Yohana 3
1 Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
2 Huyu alimjia Isa usiku akamwambia, “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
3 Isa akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
4 Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
5 Isa akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
6 Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
7 Kwa hiyo usishangae ninapokuambia, ‘Huna budi kuzaliwa mara ya pili.’
8 Upepo huvuma kokote unakopenda. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu unakotoka wala unakoenda. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
9 Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
10 Isa akamwambia, “Wewe ni mwalimu wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
11 Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
12 Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
13 Hakuna mtu yeyote aliyeenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani Mwana wa Adamu.
14 Kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu,
15 ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele.
16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
17 Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
18 Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
19 Hii ndiyo hukumu: Kwamba nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru, kwa sababu matendo yao ni maovu.
20 Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
21 Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
22 Baada ya haya, Isa na wanafunzi wake walienda katika eneo la Yudea, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza watu.
23 Yahya naye alikuwa akibatiza watu huko Ainoni karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na maji mengi. Watu wakamjia huko ili kubatizwa.
24 (Hii ilikuwa kabla Yahya hajafungwa gerezani.)
25 Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yahya na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
26 Wakamwendea Yahya wakamwambia, “Mwalimu, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ng’ambo ya Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
27 Yahya akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
28 Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Al-Masihi, ila nimetumwa nimtangulie.’
29 Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
30 Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kupungua.
31 “Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
33 Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
34 Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humpa Roho wake pasipo kipimo.
35 Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mkononi mwake.
36 Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.”
Referencias cruzadas
271
- 1Jhn 19:39, Jhn 3:10, Jhn 7:47–50, Luk 23:13
- 2Jhn 5:36, Act 10:38, Act 2:22, Jhn 9:30–33, Act 4:16–17, Jhn 9:16, Mat 22:16, Jhn 12:37
- 32Co 5:17, Jhn 3:5–6, 1Pe 1:23–25, 1Jn 3:9, 1Jn 5:1, Tit 3:5, Jhn 1:13, 1Jn 2:29
- 41Co 2:14, 1Co 1:18, Jhn 3:3, Jhn 4:11–12, Jhn 6:53, Jhn 6:60
- 5Ezk 36:25–27, Eph 5:26, Act 2:38, 1Pe 3:21, 1Co 6:11, 1Jn 5:6–8, Isa 44:3–4, Tit 3:4–7
- 6Gal 5:16–21, Ezk 36:26–27, Rom 8:4–9, 2Co 5:17, 1Co 15:47–50, 1Co 6:17, Rom 7:18, 1Jn 3:9
