1 Wafalme 13
1 Kwa neno la Mwenyezi Mungu, mtu wa Mungu alifika Betheli kutoka Yuda wakati Yeroboamu alipokuwa amesimama kando ya madhabahu ili kutoa sadaka.
2 Akapiga kelele dhidi ya madhabahu kwa neno la Mwenyezi Mungu: “Ee madhabahu, ee madhabahu! Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi Mungu: ‘Mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika nyumba ya Daudi. Juu yako atawatoa dhabihu makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia ambao hutoa sadaka hapa, nayo mifupa ya wanadamu itateketezwa juu yako.’ ”
3 Siku hiyo hiyo, mtu wa Mungu akatoa ishara: “Hii ndiyo ishara Mwenyezi Mungu aliyotangaza: Madhabahu haya yatapasuka na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.”
4 Mfalme Yeroboamu aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, alipopiga kelele dhidi ya madhabahu huko Betheli, akanyoosha mkono wake kutoka madhabahuni na kusema, “Mkamateni!” Lakini mkono aliounyoosha kumwelekea yule mtu ukakauka kiasi kwamba hakuweza kuurudisha.
5 Pia, madhabahu yakapasuka na majivu yakamwagika, sawasawa na ishara iliyotolewa na mtu wa Mungu kwa neno la Mwenyezi Mungu.
6 Kisha mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “Niombee kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wako, ili mkono wangu upate kupona.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwombea kwa Mwenyezi Mungu, nao mkono wa mfalme ukapona na kurudi ulivyokuwa hapo awali.
7 Mfalme akamwambia yule mtu wa Mungu, “Twende nyumbani mwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
8 Lakini yule mtu wa Mungu akamjibu mfalme, “Hata kama ungenipa nusu ya mali yako, nisingeenda pamoja nawe, wala nisingekula mkate au kunywa maji hapa.
9 Kwa kuwa niliagizwa kwa neno la Mwenyezi Mungu: ‘Kamwe usile mkate wala usinywe maji au kurudi kwa njia uliyojia.’ ”
10 Hivyo, akafuata njia nyingine na hakurudi kupitia njia aliyokuwa ameijia Betheli.
11 Basi kulikuwa na nabii fulani mzee aliyekuwa anaishi Betheli, ambaye wanawe walikuja kumwambia yote ambayo mtu wa Mungu alikuwa ameyafanya pale siku ile. Pia wakamwambia baba yao yale aliyomwambia mfalme.
12 Baba yao akawauliza, “Ameelekea njia gani?” Nao wanawe wakamwonesha ile njia yule mtu wa Mungu kutoka Yuda aliyopita.
13 Hivyo akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda.” Walipokwisha kumtandikia punda, akampanda
14 na kumfuatilia yule mtu wa Mungu. Akamkuta ameketi chini ya mwaloni na kumuuliza, “Je, wewe ndiwe mtu wa Mungu kutoka Yuda?” Akamjibu, “Mimi ndiye.”
15 Basi nabii akamwambia, “Karibu nyumbani pamoja na mimi, ule.”
16 Yule mtu wa Mungu akasema, “Siwezi kurudi na kwenda nawe, wala siwezi kula mkate au kunywa maji pamoja nawe mahali hapa.
17 Nimeambiwa kwa neno la Mwenyezi Mungu: ‘Kamwe usile mkate au kunywa maji huko au kurudia njia uliyojia.’ ”
18 Yule nabii mzee akajibu, “Mimi pia ni nabii, kama wewe. Naye malaika alisema nami kwa neno la Mwenyezi Mungu: ‘Mrudishe aje katika nyumba yako ili apate kula mkate na kunywa maji.’ ” (Lakini alikuwa akimwambia uongo.)
