Ezekieli 23
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, palikuwa na wanawake wawili, binti za mama mmoja.
3 Wakawa makahaba huko Misri, wakajitia kwenye ukahaba tangu ujana wao. Katika nchi ile vifua vyao vya ubikira vikakumbatiwa, na wakapoteza ubikira wao.
4 Mkubwa aliitwa Ohola, na mdogo wake Oholiba. Walikuwa wangu nao wakazaa watoto wa kiume na wa kike. Ohola ni Samaria, Oholiba ni Yerusalemu.
5 “Ohola akajitia kwenye ukahaba alipokuwa bado ni wangu, akatamani sana wapenzi wake, mashujaa Waashuru,
6 waliovaa nguo za buluu, watawala na majemadari, wote walikuwa wanaume vijana wa kuvutia, wapandao farasi.
7 Akafanya ukahaba na wakuu wote wa Ashuru, na kujinajisi kwa sanamu zote za kila mwanaume aliyemtamani.
8 Hakuacha ukahaba wake aliouanza huko Misri, wakati wa ujana wake ambapo wanaume walilala naye, wakikumbatia kifua cha ubikira wake na kumwaga tamaa zao juu yake.
9 “Kwa hiyo nilimtia mikononi mwa wapenzi wake, Waashuru, kwa kuwa ndio aliowatamani.
10 Wakamvua nguo zake wakamwacha uchi, wakawachukua wanawe wa kiume na wa kike, naye wakamuua kwa upanga. Akawa kitu cha kudharauliwa miongoni mwa wanawake, na adhabu ikatolewa dhidi yake.
11 “Oholiba dada yake aliliona jambo hili, lakini kwa tamaa zake na ukahaba wake, akaharibu tabia zake kuliko Ohola, dada yake.
12 Yeye naye aliwatamani Waashuru, watawala na majemadari, mashujaa waliovalia sare, wapandao farasi, wanaume vijana wote waliovutia.
13 Nikaona kuwa yeye pia alijinajisi, wote wawili wakaelekea njia moja.
14 “Lakini yeye akazidisha ukahaba wake. Akaona wanaume waliochorwa ukutani, picha za Wakaldayo waliovalia nguo nyekundu,
15 wakiwa na mikanda viunoni mwao na vilemba vichwani mwao, wote walifanana na maafisa wa Babeli wapandao magari ya vita, wenyeji wa Ukaldayo.
16 Mara tu alipowaona, aliwatamani, akatuma wajumbe kwao huko Ukaldayo.
17 Ndipo hao Wababeli wakaja kwake kwenye kitanda cha mapenzi, nao katika tamaa zao wakamtia unajisi. Baada ya kutiwa unajisi, akawaacha kwa kuwachukia.
18 Alipofanya ukahaba wake waziwazi na kuonesha uchi wake, nilimwacha kwa kumchukia, kama vile nilivyokuwa nimemwacha dada yake.
19 Lakini akazidisha ukahaba wake alipozikumbuka siku za ujana wake, alipokuwa kahaba huko Misri.
20 Huko aliwatamani wapenzi wake, ambao viungo vyao vya uzazi ni kama vya punda, na kile kiwatokacho ni kama kiwatokacho farasi.
21 Hivyo ulitamani uasherati wa ujana wako wakati ulipokuwa Misri, kifua chako kilipokumbatiwa, na matiti yako machanga yakapapaswa.
22 “Kwa hiyo, Oholiba, hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitawachochea wapenzi wako wawe kinyume na wewe, wale uliowaacha kwa kuchukia, nitawaleta dhidi yako kutoka kila upande:
23 Wababeli na Wakaldayo wote, watu kutoka Pekodi, na Shoa na Koa, wakiwa pamoja na Waashuru wote, vijana wazuri, wote wakiwa watawala na majemadari, maafisa wa magari ya vita na watu wa vyeo vya juu, wote wakiwa wamepanda farasi.
24 Watakuja dhidi yako wakiwa na silaha, magari ya vita, magari ya kukokota, pamoja na umati mkubwa wa watu. Watakuzingira pande zote kwa ngao na vigao na kwa chapeo. Nitakutia mikononi mwao ili wakuadhibu, nao watakuadhibu sawasawa na sheria zao.
