Ezekieli 31
1 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa tatu, siku ya kwanza, neno la Mwenyezi Mungu likanijia, kusema:
2 “Mwanadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri na makundi yake hivi: “ ‘Je, ni nani awezaye kulinganishwa na wewe katika fahari.
3 Angalia Ashuru, zamani ulikuwa mwerezi huko Lebanoni, ukiwa na matawi mazuri na kutia msitu kivuli; ulikuwa mrefu sana, kilele chake kilipita majani ya miti yote.
4 Maji mengi yaliustawisha, chemchemi zenye maji mengi ziliufanya urefuke; vijito vyake vilitiririka pale ulipoota pande zote na kupeleka mifereji yake kwenye miti yote ya shambani.
5 Hivyo ukarefuka kupita miti yote ya shambani; vitawi vyake viliongezeka na matawi yake yakawa marefu, yakitanda kwa sababu ya wingi wa maji.
6 Ndege wote wa angani wakaweka viota kwenye vitawi vyake, wanyama wote wa shambani wakazaana chini ya matawi yake, mataifa makubwa yote yaliishi chini ya kivuli chake.
7 Ulikuwa na fahari katika uzuri, ukiwa na matawi yaliyotanda, kwa kuwa mizizi yake iliteremka hadi kwenye maji mengi.
8 Mierezi katika bustani ya Mungu haikuweza kushindana nao, wala misunobari haikuweza kulingana na vitawi vyake, wala miaramoni haikulinganishwa na matawi yake, wala hakukuwa na mti katika bustani ya Mungu wa kulinganisha na uzuri wake.
9 Niliufanya kuwa mzuri, ukiwa na matawi mengi; nao ulionewa wivu na miti yote ya Edeni katika bustani ya Mungu.
10 “ ‘Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Kwa sababu ulikuwa mrefu sana, kilele chake kikiwa juu ya majani manene ya miti na kwa sababu ulikuwa na kiburi cha urefu wake,
11 niliutia mikononi mwa mtawala wa mataifa, ili yeye autende sawasawa na uovu wake. Nikaukatilia mbali,
12 nayo mataifa mageni yaliyo makatili sana yaliukata huo mti na kuuacha. Matawi yake yalianguka juu ya milima na kwenye mabonde yote, vitawi vyake vikavunjika na kusambaa katika makorongo yote ya nchi. Mataifa yote ya duniani yakaondoka kutoka kivuli chake na kuuacha.
13 Ndege wote wa angani wakakaa kwenye ule mti ulioanguka na wanyama pori wote wakakaa katikati ya vitawi vyake.
14 Kamwe hakutakuwa na miti mingine kando ya hayo maji itakayorefuka zaidi ya huo, vilele vyake vikiwa juu ya majani yote ya miti. Hakuna miti mingine, hata kama imekunywa maji vizuri namna gani, itakayofikia urefu huo. Yote mwisho wake ni kifo, na kuingia ardhini, kama vile ilivyo kwa wanadamu, pamoja na wale wanaoshuka shimoni.
15 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Katika siku ile mwerezi uliposhushwa chini kaburini nilizifunika chemchemi zenye maji mengi kwa maombolezo: Nilivizuia vijito vyake na wingi wa maji yake nikauzuia. Kwa sababu yake niliivika Lebanoni huzuni, nayo miti yote ya shambani ikanyauka.
16 Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa kishindo cha kuanguka kwake wakati nilipoushusha chini kaburini pamoja na wale wanaoshuka shimoni. Ndipo miti yote ya Edeni, miti iliyo bora kuliko yote na iliyo mizuri sana ya Lebanoni, miti yote ile iliyokunywa maji vizuri, ilifarijika hapa duniani.
17 Wale walioishi katika kivuli chake, wale walioungana naye miongoni mwa mataifa, nao pia walikuwa wamezikwa pamoja naye, wakiungana na wale waliouawa kwa upanga.
18 “ ‘Ni miti ipi ya Edeni inayoweza kulinganishwa nawe kwa fahari na utukufu? Hata hivyo, wewe pia, utashushwa pamoja na miti ya Edeni hadi chini kabisa; utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga. “ ‘Huyu ni Farao pamoja na makundi yake yote, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
Referências cruzadas
117
- 1Ezk 30:20, Jer 52:5–6, Ezk 1:2
- 2Ezk 29:19, Ezk 30:10, Ezk 31:18, Jer 1:17, Rev 10:11, Nam 3:8–10, Jer 1:5, Isa 14:13–14
- 3Isa 10:33–34, Dan 4:20–23, Dan 4:10, Jdg 9:15, Ezk 17:22, Ezk 17:3–4, Dan 4:12, Nam 3:1–19
- 4Rev 17:1, Ezk 17:8, Pro 14:28, Rev 17:15, Ezk 17:5, Jer 51:36
- 5Dan 4:11, Ezk 17:5, Isa 36:4, Psa 1:3, Isa 10:8–14, Isa 37:11–13, Isa 36:18–19, Psa 37:35–36
- 6Mat 13:32, Ezk 17:23, Dan 4:21, Dan 4:12
- 8Ezk 28:13, Isa 51:3, Gen 13:10, Psa 80:10, Ezk 31:18, Ezk 31:16, Gen 2:8–9, Psa 37:35
- 9Ezk 28:13, Gen 13:10, Dan 2:37–38, Psa 75:6–7, Isa 51:3, Psa 96:12–13, Gen 26:14, Ecc 4:4
- 10Ezk 28:17, Dan 5:20, 2Ch 32:25, Dan 4:30, Ezk 31:14, Pro 16:18, Jas 4:6, 2Ch 25:19
- 11Deu 18:12, Dan 5:18–19, Ezk 32:11–12, Nam 3:18, Jdg 1:7, Jas 2:13, Lam 1:21, Jdg 16:23
- 12Ezk 28:7, Ezk 35:8, Hab 1:6, Ezk 30:11, Nam 3:17–18, Rev 17:16, Hab 1:11, Isa 34:5–7
- 13Ezk 32:4, Isa 18:6, Ezk 29:5, Rev 19:17–18
- 14Psa 82:7, Ezk 26:20, 2Pe 2:6, 1Co 10:11, Neh 13:18, Psa 63:9–10, Dan 5:22–23, Ezk 32:18–32
- 15Nam 2:8–10, Mal 3:4, Rev 18:18–19, Rev 18:9–11
- 16Isa 14:15, Ezk 26:15, Isa 14:8, Ezk 31:9, Ezk 27:28, Hag 2:7, Hab 2:17, Rev 11:13
- 17Psa 9:17, Ezk 31:6, Ezk 31:3, Lam 4:20, Ezk 32:20–31, Isa 14:9, Neh 3:17–18, Ezk 30:6–8
- 18Ezk 32:19, Ezk 32:21, Ezk 28:10, Ezk 31:16, Ezk 31:2, Jer 9:25–26, Psa 52:7, Mat 13:19