Mwanzo 50
1 Basi Yusufu akamwangukia baba yake, akalilia juu yake na akambusu.
2 Ndipo Yusufu akawaagiza matabibu waliokuwa wakimhudumia, wamtie baba yake Israeli dawa asioze. Hivyo matabibu wakamtia dawa asioze,
3 wakatumia siku arobaini, muda uliohitajika kutia dawa asioze. Nao Wamisri wakamwombolezea Yakobo kwa siku sabini.
4 Siku za kumwombolezea zilipokwisha, Yusufu akawaambia washauri wa Farao, “Kama nimepata kibali machoni penu semeni na Farao kwa ajili yangu. Mwambieni,
5 ‘Baba yangu aliniapisha na kuniambia, “Mimi niko karibu kufa; unizike katika kaburi lile nililochimba kwa ajili yangu mwenyewe katika nchi ya Kanaani.” Sasa nakuomba uniruhusu niende kumzika baba yangu, nami nitarudi.’ ”
6 Farao akasema, “Panda, uende kumzika baba yako, kama alivyokuapiza kufanya.”
7 Hivyo Yusufu akapanda kwenda kumzika baba yake. Maafisa wote wa Farao wakaenda pamoja naye, watu mashuhuri wa baraza lake, na watu mashuhuri wote wa Misri.
8 Hawa ni mbali na watu wote wa nyumbani mwa Yusufu, na ndugu zake, na wale wote wa nyumbani mwa baba yake. Ni watoto wao, makundi yao ya kondoo, mbuzi na ng’ombe tu waliobakia katika nchi ya Gosheni.
9 Magari ya vita na wapanda farasi pia walipanda pamoja naye. Likawa kundi kubwa sana.
10 Walipofika kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Atadi, karibu na Yordani, wakalia kwa sauti na kwa uchungu. Yusufu akakaa huko kwa siku saba kumwombolezea baba yake.
11 Wakanaani walioishi huko walipoona maombolezo yaliyofanyika katika sakafu ile ya kupuria ya Atadi, wakasema, “Wamisri wanafanya maombolezo makubwa.” Kwa hiyo mahali pale karibu na Yordani pakaitwa Abel-Mizraimu.
12 Hivyo wana wa Yakobo wakafanya kama baba yao alivyowaagiza:
13 Wakamchukua hadi nchi ya Kanaani, wakamzika kwenye pango katika shamba la Makpela, karibu na Mamre, ambalo Ibrahimu alilinunua kutoka kwa Efroni Mhiti pamoja na shamba liwe mahali pa kuzikia.
14 Baada ya Yusufu kumzika baba yake, akarudi Misri pamoja na ndugu zake na wale wote waliokuwa wameenda naye kumzika baba yake.
15 Ndugu zake Yusufu walipoona kwamba baba yao amekufa, wakasema, “Itakuwaje kama Yusufu ataweka kinyongo dhidi yetu na kutulipa mabaya yote tuliyomtendea?”
16 Kwa hiyo wakampelekea Yusufu ujumbe, wakasema, “Kabla baba yako hajafa aliacha maagizo haya:
17 ‘Hili ndilo mtakalomwambia Yusufu: Ninakuomba uwasamehe ndugu zako dhambi na mabaya kwa vile walivyokutenda vibaya.’ Sasa tafadhali samehe dhambi za watumishi wa Mungu wa baba yako.” Ujumbe huu ulipomfikia, Yusufu akalia.
18 Ndipo ndugu zake wakaja na kujitupa chini mbele yake. Wakasema, “Sisi ni watumwa wako.”
19 Lakini Yusufu akawaambia, “Msiogope. Je, mimi ni badala ya Mungu?
20 Mlikusudia kunidhuru, lakini Mungu alikusudia mema, ili litimie hili linalofanyika sasa, kuokoa maisha ya watu wengi.
21 Hivyo basi, msiogope. Mimi nitawatunza ninyi nyote pamoja na watoto wenu.” Akawafariji na kusema nao kwa wema.
22 Yusufu akakaa katika nchi ya Misri, yeye pamoja na jamaa yote ya baba yake. Akaishi miaka mia moja na kumi,
23 naye akaona kizazi cha tatu cha watoto wa Efraimu. Pia akaona watoto wa Makiri mwana wa Manase, wakawekwa magotini mwa Yusufu walipozaliwa.