19 Hivyo mtu wa Mungu akarudi pamoja naye na akala na kunywa katika nyumba yake.
20 Walipokuwa wameketi mezani, neno la Mwenyezi Mungu likamjia yule nabii mzee aliyemrudisha huyo mtu wa Mungu.
21 Akampazia sauti yule mtu wa Mungu aliyekuwa ametoka Yuda, “Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi Mungu: ‘Umeasi neno la Mwenyezi Mungu na hukushika amri uliyopewa na Mwenyezi Mungu, Mungu wako.
22 Ulirudi, ukala mkate na kunywa maji mahali alipokuambia usile wala usinywe. Kwa hiyo maiti yako haitazikwa katika kaburi la baba zako.’ ”
23 Huyo mtu wa Mungu alipomaliza kula na kunywa, nabii aliyekuwa amemrudisha akamtandikia punda wake.
24 Alipokuwa akienda akakutana na simba njiani, akamuua na maiti yake ikabwagwa barabarani, huku punda wake na simba wakiwa wamesimama kando yake.
25 Watu waliopita pale, waliona maiti iliyokuwa imebwagwa, simba akiwa amesimama kando yake. Nao wakaenda kutoa habari katika mji ambao nabii mzee alikuwa anaishi.
26 Yule nabii aliyekuwa amemrudisha kutoka safari yake aliposikia habari hii akasema, “Ni yule mtu wa Mungu aliyeliasi neno la Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu amemtoa kwa simba, ambaye amemrarua na kumuua, sawasawa na neno la Mwenyezi Mungu lilivyokuwa limemwonya.”
27 Nabii akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda,” nao wakafanya hivyo.
28 Akaondoka na akakuta maiti imetupwa barabarani, punda na simba wakiwa wamesimama kando yake. Simba hakuwa amekula ile maiti wala kumrarua punda.
29 Basi yule nabii mzee akachukua maiti ya mtu wa Mungu, akailaza juu ya punda na akairudisha katika mji wake, ili amwombolezee na kumzika.
30 Kisha akailaza ile maiti katika kaburi lake huyo nabii mzee, nao wakaomboleza juu yake na kusema, “Ee ndugu yangu!”
31 Baada ya kumzika, akawaambia wanawe, “Nitakapokufa, mnizike kwenye kaburi alimozikwa huyu mtu wa Mungu; lazeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.
32 Kwa maana ujumbe alioutangaza kwa neno la Mwenyezi Mungu dhidi ya madhabahu huko Betheli, na dhidi ya nyumba zote za ibada katika mahali pa juu pa kuabudia ndani ya miji ya Samaria, hakika utatimia.”
33 Hata baada ya haya, Yeroboamu hakubadili njia zake mbaya, lakini mara nyingine tena akaweka makuhani kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia kutoka watu wa aina zote. Yeyote aliyetaka kuwa kuhani alimweka wakfu kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia.
34 Hii ilikuwa ndiyo dhambi ya nyumba ya Yeroboamu ambayo iliisababishia kuanguka na kuangamia kwake hadi kutoweka kwenye uso wa dunia.
