Ezekieli 25
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Waamoni utabiri dhidi yao.
3 Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana Mungu Mwenyezi. Hili ndilo Bwana Mungu Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ulisema, “Aha!” juu ya mahali pangu patakatifu palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli ilipoangamizwa, na juu ya watu wa Yuda walipoenda uhamishoni,
4 kwa hiyo nitawatia mikononi mwa watu wa mashariki mkawe mali yao. Watapiga kambi zao kati yenu na kufanya makazi miongoni mwenu, watakula matunda yenu na kunywa maziwa yenu.
5 Nitaufanya mji wa Raba kuwa malisho ya ngamia na Amoni kuwa mahali pa kondoo pa kupumzikia. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
6 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Kwa kuwa mmepiga makofi yenu na kufanya kishindo kwa miguu, mkifurahia kwa mioyo yenu miovu juu ya yale mabaya yaliyoipata nchi ya Israeli,
7 hivyo nitaunyoosha mkono wangu dhidi yenu na kuwatoa kuwa nyara kwa mataifa. Nitawakatilia mbali kutoka mataifa na kuwang’oa kutoka nchi. Nitawaangamiza, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’ ”
8 “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: ‘Kwa sababu Moabu na Seiri wamesema, “Tazama, nyumba ya Yuda imekuwa kama mataifa mengine yote,”
9 kwa hiyo nitaiondoa ile miji iliyo kando ya Moabu, kuanzia miji iliyo mipakani: Beth-Yeshimothi, Baal-Meoni na Kiriathaimu, iliyo utukufu wa nchi hiyo.
10 Nitaitia Moabu pamoja na Waamoni mikononi mwa watu wa Mashariki kuwa milki yao, ili Waamoni wasikumbukwe miongoni mwa mataifa,
11 nami nitatoa adhabu kwa Moabu. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’ ”
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: ‘Kwa sababu Edomu walilipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda, wakakosea sana kwa kufanya hivyo,
13 kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya Edomu na kuua watu wake na wanyama wao. Nitaufanya ukiwa, na kuanzia Temani hadi Dedani wataanguka kwa upanga.
14 Nitalipiza Edomu kisasi kwa mkono wa watu wangu Israeli, nao watawatendea Edomu sawasawa na hasira yangu na ghadhabu yangu, nao watakijua kisasi changu, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
15 “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: ‘Kwa sababu Wafilisti wamewalipiza kisasi kwa uovu wa mioyo yao na kwa uadui wa siku nyingi wakataka kuangamiza Yuda,
16 kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Mimi ninakaribia kuunyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, nami nitawakatilia mbali Wakerethi na kuwaangamiza wale waliosalia katika pwani.
17 Nitalipiza kisasi kikubwa juu yao na kuwaadhibu katika ghadhabu yangu. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapolipiza kisasi juu yao.’ ”
Referências cruzadas
120
- 2Jer 49:1–6, Amo 1:13–15, Ezk 6:2, Zep 2:8–11, Jer 9:25–26, Ezk 21:2, Jer 27:3, Ezk 21:28–32
- 3Ezk 36:2, Pro 17:5, Psa 70:2–3, Ezk 25:6, Pro 24:17–18, Mic 7:8, Lam 4:21, Ezk 35:10–15
- 4Deu 28:33, Jdg 6:33, 1Ki 4:30, Isa 1:7, Deu 28:51, Isa 32:8–9, Lev 26:16, Isa 65:22
- 5Ezk 21:20, 2Sa 12:26, Isa 17:2, Psa 83:18, Deu 3:11, Ezk 35:9, Ezk 30:8, Isa 32:14
- 6Oba 1:12, Zep 2:8, Zep 2:10, Ezk 6:11, Nam 3:19, Job 27:23, Ezk 25:15, Ezk 36:5
- 7Zep 1:4, Ezk 6:14, Ezk 25:16, Ezk 25:13, Ezk 14:9, Jer 49:2, Ezk 35:3, Amo 1:14–15
- 8Jer 25:21, Jer 48:1–47, Isa 15:1–9, Ezk 25:12–14, Isa 36:18–20, Ezk 35:1–15, Isa 10:9–11, Isa 34:1–17
- 9Jer 48:23, Jos 13:17, Jos 13:19–20, Num 32:37–38, Num 32:3, 1Ch 5:8, Num 33:49, Jos 12:3
- 10Ezk 21:32, Isa 23:16, Psa 83:3–6, Ezk 25:4
- 11Psa 149:7, Jer 25:21, Ezk 25:17, Jud 1:15, Ezk 5:8, Ezk 35:15, Psa 9:16, Ezk 5:10
- 12Jer 49:7–22, Ezk 25:8, Psa 137:7, Amo 1:11–12, Oba 1:10–16, Ezk 35:1–15, 2Ch 28:17–18, Gen 27:41–42
- 13Ezk 29:8, Mal 1:3–4, Jer 25:23, Jer 49:7–8, Ezk 14:8, Ezk 25:16, Lam 4:21–22, Gen 36:11
- 14Isa 11:14, Gen 27:29, Psa 58:10–11, Nam 1:2–4, Rev 6:16–17, Ezk 35:11, Heb 10:30–31, Isa 63:1–6
- 15Ezk 25:6, Isa 14:29–31, Jer 25:20, Ezk 25:12, 2Ch 28:18, Zec 9:5–8, 1Sa 4:1–6, Jdg 14:1–16
- 161Sa 30:14, Zep 2:4–15, Jer 47:1–7, Ezk 25:13, Ezk 25:7, 2Sa 15:18
- 17Ezk 25:11, Ezk 25:14, Ezk 5:15, Psa 9:16, Ezk 6:7, Ezk 25:5