Nehemia 5
1 Wakati huu wanaume na wake zao wakalia kilio kikuu dhidi ya ndugu zao Wayahudi.
2 Baadhi yao walikuwa wakisema, “Sisi na wana wetu wa kiume na wa kike tuko wengi. Ili tuweze kula na kuishi, ni lazima tupate nafaka.”
3 Wengine walikuwa wakisema, “Tunaweka rehani mashamba yetu, mashamba ya mizabibu, na nyumba zetu ili tupate nafaka wakati wa njaa.”
4 Bado kukawa na wengine waliokuwa wakisema, “Ilitubidi tukope fedha ili kulipa kodi ya mfalme kwa ajili ya mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu.
5 Ingawa sisi ni mwili na damu moja sawa na watu wa nchi yetu, na ijapo wana wetu ni wazuri kama wana wao, bado inatupasa kuwatoa wana wetu wa kiume na wa kike kwenye utumwa. Baadhi ya binti zetu wameshakuwa watumwa tayari, lakini hatuna uwezo wa kuwakomboa, kwa sababu mashamba yetu na mashamba ya mizabibu yetu ni mali ya watu wengine.”
6 Niliposikia kilio chao na malalamiko haya, nilikasirika sana.
7 Nikayatafakari katika akili yangu, nikiwalaumu wakuu na maafisa. Nikawaambia, “Mnawaonea ndugu zenu kwa kuwatoza riba!” Basi nikaita mkutano mkubwa ili kukabiliana nao,
8 nikasema: “Kulingana na uwezo wetu, tumewakomboa ndugu zetu Wayahudi waliokuwa wameuzwa kwa watu wasioamini. Sasa mnawauza ndugu zenu, ili wauzwe tena kwetu!” Wakanyamaza, kwa sababu hawakupata chochote cha kusema.
9 Basi nikaendelea kusema, “Mnachokifanya si sawa. Je, haikuwapasa kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili tuepukane na shutuma za adui zetu wasioamini?
10 Mimi na ndugu zangu na watu wangu tunawakopesha watu fedha na nafaka. Lakini jambo hili la kutoza riba likome!
11 Warudishieni mara moja mashamba yao, mashamba yao ya mizabibu, mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao, pia riba yao mnayowatoza na sehemu ya fungu la mia la fedha, nafaka, divai mpya na mafuta.”
12 Wakasema, “Tutawarudishia na hatutataka kitu chochote zaidi kutoka kwao. Tutafanya kama ulivyosema.” Kisha nikawaita makuhani na kuwafanya wakuu na maafisa kuapa kufanya kile walichoahidi.
13 Pia nikakung’uta makunjo ya vazi langu na kusema, “Kila mtu ambaye hatatimiza ahadi hii, Mungu na amkung’ute hivi kutoka nyumba yake na katika mali yake. Basi mtu kama huyo akung’utiwe nje na aachwe bila kitu!” Waliposikia hili, mkutano wote ukasema, “Amen,” na wakamtukuza Mwenyezi Mungu. Nao watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.
14 Zaidi ya hayo, kutoka mwaka wa ishirini wa Mfalme Artashasta, wakati nilipoteuliwa kuwa mtawala wao katika nchi ya Yuda, hadi mwaka wake wa thelathini na mbili, yaani miaka kumi na mbili, mimi wala ndugu zangu hatukula chakula ambacho kwa kawaida hupewa watawala.
15 Lakini watawala wa mwanzoni, wale walionitangulia, waliwalemea watu na kuchukua kutoka kwao shekeli arobaini za fedha, pamoja na chakula na mvinyo. Wasaidizi wao pia walijifanya wakuu juu ya watu. Lakini kwa kumheshimu Mungu sikufanya hivyo.
16 Badala yake, nilijitoa kwa bidii katika kazi ya ukuta huu. Watu wangu wote walikutanika pale kwa ajili ya kazi. Hatukujipatia shamba lolote.
17 Zaidi ya hayo, Wayahudi na maafisa mia moja na hamsini walikula mezani pangu, pamoja na wale waliotujia kutoka mataifa jirani.
