Ezekieli 37
1 Mkono wa Mwenyezi Mungu ulikuwa juu yangu, naye akanitoa nje kwa Roho wa Mwenyezi Mungu na kuniweka katikati ya bonde lililokuwa limejaa mifupa tele.
2 Akanipitisha pande zote kwenye hiyo mifupa, nami nikaona mifupa mingi sana ndani ya lile bonde, mifupa iliyokuwa imekauka sana.
3 Akaniuliza, “Mwanadamu, mifupa hii yaweza kuishi?” Nikajibu, “Ee Bwana Mungu Mwenyezi, wewe peke yako unajua.”
4 Ndipo akaniambia, “Itabirie mifupa hii na uiambie, ‘Enyi mifupa mikavu, sikieni neno la Mwenyezi Mungu!
5 Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi kwa hii mifupa: Nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi.
6 Nitawawekea mishipa, nami nitaifanya nyama ije juu yenu na kuwafunika kwa ngozi. Nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtakuwa hai. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’ ”
7 Basi nikatabiri kama nilivyoamriwa. Nilipokuwa nikitabiri, kukawa na sauti, sauti ya kugongana, nayo mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe.
8 Nikatazama: mishipa na nyama vikatokea juu ya mifupa na ngozi ikaifunika, lakini haikuwa na pumzi ndani yake.
9 Ndipo aliponiambia, “Utabirie pumzi; tabiri, mwanadamu na uiambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Njoo kutoka pande nne za pepo, ee pumzi, nawe upulizie pumzi ndani ya hawa waliouawa, ili wapate kuishi.’ ”
10 Hivyo nikatabiri kama alivyoniamuru, nayo pumzi ikawaingia, wakawa hai na wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.
11 Ndipo akaniambia: “Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli. Nao wanasema, ‘Mifupa yetu imekauka na tumaini letu limetoweka, tumekatiliwa mbali.’
12 Hivyo watabirie na uwaambie: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Enyi watu wangu, nitayafunua makaburi yenu na kuwatoa ndani yake, nami nitawarudisha tena katika nchi ya Israeli.
13 Ndipo ninyi watu wangu, mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapoyafunua makaburi yenu na kuwatoa humo.
14 Nitatia Roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi; nami nitawakalisha katika nchi yenu wenyewe. Ndipo mtajua kuwa Mimi Mwenyezi Mungu nimenena, nami nitalitenda, asema Mwenyezi Mungu!’ ”
15 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
16 “Mwanadamu, chukua fimbo na uandike juu yake, ‘Hii ni kwa ajili ya Yuda na Waisraeli waliofungamana naye.’ Kisha chukua fimbo nyingine, uandike juu yake, ‘Fimbo ya Efraimu, ni kwa ajili ya Yusufu na nyumba yote ya Israeli wanaofungamana naye.’
17 Ziunganishe pamoja kuwa fimbo moja ili ziwe fimbo moja katika mkono wako.
18 “Watu wako watakapokuuliza, ‘Je, hutatuambia ni nini maana ya jambo hili?’
19 Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitaichukua fimbo ya Yusufu iliyo mkononi mwa Efraimu, na ya makabila ya Israeli yanayofungamana naye, na kuiunganisha na fimbo ya Yuda, nikizifanya kuwa fimbo moja, nao watakuwa mmoja katika mkono wangu.’
20 Inua mbele ya macho yao zile fimbo ulizoziandika
21 kisha waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitawatoa Waisraeli katika mataifa walikokuwa wameenda. Nitawakusanya popote walipo na kuwarudisha katika nchi yao wenyewe.
22 Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi, katika milima ya Israeli. Patakuwa na mfalme mmoja juu yao wote na kamwe hawatagawanyika tena kuwa mataifa mawili au kugawanyika katika falme mbili.
23 Hawatajitia tena unajisi kwa sanamu zao, au vinyago vyao vinavyochukiza, wala kwa makosa yao yoyote, kwa maana nitawaokoa kutoka dhambi zao zote zilizowarudisha nyuma, nami nitawatakasa. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
24 “ ‘Mtumishi wangu Daudi atakuwa mfalme juu yao, nao wote watakuwa na mchungaji mmoja. Watafuata sheria zangu na kuzishika amri zangu kwa uangalifu.
25 Wataishi katika nchi niliyompa mtumishi wangu Yakobo, nchi ambamo baba zenu waliishi. Wao na watoto wao na watoto wa watoto wao wataishi humo milele, naye Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao milele.
