Nehemia 3
1 Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walienda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
2 Wanaume wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
3 Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
4 Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
5 Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
6 Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
7 Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ng’ambo ya Frati.
8 Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu kufikia Ukuta Mpana.
9 Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
10 Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
11 Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
12 Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
13 Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa dhiraa elfu moja hadi Lango la Samadi.
14 Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
15 Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
16 Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, hadi kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
17 Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
18 Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
19 Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, hadi kwenye pembe ya ukuta.
20 Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, hadi kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
21 Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu hadi mwisho wake.
22 Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
23 Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
24 Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria hadi kwenye pembe ya ukuta.
25 Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, hadi kwenye mnara wa juu ambao unachomoka kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
26 na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliochomoza.
27 Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa unaochomoza hadi ukuta wa Ofeli.
28 Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
29 Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
30 Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
31 Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati hadi kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
32 Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.
Références croisées
146
- 1Neh 12:39, Jer 31:38, Jhn 5:2, Zec 14:10, Neh 3:32, Pro 3:9, Neh 13:28, Neh 12:30
- 2Neh 7:36, Ezr 2:34, Neh 10:12
- 32Ch 33:14, Neh 12:39, Neh 2:8, Zep 1:10, Neh 7:1, Neh 6:1, Neh 3:6
- 4Ezr 8:33, Neh 3:21, Neh 10:7, Neh 10:15
- 5Neh 3:27, 2Sa 14:2, Mat 11:29, Amo 1:1, Jdg 5:23, Jer 27:12, 1Ti 6:17–18, Jer 27:2
- 6Neh 12:39
- 72Sa 21:2, Neh 2:7–8, 2Ch 16:6, Neh 3:19, Jos 9:3–27
- 8Neh 12:38, Neh 3:31–32, Exo 30:25, Ecc 10:1, Gen 50:2, Isa 46:6
- 9Neh 3:12, Neh 3:17
- 10Neh 10:4, Neh 3:23, Neh 3:28–30
- 11Neh 12:38, Ezr 2:6, Neh 7:11, Neh 10:14, Neh 10:5, Ezr 8:4
- 12Neh 3:9, Act 21:8–9, Php 4:3, Exo 35:25, Neh 3:14–18
- 13Neh 2:13, Jos 15:34, Jos 15:56, Neh 11:30, 1Ch 4:18, 2Ch 26:9
- 14Jer 6:1, Neh 2:13, Neh 3:15–18, Neh 3:12–13, Neh 3:9, Neh 12:31
- 15Jhn 9:7, Isa 8:6, Neh 12:37, Luk 13:4, Neh 2:14, Jdg 20:3, 2Ki 25:4, Jdg 20:1
- 16Neh 3:12, Neh 3:9, Act 2:29, 2Ki 20:20, Neh 3:14, Isa 7:3, Isa 22:11, Jos 15:58
- 17Jos 15:44, Neh 3:16, 1Sa 23:1–13, 1Ch 23:4
- 192Ch 26:9, Neh 10:9, Neh 12:8
- 20Neh 3:1, Ecc 9:10, Rom 12:11, Neh 13:4, Neh 12:22–23, Neh 13:28, Neh 3:21
- 21Ezr 2:61, Neh 7:63
- 22Neh 12:28, Neh 6:2
- 23Neh 10:2, Neh 8:4, Neh 3:10, Neh 8:7, Neh 3:29–30
- 24Neh 3:19, Neh 10:9, Neh 3:27, Neh 3:11
- 25Jer 32:2, Jer 37:21, Ezr 2:3, Jer 33:1, Neh 12:39, Jer 22:14, Neh 7:8, Jer 39:8
- 26Neh 8:1, Neh 11:21, Neh 8:3, Neh 12:37, 2Ch 33:14, Neh 8:16, 2Ch 27:3, 1Ch 9:2
- 27Neh 3:5
- 28Jer 31:40, 2Ch 23:15, 2Ki 11:16, Neh 3:23, Neh 3:10
- 29Ezr 10:2, Neh 7:40, Ezr 2:37, Jer 19:2
- 31Neh 3:8, Neh 3:32
- 32Neh 3:1, Neh 12:39, Jhn 5:2, Neh 3:31, Neh 3:8
Thèmes dans ce chapitre
89
Ananiah, Apothecary, Armies, Armory, Azbuk, Baana, Bani, Baruch, Bavai, Benjamin, Berechiah, Besodeiah, Beth-Haccerem, Beth-Zur, Binnui, Cities, Commerce, Eliashib, Ezer, Fish Gate, Gihon, Goldsmith, Government, Hakkoz, Halohesh, Hananeel, Hananiah, Harhaiah, Harumaph, Hashabiah, Hashabniah, Hashub, Hattush, Henadad, Hezekiah, Hur, Immer, Imri, Israel, Prophecies Concerning, Jedaiah, Jehoiada, Jericho, Jerusalem, Jeshua, Keilah, Koz, Liberality, Lock, Lukewarmness, Maaseiah, Malchiah, Meah, Melatiah, Merchant, Meremoth, Meshezabeel, Meshullam, Mizpah, Nehemiah, Nethinims, Ophel, Pahath-Moab, Palal, Paseah, Pedaiah, Persia, Phaseah, Pool, Rechab, Rehum, Rephaiah, Shallum, Shallun, Shechaniah, Sheep Gate, Shelemiah, Shemaiah, Siloam, Stairs, Tekoah, Tower, Uriah, Uzai, Uzziel, Zabbai, Zaccur, Zadok, Zalaph, Zanoah