Ezekieli 11
1 Ndipo Roho wa Mungu akaniinua na kunileta hadi kwenye lango la nyumba ya Mwenyezi Mungu linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango palikuwa na wanaume ishirini na watano. Nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
2 Mwenyezi Mungu akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
3 Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
4 Kwa hiyo tabiri dhidi yao; tabiri, ewe mwanadamu.”
5 Kisha Roho wa Mwenyezi Mungu akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
6 Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
7 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Maiti mlizozitupa huko ndizo nyama, na mji huu ndio chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
8 Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta dhidi yenu, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
9 Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
10 Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
11 Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
12 Nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
13 Basi nilipokuwa nikitoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu, nikasema, “Ee Bwana Mungu Mwenyezi! Je, utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
14 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia, kusema:
15 “Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu nawe pamoja na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema kuwahusu, ‘Wako mbali na Mwenyezi Mungu; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
16 “Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, hata hivyo, kwa kitambo kidogo, nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizoenda.’
17 “Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitawakusanya kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
18 “Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za kuchukiza.
19 Nitawapa moyo usiogawanyika na kuweka roho mpya ndani yao; nitaondoa ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
20 Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
21 Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za kuchukiza, nitawalipa kikamilifu kulingana na matendo yao,” asema Bwana Mungu Mwenyezi.
22 Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
23 Basi utukufu wa Mwenyezi Mungu ukapaa juu kuanzia katika mji na kutua juu ya mlima ulio mashariki mwa mji.
24 Roho akaniinua na kunileta kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
25 nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Mwenyezi Mungu alichokuwa amenionesha.
Referencias cruzadas
170
- 1Ezk 3:12, Ezk 3:14, Ezk 8:16, Ezk 8:3, Ezk 11:24, Ezk 11:13, Ezk 37:1, Isa 1:23
- 2Isa 30:1, Psa 2:1–2, Jer 5:5, Psa 52:2, Isa 59:4, Mic 2:1–2, Est 8:3, Psa 36:4
- 3Ezk 12:22, Ezk 12:27, Isa 5:19, Ezk 11:7–11, Ezk 7:7, Ezk 24:3–14, Amo 6:5, 2Pe 3:4
- 4Hos 8:1, Isa 58:1, Hos 6:5, Ezk 21:2, Ezk 20:46–47, Ezk 3:17–21, Ezk 3:2–15, Ezk 25:2
- 5Jer 17:10, Ezk 2:2, Rev 2:23, Jer 16:17, Isa 58:1, Ezk 2:7, 1Sa 10:6, Mal 3:13–14
- 6Ezk 7:23, Isa 1:15, Ezk 22:2–6, Ezk 22:12, Ezk 22:27, Hos 4:2–3, Mic 3:2–3, Jer 2:34
- 7Mic 3:2–3, Ezk 24:3–13, Jer 52:24–27, 2Ki 25:18–22, Ezk 3:9–11
- 8Pro 10:24, Isa 66:4, Isa 24:17–18, Job 3:25, Jhn 11:48, Job 20:24, Jer 44:12–13, 1Th 2:15–16
- 9Ezk 5:8, Deu 28:36, Psa 106:41, Ezk 16:41, Deu 28:49–50, Ezk 21:31, Ecc 8:11, Ezk 5:10
- 102Ki 14:25, 2Ki 25:19–21, Jer 39:6, Ezk 6:7, Jer 52:9–10, Ezk 13:9, Num 34:8–9, Jer 9:24
- 11Ezk 11:3, Ezk 11:7–10
- 12Ezk 8:10, Ezk 8:14, Ezk 8:16, Psa 106:35–39, 2Ki 18:12, 2Ch 28:3, Neh 9:34, Ezk 11:21
- 13Ezk 11:1, Ezk 9:8, Act 5:5, Deu 7:4, Jer 28:15–17, Psa 106:23, Amo 7:2, 1Ki 13:4
- 15Ezk 33:24, Isa 66:5, Jhn 16:2, Isa 65:5, Jer 24:1–5
- 16Isa 8:14, Psa 90:1, Deu 30:3–4, Psa 91:1, Psa 31:20, Lev 26:44, Jer 31:10, Jer 30:11
- 17Ezk 28:25, Jer 3:18, Ezk 34:13, Isa 11:11–16, Jer 24:5, Ezk 36:24, Jer 3:12, Ezk 20:41
- 18Ezk 37:23, Ezk 5:11, Ezk 7:20, Ezk 42:7–8, Isa 30:22, Ezk 11:21, Mic 5:10–14, Isa 1:25–27
- 19Ezk 36:26–27, Jer 31:33, Psa 51:10, Jer 32:39–40, Jer 24:7, Deu 30:6, 2Co 3:3, Ezk 18:31
- 20Ezk 14:11, Psa 105:45, Tit 2:11–12, Jer 30:22, Luk 1:6, Jer 31:33, Psa 119:4–5, Ezk 37:27
- 21Ecc 11:9, Ezk 9:10, Jas 1:14–15, Jer 1:16, Ezk 11:18, Ezk 22:31, Ezk 20:31, Mrk 7:21–23
- 22Ezk 10:19, Ezk 1:19–20
- 23Zec 14:4, Ezk 8:4, Ezk 10:4, Ezk 43:2, Ezk 9:3, Ezk 43:4, Ezk 10:18, Mat 23:37–24:2
- 24Ezk 3:12, Ezk 8:3, Ezk 11:1, Act 10:16, Ezk 1:3, Gen 35:13, 2Co 12:2–4, 2Ki 2:16
- 25Ezk 3:4, Ezk 3:17, Ezk 3:27, Ezk 2:7
Temas en este capítulo
28
Afflictions and Adversities, Azur, Backsliders, Benaiah, Caldron, Cloud, Ezekiel, Gifts From God, God, Heart, Holy Spirit, Infidelity, Intercession, Israel, Prophecies Concerning, Jaazaniah, Judgments, Pelatiah, Procrastination, Prophecy, Prophets, Regeneration, Repentance, Sanctuary, Scoffing, Sin, Wheel, Wicked (People), Word of God