Ezekieli 26
1 Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
3 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
4 Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
5 Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mungu Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
6 nayo makazi yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
7 “Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
8 Atayaharibu makazi yako huko bara kwa upanga; atajenga husuru dhidi yako, na kupandisha kilima hadi kuta zako, na kuinua ngao zake dhidi yako.
9 Ataelekeza mapigo ya magogo ya kubomoa boma dhidi ya kuta zako, na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
10 Farasi wake watakuwa wengi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari ya kukokotwa, na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu wanaoingia mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
11 “Kwato za farasi wake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
12 Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
13 Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
14 Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Mwenyezi Mungu nimenena, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
15 “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
16 Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka viti vyao vya utawala, na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wataketi chini ardhini, wakiwa wamevikwa hofu kuu, wakitetemeka kila dakika na kukustaajabia.
17 Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “ ‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na wakaaji wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
18 Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
19 “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
20 ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale wanaoshuka shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale wanaoshuka shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
21 Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mungu Mwenyezi.”
Referências cruzadas
142
- 1Ezk 20:1, Jer 39:2, Ezk 1:2, Ezk 8:1
- 2Isa 23:1–18, Jol 3:4, Jer 25:22, Ezk 36:2, Psa 83:2–4, Jer 27:3, Ezk 25:6, 2Sa 5:11
- 3Jer 51:42, Isa 5:30, Mic 4:11, Ezk 27:32–34, Ezk 38:3, Psa 93:3–4, Jer 21:13, Ezk 5:8
- 4Isa 23:11, Amo 1:10, Ezk 26:9, Zec 9:3, Ezk 26:12, Lev 14:41–45, Ezk 24:7–8, Jer 5:10
- 5Ezk 29:19, Ezk 26:19, Ezk 47:10, Ezk 27:32, Ezk 25:7, Ezk 26:14
- 6Ezk 26:8, Ezk 16:46, Ezk 25:11, Ezk 16:48, Ezk 25:5, Ezk 25:7, Jer 49:2, Ezk 25:14
- 7Dan 2:37, Ezr 7:12, Ezk 23:24, Nam 2:3–4, Hos 8:10, Isa 10:8, Jer 25:9, Jer 52:32
- 8Ezk 21:22, Jer 52:4, Jer 32:24, Jer 6:6, 2Sa 20:15
- 92Ch 26:15
- 10Ezk 26:15, Ezk 27:28, Jer 47:3, Jer 4:13, Ezk 26:7, Jos 6:5, Nam 2:3–4, Jos 6:20
- 11Isa 5:28, Isa 26:5, Hab 1:8, Jer 43:13, Jer 51:27
- 12Isa 23:8, 2Ch 32:27, Amo 5:11, Zec 9:3–4, Dan 11:8, Jer 25:34, Rev 18:11–13, 2Ch 36:10
- 13Jer 7:34, Isa 23:16, Jer 25:10, Jer 16:9, Isa 24:8–9, Isa 14:11, Amo 6:4–7, Ezk 28:13
- 14Job 12:14, Mal 1:4, Deu 13:16, Ezk 26:4–5, Isa 14:27, Num 23:19, Mat 24:35, Ezk 30:12
- 15Ezk 27:35, Jer 49:21, Ezk 31:16, Ezk 26:18, Isa 2:19, Ezk 32:10, Heb 12:26–27, Ezk 27:28
- 16Ezk 32:10, Hos 11:10, Jon 3:6, Job 8:22, Psa 35:26, Isa 3:26, 1Pe 5:5, Rev 18:11–19
- 17Isa 14:12, Ezk 19:1, 2Sa 1:25–27, Rev 18:9–10, Ezk 32:16, Ezk 27:2–36, Ezk 19:14, Ezk 32:2
- 18Isa 23:5–7, Ezk 26:15, Ezk 27:28–30, Ezk 27:35, Isa 23:10–12, Isa 41:5
- 19Ezk 26:3, Isa 8:7–8, Dan 9:26, Dan 11:40, Rev 17:15
- 20Luk 10:15, Psa 27:13, Zec 2:8, Ezk 28:25–26, Ezk 32:18–32, Isa 4:5, Lam 3:6, Jon 2:6
- 21Ezk 27:36, Ezk 28:19, Rev 18:21, Psa 37:36, Ezk 26:14–16, Jer 51:64