1 Mambo Ya Nyakati 26
1 Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
2 Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
3 Elamu wa tano, Yehohanani wa sita, na Eliehoenai wa saba.
4 Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
6 Shemaya mwanawe Obed-Edomu pia alikuwa na wana waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao, kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
7 Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
8 Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
9 Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
10 Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu, ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
11 Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne.
12 Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Mwenyezi Mungu kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
13 Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
14 Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe Shelemia, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
15 Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
16 Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa.
17 Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
18 Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
19 Hii ilikuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
20 Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
21 Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
22 wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Mwenyezi Mungu.
23 Kutoka kwa Waamrami, Waishari, Wahebroni na Wauzieli:
24 Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Musa, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
25 Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
26 Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
27 Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Mwenyezi Mungu.
28 Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
29 Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
30 Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu elfu moja na mia saba wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi mwa Yordani kwa ajili ya kazi zote za Mwenyezi Mungu na utumishi wa mfalme.
31 Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi, uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
32 Yeria alikuwa na jamaa ya watu elfu mbili mia saba waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.
Cross-references
101
- 12Ch 23:19, 1Ch 9:17–27, Psa 44:1, 1Ch 15:18, 1Ch 15:23–24, 1Ch 6:37, Psa 49:1, Num 26:9–11
- 21Ch 9:21
- 41Ch 15:24, 1Ch 16:38, 1Ch 15:18, 1Ch 15:21, 1Ch 16:5
- 5Psa 128:1
- 61Ch 12:28, 2Sa 2:7, 1Ch 26:8, 2Ti 2:3, Jdg 6:12, 2Ch 26:17, 1Ti 6:12, Neh 11:14
- 82Co 3:6, Mat 25:15, 1Pe 4:11, 1Co 12:4–11
- 91Ch 26:14, 1Ch 26:1
- 101Ch 16:38, 1Ch 5:1–2
- 121Ch 25:8
- 131Ch 24:31, 1Ch 25:8, 1Ch 24:5
- 152Ch 25:24, 1Ch 26:17
- 16Neh 12:24, 2Ch 9:4, 1Ch 26:10–12, 1Ki 10:5, 1Ch 25:8
- 172Ch 8:14, 1Ch 9:24
- 182Ki 23:11
- 19Num 16:11
- 201Ch 26:22, 1Ch 28:12–19, 1Ki 14:26, 1Ch 9:26–30, 1Ch 29:2–8, 1Ch 22:3–4, Mal 3:10, 1Ki 15:18
- 211Ch 23:7, 1Ch 6:17, 1Ch 29:8
- 221Ch 23:8, Neh 10:38, 1Ch 29:8, 1Ch 26:20
- 231Ch 23:12, Num 3:27, Num 3:19
- 241Ch 24:20, 1Ch 23:15–16
- 251Ch 23:17–18, Exo 18:4, 1Ch 23:15
- 262Sa 8:11, 1Ch 18:11, 1Ch 29:2–9, Num 31:30–52, 1Ch 22:14
- 27Neh 10:32–34, 2Ki 12:14, Jos 6:19
- 281Sa 9:9, 1Sa 17:55, 2Sa 10:9–14, 1Sa 14:47–51
- 291Ch 23:4, Neh 11:16, 1Ch 26:23, 2Ch 34:13, 2Ch 19:8–11, 1Ch 23:12
- 301Ch 27:17, 1Ch 23:19, 1Ch 23:12
- 311Ch 23:19, Jos 21:39, Isa 16:9, 1Ki 2:11, 1Ch 6:81, 1Ch 29:27
- 322Ch 19:11, 1Ch 23:24, 1Ch 12:37, 1Ch 24:31, 1Ch 15:12
Topics in this chapter
67
Abner, Ahijah, Ammiel, Amram, Asaph, Asuppim, Birthright, Chenaniah, Church, Court, Dedication, Ebiasaph, Elam, Elihoenai, Elihu, Elzabad, Firstborn, Gershom, Hashabiah, Hilkiah, Hosah, Jathniel, Jediael, Jehieli, Jehohanan, Jehozabad, Jeriah, Jerusalem, Jesaiah, Joab, Joah, Joel, King, Kore, Laadan, Levites, Liberality, Lot, the, Meshelemiah, Nethaneel, Obed, Obed-Edom, Othni, Peulthai, Porters, Rehabiah, Rephael, Sacar, Samuel, Saul, Semachiah, Shallecheth, Shebuel, Shelemiah, Shelomith, Shemaiah, Shimri, Shuppim, Simri, Spoils, Tebaliah, Treasure-Houses, Worship, Zebadiah, Zechariah (Zecharias), Zetham, Zichri