1 Wafalme 19
1 Ahabu akamwambia Yezebeli kila kitu Ilya alichokuwa amefanya na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
2 Hivyo Yezebeli akamtuma mjumbe kwa Ilya, kusema, “Miungu waniadhibu vikali zaidi, ikiwa kesho wakati kama huu sitakuwa nimeondoa uhai wako kama mmoja wa hao manabii.”
3 Ilya aliogopa, na akatoroka kuokoa maisha yake. Alipofika Beer-Sheba katika Yuda, akamwacha mtumishi wake huko,
4 lakini yeye mwenyewe akatembea mwendo wa kutwa nzima katika jangwa. Akafika kwenye mti wa mretemu, akakaa chini yake na kuomba ili afe. Akasema, “Yatosha sasa, Mwenyezi Mungu, ondoa roho yangu, kwani mimi si bora kuliko baba zangu.”
5 Kisha akajinyoosha chini ya mti, akalala usingizi. Mara malaika akamgusa na kumwambia, “Inuka ule.”
6 Akatazama pande zote, na hapo karibu na kichwa chake palikuwa na mkate uliookwa kwenye makaa ya moto, na gudulia la maji. Akala na kunywa, kisha akajinyoosha tena.
7 Yule malaika wa Mwenyezi Mungu akaja tena mara ya pili, akamgusa na kumwambia, “Inuka ule, kwa kuwa bado una safari ndefu mbele yako.”
8 Kwa hiyo akainuka, akala na kunywa. Akiwa ametiwa nguvu na kile chakula, akasafiri siku arobaini usiku na mchana hadi akafika Horebu, mlima wa Mungu.
9 Huko akaingia katika pango, akalala humo usiku ule. Mwenyezi Mungu amtokea Ilya Nalo neno la Mwenyezi Mungu likamjia, kusema, “Unafanya nini hapa, Ilya?”
10 Akajibu, “Nimekuwa nikifanya bidii sana kwa ajili ya Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni. Waisraeli wamelikataa agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi peke yangu niliyebaki, sasa wananitafuta ili waniue pia.”
11 Mwenyezi Mungu akasema, “Toka nje ukasimame juu ya mlima mbele za Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Mwenyezi Mungu yu karibu kupita hapo.” Kisha upepo mzito na wenye nguvu ukapasua milima ile na kuvunjavunja miamba mbele za Mwenyezi Mungu, lakini Mwenyezi Mungu hakuwamo katika ule upepo. Baada ya upepo palikuwa na tetemeko la ardhi, lakini Mwenyezi Mungu hakuwamo kwenye lile tetemeko.
12 Baada ya tetemeko la ardhi moto ukaja, lakini Mwenyezi Mungu hakuwamo katika ule moto. Baada ya moto ikaja sauti ya utulivu ya kunong’ona.
13 Ilya alipoisikia, akafunika uso kwa vazi lake, akatoka na kusimama kwenye mlango wa pango. Kisha ile sauti ikamwambia, “Ilya, unafanya nini hapa?”
14 Akajibu, “Nimekuwa nikifanya bidii sana kwa ajili ya Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni. Waisraeli wamelikataa agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi peke yangu niliyebaki, sasa wananitafuta ili waniue pia.”
15 Mwenyezi Mungu akamwambia, “Rudi kwa njia uliyoijia, uende kwenye Jangwa la Dameski. Utakapofika huko, mpake Hazaeli mafuta awe mfalme wa Aramu.
16 Pia mpake mafuta Yehu, mwana wa Nimshi awe mfalme wa Israeli, na umpake mafuta Al-Yasa mwana wa Shafati kutoka Abel-Mehola awe nabii baada yako.
17 Yehu atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Hazaeli, naye Al-Yasa atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Yehu.
18 Hata sasa nimeweka akiba ya watu elfu saba katika Israeli, wote ambao hawajampigia Baali magoti, na wote ambao midomo yao haijambusu.”
19 Hivyo Ilya akaondoka huko na kumkuta Al-Yasa mwana wa Shafati. Alikuwa akilima kwa jozi kumi na mbili za maksai, na yeye mwenyewe aliiongoza ile jozi ya kumi na mbili. Ilya akamwendea, na kumvisha vazi lake.
20 Kisha Al-Yasa akawaacha maksai wake, akamkimbilia Ilya, akamwambia, “Niruhusu nikawabusu baba yangu na mama yangu, halafu nitafuatana nawe.” Ilya akajibu, “Rudi zako, kwani nimekufanya nini?”