25 Nitaelekeza hasira yangu yenye wivu dhidi yako, nao watakuadhibu kwa hasira kali. Watakatilia mbali pua yako na masikio yako, na wale watakaosalia miongoni mwako watauawa kwa upanga. Watachukua wana wako wa kiume na wa kike, na wale watakaosalia miongoni mwenu watateketezwa kwa moto.
26 Watakuvua nguo zako pia, na kuchukua mapambo yako yaliyotengenezwa kwa vito na dhahabu.
27 Hivyo ndivyo nitakavyokomesha uasherati wako na ukahaba wako uliouanza huko Misri. Hutatazama vitu hivi kwa kuvitamani wala kukumbuka Misri tena.
28 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Ninakaribia kukutia mikononi mwa wale unaowachukia, kwa wale uliojitenga nao kwa kuwachukia.
29 Watakutenda mambo ya chuki na kukunyang’anya kila kitu ulichokifanyia kazi. Watakuacha uchi na mtupu na aibu ya ukahaba wako itafunuliwa. Uasherati wako na uzinzi wako
30 umekuletea haya yote, kwa sababu ulitamani mataifa na kujinajisi kwa sanamu zao.
31 Umeiendea njia ya dada yako, hivyo nitakitia kikombe chake mkononi mwako.
32 “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “Utakinywea kikombe cha dada yako, kikombe kikubwa na chenye kina kirefu; kitakuletea dharau na dhihaka, kwa kuwa kimejaa sana.
33 Utalewa ulevi na kujawa huzuni, kikombe cha maangamizi na ukiwa, kikombe cha dada yako Samaria.
34 Utakinywa chote na kukimaliza; utakivunja vipande vipande na kuyararua matiti yako. Nimenena haya, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
35 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Kwa kuwa ulinisahau mimi na kunitupa nyuma yako, lazima ubebe matokeo ya uasherati wako na ukahaba wako.”
36 Mwenyezi Mungu akaniambia, “Mwanadamu, je, utawahukumu Ohola na Oholiba? Basi wakabili kwa ajili ya matendo yao ya machukizo,
37 kwa kuwa wamefanya uzinzi na damu imo mikononi mwao. Wamefanya uzinzi na sanamu zao, hata watoto walionizalia wamewatoa kafara, kuwa chakula kwa sanamu hizo.
38 Pia wamenifanyia hili: wakati huo huo wamenajisi patakatifu pangu na kuzitangua Sabato zangu.
39 Siku ile ile walitoa kafara watoto wao kwa sanamu zao, waliingia patakatifu pangu na kupanajisi. Hilo ndilo walilolifanya katika nyumba yangu.
40 “Hata waliwatuma wajumbe kuwaita watu kutoka mbali, nao walipowasili ulioga kwa ajili yao, ukapaka macho yako wanja, na ukavaa mapambo yako yaliyotengenezwa kwa vito vya dhahabu.
41 Ukaketi kwenye kiti cha anasa, kukiwa na meza iliyoandaliwa mbele yake ambayo juu yake ulikuwa umeweka uvumba na mafuta ambayo yalikuwa yangu.
42 “Kelele za umati wa watu wasiojali zilikuwa zimemzunguka, wakaleta watu wengi waliokuwa wakifanya makelele na walevi kutoka nyikani, ambao walitia bangili kwenye mikono ya yule mwanamke na dada yake na pia taji nzuri za kupendeza kwenye vichwa vyao.
43 Ndipo nikasema kuhusu yule aliyechakazwa na uzinzi, ‘Basi wamtumie kama kahaba, kwa kuwa ndivyo alivyo.’
44 Nao wakazini naye. Kama vile watu wazinivyo na kahaba, ndiyo hivyo walivyozini na hao wanawake waasherati, Ohola na Oholiba.
45 Lakini watu wenye haki, watawahukumia adhabu wanawake wafanyao uzinzi na kumwaga damu, kwa kuwa ni wazinzi na damu iko mikononi mwao.
46 “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Leteni watu wengi wenye makelele dhidi yao na uwaache wapate hofu na watekwe nyara.
47 Hao watu wengi watawapiga kwa mawe na kuwaua kwa panga zao, watawaua wana wao wa kiume na wa kike, na kuzichoma nyumba zao.