26 Nitafanya agano la amani nao; litakuwa agano la milele. Nitawafanya imara na kuongeza idadi yao, nami nitaweka mahali patakatifu pangu miongoni mwao milele.
27 Maskani yangu yatakuwa pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
28 Ndipo mataifa watajua kuwa Mimi Mwenyezi Mungu ndiye ninayeifanya Israeli kuwa takatifu, wakati mahali patakatifu pangu patakuwa miongoni mwao milele.’ ”
Referencias cruzadas
172
- 1Ezk 3:22, Ezk 1:3, Act 8:39, Ezk 33:22, Jer 7:32, Ezk 8:3, 1Ki 18:12, Luk 4:1
- 2Psa 141:7, Ezk 37:11
- 3Jhn 11:25–26, Jhn 5:21, Deu 32:39, Rom 4:17, Heb 11:19, 2Co 1:9–10, 1Sa 2:6, Act 26:8
- 4Jhn 5:25, Jhn 5:28–29, Mat 21:21, Ezk 36:1, Jer 22:29, Isa 26:19, Ezk 37:11, Jhn 2:5
- 5Psa 104:29–30, Gen 2:7, Ezk 37:14, Ezk 37:9–10, Jhn 20:22, Eph 2:5, Rom 8:2
- 6Jol 2:27, Isa 49:23, Jol 3:17, Ezk 37:14, Ezk 35:9, 1Ki 20:28, Ezk 39:6, Ezk 38:23
- 7Act 2:2, 1Ki 19:11–13, Act 4:19, Act 16:26–29, Jer 13:5–7, Act 5:20–29, Jer 26:8, Act 2:37
- 9Jhn 3:8, Sng 4:16, Ezk 37:5, Ezk 37:14, Psa 104:30
- 10Rev 11:11, Psa 104:30, Rev 20:4–5
- 11Eph 2:1, Psa 77:7–9, Ezk 39:25, Ezk 36:10, Jer 31:1, Isa 49:14, Ezk 37:1–8, Hos 1:11
- 12Isa 26:19, Hos 13:14, 1Th 4:16, Amo 9:14–15, Isa 66:14, Rev 20:13, Hos 6:2, Ezk 36:24
- 13Ezk 37:6, Ezk 16:62, Psa 126:2–3
- 14Jol 2:28–29, Ezk 36:27, Ezk 11:19, Ezk 36:36, Ezk 39:29, 1Co 15:45, Ezk 17:24, Ezk 37:9
- 162Ch 15:9, 2Ch 10:19, 2Ch 10:17, Num 17:2–3, 1Ki 12:16–20, 2Ch 11:11–17, 2Ch 30:11–18
- 17Hos 1:11, Jer 50:4, Isa 11:13, Zep 3:9, Ezk 37:22–24
- 18Ezk 24:19, Ezk 12:9, Ezk 20:49, Ezk 17:12
- 19Zec 10:6, Eph 2:13–14, Col 3:11, Ezk 37:16–17, 1Ch 9:1–3
- 20Ezk 12:3, Num 17:6–9, Hos 12:10
- 21Ezk 36:24, Jer 23:8, Jer 29:14, Jer 16:15, Amo 9:14–15, Jer 32:37, Ezk 34:13, Isa 11:11–16
- 22Ezk 37:24, Ezk 34:23–24, Jer 50:4, Jer 3:18, Luk 1:32–33, Isa 11:12–13, Hos 1:11, Isa 9:6–7
- 23Rev 21:3–4, 1Jn 1:9, Ezk 36:28–29, Rev 21:7, Zec 13:1–2, Eph 5:26–27, 1Jn 1:7, Hos 14:8
- 24Ezk 34:23–24, Hos 3:5, Ezk 37:25, Jer 30:9, Jer 23:5, Ezk 36:27, Jer 31:33, Tit 2:11–13
- 25Amo 9:15, Ezk 37:24, Ezk 28:25, Ezk 36:28, Isa 9:6–7, Ezk 37:21, Isa 60:21, Ezk 37:26
- 26Isa 55:3, Ezk 34:25, Jer 30:19, Lev 26:11–12, 2Co 6:16, Heb 13:20–21, Ezk 43:7, Ezk 16:62
- 27Rev 21:3, Col 2:9–10, Jhn 1:14, Ezk 37:23, Lev 26:11–12, 2Co 6:16, Ezk 36:28, Ezk 11:20
- 28Jhn 17:17–19, Ezk 20:12, Exo 31:13, 1Co 1:30, Eph 5:26, Lev 21:8, 1Th 5:23, Ezk 36:23