21 Basi Al-Yasa akamwacha Ilya, naye akarudi. Akachukua ile jozi yake ya maksai na kuwachinja. Akaipika ile nyama kwa kutumia miti ya nira kama kuni na kuwapa watu, nao wakala. Kisha akaondoka, akamfuata Ilya, akamtumikia.
Mga kaugnay na talata
154
- 11Ki 18:40, 1Ki 21:5–7, 1Ki 21:25, 1Ki 16:31
- 21Ki 20:10, Rut 1:17, 2Ki 6:31, Exo 10:28, Dan 3:15, Pro 27:1, 1Ki 2:28, 2Ki 19:10–12
- 3Gen 21:31, Mat 26:56, Mat 26:70–74, 2Co 12:7, Gen 12:12–13, 1Sa 27:1, Amo 7:12–13, Isa 51:12–13
- 4Jon 4:3, Num 11:15, Jon 4:8, Jer 20:14–18, Php 1:21–24, Rom 3:9, Mat 6:26, Nam 3:8
- 5Psa 34:7, Heb 13:5, Act 12:7, Psa 34:10, Heb 1:14, Dan 10:9–10, Dan 9:21, Gen 28:11–15
- 61Ki 17:6, Mat 4:11, Jhn 21:9, Isa 33:16, Psa 37:3, Mat 6:32, Jhn 21:5, 1Ki 17:9–15
- 8Deu 9:18, Exo 34:28, Exo 3:1, Exo 24:18, Mat 4:2, Luk 4:2, 2Co 12:9, Mrk 1:13
- 9Gen 3:9, Gen 16:8, 1Ki 19:13, Exo 33:21–22, Jer 2:18, Heb 11:38, Jer 9:2, Jon 1:3–4
- 101Ki 18:4, Exo 34:14, 1Ki 18:22, Rom 11:2–4, Exo 20:5, 1Ki 18:30, Num 25:13, Num 25:11
- 11Ezk 1:4, Psa 50:3, Job 38:1, Isa 30:30, Heb 12:26, Exo 19:20, Psa 68:8, Rev 11:19
- 12Job 4:16, Zec 4:6, Deu 4:33, Exo 34:6, Job 33:7, Deu 4:11–12, Gen 15:17, Exo 3:2
- 131Ki 19:9, Gen 16:8, Isa 6:5, 1Ki 18:42, Exo 33:23, Jhn 21:15–17, Isa 6:2, Exo 3:5–6
- 14Isa 1:4, 1Ki 19:9–10, Isa 62:1, Deu 31:20, Hos 6:7, Dan 11:30, Jer 22:9, Heb 8:9
- 15Isa 45:1, Jer 1:10, 2Ki 8:7–15, 2Ki 9:14, Gen 14:15, 2Ki 8:28, Jer 27:2–22, Amo 1:4
- 162Ki 9:1–14, 1Ki 19:19–21, 2Ki 2:9, 2Ki 2:15, Jdg 7:22, 1Ki 4:12, Luk 4:27
- 172Ki 13:22, 2Ki 13:3, 2Ki 8:12, Hos 6:5, 2Ki 10:32, Jer 1:10, Isa 11:4, 2Ki 2:23–24
- 18Rom 11:4–5, Isa 1:9, Isa 10:20–22, Hos 13:2, Psa 2:12, Php 2:10, Exo 20:5, Job 31:27
- 192Ki 2:8, 2Ki 2:13–14, 1Sa 28:14, Psa 78:70–72, Mat 4:18–19, Exo 3:1, 1Ki 19:13, Zec 13:5
- 20Luk 9:61–62, Mat 8:21–22, Act 20:37, Mat 4:20, Mat 9:9, Mat 19:27, Mat 4:22
- 212Sa 24:22, Phm 1:13, Exo 24:13, Luk 5:28–29, 2Ti 4:11, 2Ki 3:11, 1Ki 18:43, Num 27:18–20
Mga paksa sa kabanatang ito
54
Abel-Meholah, Agriculture, Angel (Holy Trinity), Angel (A Spirit), Anointing, Baal, Beer-Sheba, Blessing, Bread, Bullock, Cave, Damascus, Day, Death, Decision, Despondency, Doubting, Dress, Earthquakes, Elijah, Elisha, Excuses, Faithfulness, Fasting, Forty, God, Hazael, Horeb, Idolatry, Jehu, Jezebel, Juniper, King, Liberality, Life, Malice, Mantle, Minister, Christian, Miracles, Mother, Murmuring, Obedience, Persecution, Plow, Procrastination, Prophets, Prudence, Quotations and Allusions, Revenge, Shaphat, Symbols and Similitudes, Trouble, Women, Zeal, Religious