Mga kaugnay na talata
191
- 12Ki 23:17, 1Ki 12:32–33, 1Th 4:15, Jer 25:3, Jer 32:29, Jer 11:12, Num 16:40, 1Ki 13:5
- 22Ki 23:15–18, Ezk 36:1, 2Ki 22:1–2, Jer 22:29, Isa 42:9, Luk 19:40, 2Ch 34:4–7, 1Ki 13:32
- 31Co 1:22, Exo 4:3–5, Jdg 6:17, Jhn 2:18, Isa 38:6–8, Isa 38:22, Exo 7:10, Exo 4:8–9
- 4Rev 11:5, 2Ch 18:25–27, Luk 3:19–20, 2Ch 16:10, 2Ch 25:15–16, 2Ki 6:18–20, Gen 19:11, Jer 26:8–11
- 5Act 5:1–10, Mrk 16:20, Num 16:23–35, 1Ki 13:3, 1Ki 22:28, 1Ki 22:35, Exo 9:18–25, Deu 18:22
- 6Exo 10:17, Exo 8:8, Exo 9:28, Act 8:24, Luk 6:27–28, Num 21:7, Exo 8:28, Jer 37:3
- 72Ki 5:15, 1Sa 9:7–8, Jer 40:5, Jdg 19:21, Jdg 13:15, 1Pe 5:2, Mal 1:10, Act 8:18–20
- 8Num 24:13, Num 22:18, 2Ki 5:16, 1Ki 13:16–17, Mrk 6:23, Exo 7:2, 2Co 11:9–10, Exo 5:3
- 9Jhn 15:9–10, Jhn 13:17, Rom 16:17, Jhn 15:14, Job 23:12, 1Ki 13:21–22, 1Ki 13:1, Deu 13:13–18
- 112Ki 23:18, 2Pe 2:16, Num 23:4–5, 1Ki 13:20–21, 1Sa 10:11, Num 24:2, 1Ti 3:5, Mat 7:22
- 132Sa 19:26, Num 22:21, 1Ki 13:27, Jdg 5:10, Jdg 10:4
- 142Co 11:27, 1Ki 19:4, Php 4:12–13, Jhn 4:34, 1Co 4:11–12, Jhn 4:6
- 161Ki 13:8–9, Mat 16:23, Num 22:13, Mat 4:10, Num 22:19, Gen 3:1–3
- 171Ki 20:35, 1Th 4:15, 1Ki 13:1
- 181Jn 4:1, Mat 7:15, Num 22:35, Jer 28:15–16, 2Co 11:13–15, 2Pe 2:1, Jer 23:32, Rom 16:18
- 19Deu 13:1, Deu 18:20, Act 4:19, Deu 13:5, 2Pe 2:18–19, Deu 13:3, 1Ki 13:9, Gen 3:6
- 201Co 13:2, Num 24:4, Num 23:16, Jhn 11:51, Mat 7:22, Num 24:16–24, Num 23:5
- 211Sa 15:22–24, 1Sa 13:13–14, Gal 1:8–9, 1Sa 15:19, Gen 3:7, Lev 10:3, 2Sa 24:13, Rev 3:19
- 221Ki 13:30, 2Ch 21:19–20, Jer 22:18–19, Isa 14:18–20, 1Ki 14:13
- 241Ki 20:36, 2Ki 2:24, 1Pe 4:17–18, Amo 5:19, Pro 22:13, Pro 26:13, 1Co 11:31–32
- 251Ki 13:11
- 26Ezk 9:6, Lev 10:3, Heb 12:28–29, 1Co 11:30, Psa 119:120, 2Sa 12:10, 2Sa 12:14, Pro 11:31
- 28Job 38:11, Dan 6:22–24, Act 16:26, 1Ki 17:6, Jer 5:22–23, 1Ki 17:4, Psa 148:7–8, Dan 3:22
- 30Jer 22:18, Act 8:2, 1Ki 14:13
- 312Ki 23:17–18, Psa 26:9, Num 23:10, Luk 16:22–23, Ecc 8:10
- 321Ki 16:24, 1Ki 13:2, Lev 26:30, 1Ki 12:31, 2Ki 23:16–19, 1Ki 12:29, 2Ch 25:13, Ezr 4:10
- 332Ch 11:15, 2Ch 13:9, Num 17:5, 2Ti 3:13, Amo 6:11, Jer 18:4, Num 17:12–13, Num 1:51
- 341Ki 12:30, 1Ki 15:29–30, 1Ki 14:10, 2Ki 17:21, 2Ki 10:31, 1Ki 12:26, Pro 13:6
Mga paksa sa kabanatang ito
29
Afflictions and Adversities, Beth-El, Brother, Calf, Conscience, Deception, Decision, Disobedience to God, Falsehood, Fellowship, Forgiveness, Intercession, Jeroboam, Josiah, Judgments, Lion, Minister, Christian, Miracles, Presumption, Priest, Prophecy, Prophets, Reproof, Rulers, Sheba, Sign, Sin, Symbols and Similitudes, Temptation