pro 8:19, Pro 8:10–11, Job 28:18, Pro 8:17
- 16Ezk 28:13, Isa 13:12, Psa 45:9, 1Ch 29:4, Exo 28:20
- 17Rev 22:1, Ezk 1:22, Pro 16:16, Rev 4:6, Rev 21:11
- 18Pro 3:15, Pro 31:10, Ezk 27:16, Lam 4:7, Rev 21:21, Rev 18:12, 1Ti 2:9, Mat 13:45–46
- 19Ezk 28:13, Exo 39:10, Pro 8:19, Exo 28:17, Rev 21:20
- 20Job 28:12, Jas 1:5, Job 28:28, Jas 1:17, Job 28:23, 1Co 2:6–15, Pro 2:6, Ecc 7:23–24
- 21Psa 49:3–4, 1Co 2:7–10, Mat 11:25, Col 2:3, Mat 13:35, Mat 13:17
- 22Psa 83:10–12, Job 26:6, Job 28:14
- 23Pro 8:22–31, 1Co 1:30, Rom 11:33, Jud 1:25, Pro 2:6, Psa 147:5, Luk 10:21–22, Mat 11:27
- 24Pro 15:3, Zec 4:10, Rev 5:6, Psa 33:13–14, 2Ch 16:9
- 25Psa 135:7, Isa 40:12, Job 12:15
- 26Job 38:25, Job 37:3, Zec 10:1, Jer 14:22, Job 36:26, Job 38:27, Psa 148:8, Job 36:32
- 27Psa 19:1, Pro 8:22–29
- 28Psa 111:10, Pro 1:7, Pro 9:10, Pro 3:7, Ecc 12:13, Deu 4:6, Jas 3:13–17, Psa 34:14
Temas neste capítulo
32
Art, Brass, Civil Engineering, Continents, Coral, Crystal, Fear, Geology, Glass, God, Gold, Holiness, Ignorance, Iron, Job, Lightning, Lion, Meteorology and Celestial Phenomena, Molding, Money, Mountain, Onyx, Ophir, Pearl, Philosophy, Readings, Select, Ruby, Sapphire, Science, Topaz, Vulture, Wisdom