48 “Hivyo nitaukomesha uasherati katika nchi, ili wanawake wote wapate onyo nao wasije wakafanya uasherati kama ninyi mlivyofanya.
49 Utapata adhabu kwa ajili ya uasherati wako na kuchukua matokeo ya dhambi zako za uasherati. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mungu Mwenyezi.”
Referências cruzadas
311
- 2Jer 3:7–10, Ezk 16:44–46
- 3Lev 17:7, Jos 24:14, Ezk 16:22, Deu 29:16, Ezk 23:19, Hos 2:15, Ezk 23:21, Ezk 20:8
- 4Ezk 16:8, Jhn 4:22, Ezk 16:20, Ezk 16:40, Psa 45:11–16, Exo 19:5–6, 1Ki 12:20, Jer 2:2–3
- 5Hos 5:13, 2Ki 15:19, 2Ki 17:3, 2Ki 16:7, Hos 8:9–10, Jer 50:38, Ezk 16:28, 2Ki 17:7–18
- 6Ezk 23:23
- 7Hos 5:3, Hos 6:10, Ezk 22:3–4, Ezk 20:7, Psa 106:39, Ezk 16:15, Ezk 23:30, Gen 10:22
- 8Ezk 23:3, Exo 32:4, Ezk 23:19, 1Ki 12:28, 2Ki 17:16, 2Ki 10:29, Ezk 23:21
- 92Ki 17:23, Hos 11:5, 2Ki 15:29, 1Ch 5:26, Rev 17:12–13, Rev 17:16, 2Ki 17:3–6, 2Ki 18:9–12
- 10Ezk 23:29, Hos 2:10, Hos 2:3, Jer 22:8–9, Ezk 16:37–41, Ezk 23:48
- 11Jer 3:8–11, Ezk 16:47–51, Ezk 23:4
- 122Ki 16:7–15, 2Ch 28:16–23, Ezk 23:5–6, Ezk 23:23, Ezk 16:28
- 132Ki 17:18–19, Ezk 23:31, Hos 12:1–2
- 14Ezk 8:10, Jer 22:14, Isa 46:1, Jer 50:2, Ezk 16:29
- 15Isa 22:21, Jdg 8:18, 2Sa 14:25, 1Sa 18:4
- 16Ezk 16:29, Mat 5:28, Gen 3:6, Ezk 16:17, Job 31:1, Gen 39:7, 2Ki 24:1, Ezk 23:40–41
- 17Ezk 23:22, Ezk 23:28, Gen 11:9, Ezk 16:37, 2Sa 13:15, Gen 10:10
- 18Psa 78:59, Psa 106:40, Jer 12:8, Ezk 21:24, Jer 8:12, Jer 6:8, Isa 3:9, Amo 6:8
- 19Ezk 23:3, Ezk 20:7, Ezk 16:51, Ezk 23:14, Ezk 23:21, Ezk 16:22, Amo 4:4, Ezk 23:8
- 20Ezk 16:26, Ezk 17:15, Ezk 16:20, Jer 5:8
- 22Ezk 16:37, Rev 17:16, Ezk 23:9, Jer 6:22–23, Isa 10:5–6, Jer 12:9–12, Ezk 23:28, Hab 1:6–10
- 23Jer 50:21, 2Ki 20:14–17, 2Ki 24:2, Isa 23:13, Gen 2:14, Gen 25:18, Ezk 23:6, Ezk 23:12
- 24Ezk 23:45, Ezk 26:10, Ezk 16:38, 2Sa 24:14, Nam 2:3–4, Jer 39:5–6, Jer 47:3, Nam 3:2–3
- 25Ezk 23:47, Ezk 5:13, Ezk 8:1–18, Ezk 20:47–48, Hos 2:4–5, Ezk 15:6–7, Ezk 16:38–42, Exo 34:14
- 26Ezk 16:39, Jer 13:22, Ezk 23:29, Rev 17:16, Hos 2:9–10, Ezk 16:37, Isa 3:17–24, 1Pe 3:3–4
- 27Ezk 16:41, Ezk 23:19, Ezk 23:3, Zec 13:2, Mic 5:10–14, Ezk 22:15, Isa 27:9
- 28Ezk 23:22, Jer 34:20, Ezk 23:17, Ezk 16:37, Jer 21:7–10, Jer 24:8