- 7Jhn 3:3, Eph 4:22–24, Rom 12:1–2, Jhn 3:12, Rev 21:27, 1Pe 1:22, Mat 13:33–35, Col 1:12
- 8Ecc 11:4–5, 1Co 2:11, Act 2:2, Ezk 37:9, 1Jn 2:29, Mrk 4:26–29, Act 4:31, Jhn 1:13
- 9Isa 42:16, Jhn 6:60, Jhn 6:52, Luk 1:34, Jhn 3:4, Pro 4:18, Mrk 8:24–25
- 10Mat 22:29, Jer 8:8–9, Ezk 11:19, Mat 15:14, Psa 51:6, Ezk 36:25–27, Psa 51:10, Psa 73:1
- 11Jhn 8:38, 1Jn 5:6–12, Jhn 12:49, Jhn 14:24, Jhn 1:18, Jhn 8:14, Jhn 8:28–29, Jhn 7:16
- 121Co 3:1–2, 1Co 2:7–9, Jhn 3:31–36, Heb 5:11, 1Pe 2:1–3, Jhn 3:5, Jhn 3:13–17, Jhn 1:1–14
- 13Pro 30:4, Jhn 6:38, Act 2:34, Jhn 1:18, Jhn 13:3, 1Co 15:47, Eph 4:9–10, Rom 10:6
- 14Num 21:7–9, Jhn 8:28, Jhn 12:32–34, Luk 24:26–27, Luk 24:44–46, Psa 22:16, 2Ki 18:4, Mat 26:54
- 15Jhn 3:16, Jhn 6:40, Jhn 3:36, Jhn 12:44–46, 1Jn 5:11–13, Rom 10:9–14, Jhn 10:28–30, 1Jn 5:20
- 16Rom 5:8, 1Jn 4:9–10, Rom 8:32, Jhn 3:15, Jhn 11:25–26, Jhn 6:40, Jhn 3:36, 1Jn 4:19
- 171Jn 4:14, Luk 19:10, Jhn 12:47–48, Jhn 6:57, Jhn 6:40, Jhn 6:29, 1Ti 2:5–6, Jhn 20:21
- 181Jn 5:10, Mrk 16:16, Rom 8:1, Jhn 5:24, 1Jn 5:12, Jhn 3:36, Rom 5:1, 1Jn 4:9
- 19Jhn 8:12, 2Th 2:12, Jhn 9:39–41, Rom 2:8, Jhn 12:43, Rom 1:32, Jhn 5:44, 2Pe 3:3
- 20Eph 5:11–13, Jhn 7:7, Job 24:13–17, Pro 4:18, Pro 1:29, Jas 1:23–25, 1Ki 22:8, Psa 50:17
- 211Jn 1:6, Psa 139:23–24, 3Jn 1:11, Eph 5:9, Php 2:13, Psa 119:105, 1Jn 4:15–16, 1Jn 2:27–29
- 22Jhn 4:1–3, Jhn 3:26, Jhn 7:3
- 23Mrk 1:4–5, Luk 3:7, Mat 3:5–6, 1Sa 9:4, Ezk 43:2, Ezk 19:10, Gen 33:18, Jer 51:13
- 24Mat 4:12, Mat 14:3, Mrk 6:17, Luk 9:7–9, Luk 3:19–20
- 25Jhn 2:6, Mat 3:11, Heb 6:2, Heb 9:10, 1Pe 3:21, Heb 9:23, Heb 9:13–14, Mrk 7:8
- 26Jhn 1:7, Jhn 1:15, Jas 3:14–18, Gal 6:12–13, Jhn 12:19, Act 19:26–27, Jhn 1:26–36, Isa 45:23
- 27Jas 1:17, 1Co 4:7, 1Co 15:10, 1Pe 4:10–11, 1Co 2:12–14, Amo 7:15, Jer 1:5, Mat 25:15
- 28Jhn 1:20, Jhn 1:23, Luk 1:16–17, Mat 3:11–12, Mal 3:1, Jhn 1:25, Luk 1:76, Mrk 1:2–3
- 29Isa 54:5, Hos 2:19, Eph 5:25–27, Mat 9:15, Ezk 16:8, Rev 21:9, Rev 19:7–9, Php 2:2
- 30Col 1:18, Psa 72:17–19, Heb 3:2–6, Isa 9:7, 1Co 3:5, Rev 11:15, Act 13:36–37, Dan 2:34–35
- 31Mat 28:18, Jhn 8:23, Rom 9:5, Jhn 6:33, 1Jn 4:5, Jhn 3:12–13, Php 2:9–11, Jhn 6:51
- 32Jhn 3:11, Jhn 15:15, Jhn 8:26, Jhn 1:11, Jhn 5:20, Jhn 3:33
- 33Eph 1:13, Heb 6:17, Tit 1:1–2, 2Co 1:18, Jhn 6:27, Rom 4:18–21, 2Co 1:22, Rom 3:3–4
- 34Act 10:38, Mat 12:18, Jhn 15:26, Jhn 5:26, Col 2:9, Isa 11:2–5, Luk 4:18, Jhn 7:37–39
- 35Mat 28:18, Jhn 5:20, Luk 10:22, Jhn 5:22, Jhn 17:2, Mat 11:27, Eph 1:22, 1Co 15:27
- 36Jhn 5:24, Jhn 1:12, 1Th 5:9, Eph 5:6, Jhn 3:15–16, 1Jn 5:10–13, Rom 1:17–18, Rom 5:9
Temas en este capítulo
49
Baptism, Blindness, Brazen Serpent, Character, Condescension of God, Cowardice, Darkness, Depravity of Man, Enon (Aenon), Faith, Gifts From God, God, Heart, Heredity, Holy Spirit, Humility, Immortality, Jesus, the Christ, John, Judgment, Life, Light, Man, Meteorology and Celestial Phenomena, Minister, Christian, Miracles, Mysteries, Nicodemus, Opinion, Public, Pharisees, Power, Rabbi, Regeneration, Responsibility, Righteous, Righteousness, Salim, Salvation, Scriptures, Sign, Sin, Symbols and Similitudes, Trinity, Types, Unbelief, Wicked (People), Wind, Word of God, Works