24 Ndipo Yusufu akawaambia ndugu zake, “Mimi ninakaribia kufa. Lakini kwa hakika Mungu atawasaidia na kuwachukueni kutoka nchi hii na kuwapeleka katika nchi aliyomwahidi kwa kiapo Ibrahimu, Isaka na Yakobo.”
25 Naye Yusufu akawaapisha wana wa Israeli na kuwaambia, “Hakika Mungu atawasaidia, nanyi ni lazima mhakikishe mmepandisha mifupa yangu kutoka mahali hapa.”
26 Kwa hiyo Yusufu akafa akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi. Baada ya kumtia dawa asioze, akawekwa kwenye jeneza huko Misri.
Cross-references
145
- 1Gen 46:4, Mrk 5:38–39, Act 8:2, Jhn 11:35–38, Deu 6:7–8, Eph 6:4, 1Th 4:13, Gen 23:2
- 2Gen 50:26, 2Ch 16:14, Mrk 16:1, Jhn 19:39–40, Mat 26:12, Jhn 12:7, Mrk 14:8, Luk 24:1
- 3Deu 34:8, Num 20:29, Gen 50:10, Deu 21:13
- 4Gen 18:3, Est 4:2
- 5Isa 22:16, 2Ch 16:14, Mat 27:60, Gen 47:29–31, 1Sa 14:43, Luk 9:59–60, Deu 4:22, Ecc 12:7
- 6Gen 48:21
- 7Gen 14:16
- 8Exo 10:8–9, Num 32:24–27, Exo 10:26
- 9Act 8:2, Exo 14:28, Exo 14:7, Sng 1:9, 2Ki 18:24, Exo 14:17, Gen 46:29, Gen 41:43
- 10Job 2:13, Act 8:2, 2Sa 1:17, 1Sa 31:13, Num 19:11, Deu 1:1, Deu 34:8, Gen 50:11
- 11Gen 10:15–19, Gen 24:6, Gen 13:7, 1Sa 6:18, Deu 3:27, Deu 11:30, Gen 34:30, Gen 50:10
- 12Gen 49:29–32, Act 7:16, Exo 20:12, Gen 47:29–31, Eph 6:1
- 13Gen 49:29–31, Act 7:16, Gen 23:16–18, Gen 35:27, Gen 25:9, Gen 23:20, Gen 35:29, 2Ki 21:18
- 15Pro 28:1, Gen 42:21–22, Job 15:21–22, Gen 27:41–42, Lev 26:36, Psa 53:5, Psa 14:5, Gen 42:17
- 16Pro 29:25
- 17Mat 6:14–15, Eph 4:32, Gen 49:25, Luk 17:3–4, Gen 45:4–5, Pro 28:13, Gen 45:8, Psa 21:11
- 18Gen 37:7–11, Gen 45:3, Gen 27:29, Gen 44:14, Gen 42:6
- 19Rom 12:19, Gen 30:2, Gen 45:5, Heb 10:30, 2Ki 5:7, Job 34:19–29, Deu 32:35, Mat 14:27
- 20Rom 8:28, Psa 119:71, Gen 45:5–8, Gen 37:18–20, Act 2:23, Psa 105:16–17, Act 3:13–15, Gen 37:4
- 21Gen 47:12, 1Pe 3:9, Gen 45:10–11, Rom 12:20–21, Mat 6:14, Mat 5:44, Isa 40:2, 1Th 5:15
- 23Num 32:39, Job 42:16, Gen 30:3, Psa 128:6, Num 32:33, Jos 17:1, Gen 48:19, Gen 49:12
- 24Exo 3:16–17, Gen 35:12, Gen 26:3, Gen 28:13, Gen 46:4, Gen 48:21, Gen 15:18, Gen 13:17
- 25Exo 13:19, Jos 24:32, Act 7:16, Gen 47:29–31, Heb 11:22, Gen 50:5
- 26Gen 50:22, Jos 24:29, Gen 50:2–3, Gen 47:9, Gen 47:28
Topics in this chapter
34
Abel-Mizraim, Afflictions and Adversities, Atad, Bereavement, Brother, Burial, Cave, Children, Coffin, Conviction, Covenant, Egyptians, Embalming, Ephron, Faith, Family, Forgiveness, Forty, God, Government, Jacob, Joseph, Kiss, Longevity, Machir, Machpelah, Mourning, Oath, Repentance, Rulers, Seven, Shechem, Threshing, Weeping