18 Kila siku niliandaliwa maksai mmoja, kondoo sita wazuri, na kuku, na mvinyo wa kila aina kwa wingi kila baada ya siku kumi. Licha ya mambo haya yote, sikudai chakula kilichokuwa fungu la mtawala, kwa sababu madai yalikuwa mazito sana kwa watu hawa.
19 Unikumbuke kwa fadhili, Ee Mungu wangu, kwa yote niliyofanya kwa ajili ya watu hawa.
Mga kaugnay na talata
134
- 1Isa 5:7, Deu 15:7–11, 1Co 6:6–8, Lev 25:35–37, Jas 5:4, Exo 22:25–27, Job 31:38–39, Exo 3:7
- 2Mal 2:2, Psa 128:2–4, Psa 127:3–5, Gen 42:2, Gen 43:8, Gen 41:57
- 3Lev 25:35–39, Mal 3:8–11, Gen 47:15–25, Deu 15:7
- 4Ezr 4:13, Ezr 4:20, Deu 28:47–48, Ezr 7:24, Neh 9:37, 1Ki 9:21, Jos 16:10
- 5Lev 25:39–43, 2Ki 4:1, Gen 37:27, Isa 58:7, Gen 29:14, Exo 21:1–11, Jas 2:5–6, Mat 18:25
- 6Exo 11:8, Neh 13:25, Eph 4:26, Num 16:15, Mrk 3:5, Neh 13:8
- 7Lev 25:36, Deu 23:19–20, Exo 22:25, Ezk 22:12, 2Ch 19:6–7, Deu 24:10–13, Psa 15:5, Deu 15:2–3
- 8Lev 25:47–49, 1Co 8:11, Exo 21:16, 2Co 8:12, Job 32:15, Mat 25:29, Rom 3:19, Rom 14:15
- 9Lev 25:36, 2Sa 12:14, 1Pe 2:12, Pro 18:5, Rom 2:24, Tit 2:5, Act 9:31, Gen 13:7–8
- 102Co 6:1, Exo 22:25–27, Phm 1:8–9, 2Co 5:11, 2Co 5:20, Ezk 18:8, Luk 3:13–14, Ezk 18:13
- 11Isa 58:6, Lev 6:4–5, Neh 5:3–4, 2Sa 12:6, 1Sa 12:3, Luk 3:8
- 12Ezr 10:5, Jer 34:8–10, 2Ch 6:22–23, 2Ch 28:14–15, Neh 13:25, Neh 10:29, Ezr 10:12, Luk 19:8
- 13Act 18:6, Mat 10:14, 1Ch 16:36, Zec 5:3–4, 1Sa 15:28, Num 5:22, Deu 27:14–26, Act 13:51
- 14Neh 13:6, 1Co 9:18, 2Th 3:8–9, 1Co 9:4–15, Neh 2:1, Ezr 4:13–14, Rom 13:6–7
- 15Neh 5:9, Isa 50:10, Pro 16:6, 2Co 11:9, Mat 5:47, Ecc 12:13–14, Job 31:23, Pro 29:12
- 16Gal 6:9, 1Th 2:5–6, Act 20:33–35, Php 2:20–21, 1Co 15:58, Luk 8:15, Num 16:15, 2Co 12:16–18
- 171Ki 18:19, 1Pe 4:9–10, 2Sa 9:7, Isa 32:8, 2Sa 9:13, Rom 12:13
- 181Ki 4:22–23, Psa 37:21, Psa 37:26, Neh 5:14–15
- 19Neh 13:31, Psa 106:4, Neh 13:14, Neh 13:22, Psa 25:6–7, Jer 29:11, Mrk 9:41, Psa 18:23–25
Mga paksa sa kabanatang ito
46
Amen, Artaxerxes, Beneficence, Borrowing, Brother, Children, Civil Service, Conscience, Consistency, Country, Covetousness, Creditor, Debt, Debtor, Example, Fear, Government, Homestead, House, Inconsistency, Influence, Integrity, Interest, Israel, Prophecies Concerning, Jerusalem, Kindness, Land, Lending, Lock, Love, Money, Mortgage, Nehemiah, Oath, Persia, Poor, Prayer, Repentance, Reproof, Rich, the, Rulers, Servant, Tax, Unselfishness, Usury, Works