- 29Ezk 16:39, Ezk 23:25–26, Ezk 23:45–47, Ezk 23:18, 2Sa 13:15, Ezk 16:36–37, Deu 28:47–51
- 30Ezk 6:9, Ezk 23:7, Jer 22:8–9, Ezk 23:12–21, Jer 2:18–20, Psa 106:35–38, Jer 16:11–12
- 31Jer 7:14–15, 2Ki 21:13, Ezk 23:13, Ezk 16:47–51, Dan 9:12, Jer 3:8–11, Jer 25:15
- 32Psa 60:3, Isa 51:17, Ezk 22:4–5, Rev 18:6, Jer 25:9, Jer 25:15–28, 1Ki 9:7, Ezk 35:15
- 33Isa 51:17, Jer 25:27, Jer 25:15–16, Isa 51:22, Hab 2:16
- 34Psa 75:8, Isa 51:17, Ezk 23:3, Ezk 23:8, Rev 18:7
- 351Ki 14:9, Isa 17:10, Ezk 22:12, Jer 3:21, Jer 32:33, Jer 2:32, Num 14:34, Hos 8:14
- 36Ezk 22:2, Ezk 20:4, Isa 58:1, Ezk 16:2, Jer 1:10, 1Co 6:2–3, Luk 11:39–52, Mic 3:8–11
- 37Ezk 16:36, Ezk 16:20–21, Jer 7:31, Jer 32:35, Ezk 20:26, Ezk 16:38, Psa 106:37–38, Ezk 23:4–5
- 38Ezk 20:13, Ezk 7:20, 2Ki 21:7, Ezk 20:24, Ezk 8:5–16, Neh 13:17–18, 2Ki 23:11–12, Ezk 22:8
- 392Ki 21:4, Ezk 44:7, Jer 23:11, Ezk 23:38, Mic 3:11, 2Ch 33:4–7, Jhn 18:28, Jer 11:15
- 402Ki 9:30, Jer 4:30, Ezk 16:13–16, Isa 57:9, Isa 3:18–23, Rut 3:3, Pro 7:10, Est 2:12
- 41Est 1:6, Amo 6:4, Isa 65:11, Jer 44:17, Ezk 44:16, Isa 57:7, Pro 7:16–17, Amo 2:8
- 42Ezk 16:11–12, Exo 32:18–19, Hos 13:6, Rev 12:3, Jol 3:8, Amo 6:1–6, Exo 32:6, Gen 24:30
- 43Ezk 23:3, Ezr 9:7, Jer 13:23, Psa 106:6, Dan 9:16
- 44Ezk 23:3, Ezk 23:9–13
- 45Ezk 23:36–39, Hos 6:5, Ezk 16:38–43, Lev 20:10, Lev 21:9, Deu 22:21–24, Zec 1:6, Jhn 8:3–7
- 46Ezk 16:40, Jer 15:4, Jer 24:9, Ezk 23:22–26, Jer 34:17, Jer 25:9
- 47Ezk 24:21, Ezk 16:40–41, Jer 39:8, Ezk 23:25, Ezk 9:6, Jer 33:4–5, Ezk 23:29, 2Ch 36:17–19
- 48Ezk 6:6, Ezk 16:41, 2Pe 2:6, Ezk 23:27, Zep 1:3, Ezk 36:25, Ezk 5:15, Deu 13:11
- 49Ezk 9:10, Ezk 7:4, Isa 59:18, Ezk 6:7, Ezk 20:38, Ezk 7:9, Ezk 23:35, Ezk 22:31
Temas neste capítulo
43
Adultery, Aholah, Aholibah, Armies, Backsliders, Captive, Church, Colors, Cosmetics, Crown, Cup, Drunkenness, Dyeing, Eyelids, Ezekiel, Fire, Forgetting God, God, Helmet, Idolatry, Israel, Prophecies Concerning, Jealousy, Jerusalem, Jewels, Koa, Molech, Nose, Offerings, Oil, Painting, Parables, Pekod, Prophecy, Punishment, Sabbath, Sabeans, Shoa, Sin, Tabernacle, Vermilion, Vision, War, Whoredom