Nehemia 8
1 watu wote wakakusanyika kama mtu mmoja kwenye uwanja mbele ya Lango la Maji. Wakamwambia Ezra mwandishi alete Kitabu cha Torati ya Musa, ambacho Mwenyezi Mungu aliamuru kwa ajili ya Israeli.
2 Basi katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba, kuhani Ezra akaleta Torati mbele ya kusanyiko, ambamo walikuwamo wanaume, wanawake na watu wote walioweza kufahamu.
3 Akaisoma kwa sauti kubwa tangu mapambazuko hadi adhuhuri, akiwa ameuelekea uwanja uliokuwa mbele ya Lango la Maji mbele ya wanaume, wanawake na wengine ambao waliweza kufahamu. Watu wote wakasikiliza kwa makini kile Kitabu cha Torati.
4 Mwandishi Ezra alikuwa amesimama juu ya jukwaa la miti lililojengwa kwa kusudi hilo. Karibu naye upande wa kuume walisimama Matithia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia na Maaseya. Upande wake wa kushoto walikuwa Pedaya, Mishaeli, Malkiya, Hashumu, Hashbadani, Zekaria na Meshulamu.
5 Ezra akakifungua kile kitabu. Watu wote waliweza kumwona kwa sababu alikuwa amesimama juu zaidi, naye alipokifungua watu wote wakasimama.
6 Ezra akamsifu Mwenyezi Mungu, Mungu mkuu, nao watu wote wakainua mikono yao na kuitikia, “Amen! Amen!” Kisha wakasujudu na kumwabudu Mwenyezi Mungu, nyuso zao zikigusa chini.
7 Watu wakiwa wamesimama pale, Walawi wafuatao waliwafundisha ile Torati: Yeshua, Bani, Sherebia, Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya.
8 Walisoma kutoka kile Kitabu cha Torati ya Mungu, wakiifafanua na kuwapa maelezo ili watu waweze kufahamu kile kilichokuwa kikisomwa.
9 Ndipo Nehemia aliyekuwa mtawala, Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliokuwa wakiwafundisha watu wakawaambia wote, “Siku hii ni takatifu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Msiomboleze wala msilie.” Kwa kuwa watu wote walikuwa wakilia walipokuwa wakisikiliza maneno ya ile Torati.
10 Nehemia akasema, “Nendeni mkafurahie chakula kizuri na vinywaji vitamu, na mpeleke sehemu kwa wale ambao hawana chochote cha kula. Siku hii ni takatifu kwa Mwenyezi Mungu. Msihuzunike, kwa kuwa furaha ya Mwenyezi Mungu ni nguvu zenu.”
11 Walawi wakawatuliza watu wote wakisema, “Kuweni watulivu, kwa kuwa hii ni siku takatifu. Msihuzunike.”
12 Kisha watu wote wakaondoka kwenda kula na kunywa, na kupeana sehemu ya chakula, na wakaadhimisha kwa furaha kubwa, kwa sababu sasa walifahamu maneno yale waliyokuwa wameelezwa.
13 Katika siku ya pili ya mwezi, wakuu wa jamaa zote, pamoja na makuhani na Walawi, walikusanyika wakimzunguka Ezra mwandishi ili wapate kusikiliza kwa makini maneno ya Torati.
14 Wakakuta imeandikwa katika ile Torati, ambayo Mwenyezi Mungu aliiamuru kupitia kwa Musa, kwamba Waisraeli walipaswa kukaa katika vibanda wakati wa sikukuu ya mwezi wa saba,
15 na kwamba walipaswa kutangaza neno hili na kulieneza katika miji yao na katika Yerusalemu wakisema: “Nendeni katika nchi ya vilima na kuleta matawi kutoka miti ya mizeituni, mizeituni mwitu, mihadasi, mitende na miti ya kivuli, ili kutengeneza vibanda,” kama ilivyoandikwa.
16 Basi watu wakaenda na kuleta matawi, nao wakajijengea vibanda juu ya paa za nyumba zao, katika nyua zao, katika nyua za nyumba ya Mungu, na katika uwanja karibu na Lango la Maji, na uwanja wa Lango la Efraimu.
17 Jamii yote ya watu waliorudi kutoka utumwani wakajenga vibanda na kuishi ndani yake. Tangu wakati wa Yoshua mwana wa Nuni hadi siku ile, Waisraeli hawakuwahi kuiadhimisha namna hii. Furaha yao ilikuwa kubwa sana.
18 Siku baada ya siku, kuanzia siku ya kwanza hadi ya mwisho, Ezra alisoma katika kile Kitabu cha Torati ya Mungu. Wakaiadhimisha sikukuu ile kwa siku saba, nayo siku ya nane, kufuatana na maagizo, kulikuwa na kusanyiko maalum.
Перекрёстные ссылки
126
- 1Ezr 7:6, 2Ch 34:15, Neh 3:26, Mat 13:52, Ezr 3:1–13, Ezr 7:11, Neh 8:16, Mat 23:13
- 2Lev 23:24, Mal 2:7, Num 29:1, Deu 31:9–13, Deu 17:18, Act 15:21, Isa 28:9, 2Ch 17:7–9
- 3Rev 3:22, Heb 2:1–3, Rev 2:29, Luk 4:16–20, 1Th 2:13, Luk 8:18, Act 16:14, Act 15:21
- 4Ezr 10:33, Neh 11:5, Neh 10:25, Neh 11:7, Neh 10:20, Neh 10:3, Ezr 10:29, Neh 12:13
- 5Jdg 3:20, 1Ki 8:14, Luk 4:16–17
- 61Ti 2:8, Lam 3:41, Exo 4:31, 2Ch 20:18, Rev 7:11, Gen 24:26, Psa 134:2, Neh 5:13
- 7Neh 9:4, Lev 10:11, Neh 3:23, Ezr 10:22–23, Mal 2:7, Neh 12:33, Neh 10:2, 2Ch 30:22
- 8Luk 24:45, Act 28:23, Act 17:2–3, Luk 24:32, Luk 24:27, Act 8:30–35, Hab 2:2, Mat 5:27–28
- 9Neh 7:70, Neh 7:65, Deu 12:12, Deu 16:11, Neh 8:2, Isa 61:3, Deu 12:7, Ezr 2:63
- 10Psa 28:7–8, Pro 17:22, 2Co 12:8–9, Ecc 9:7, Isa 12:1–3, Isa 61:10, Psa 149:2, Est 9:19
- 11Num 13:30
- 12Psa 119:174, Psa 119:127, Psa 119:130, Psa 119:111, Psa 119:72, Luk 24:32, Psa 119:97, Neh 8:7–8
- 13Pro 12:1, Pro 2:1–6, Pro 8:33–34, Luk 24:32, Act 4:1, Luk 19:47–48, Neh 8:7–8, Mrk 6:33–34
- 14Lev 23:34, Lev 23:40–43, Deu 16:13–15, Zec 14:16–19, Jhn 7:2, Gen 33:17
- 15Lev 23:40, Deu 16:16, Lev 23:4, Gen 8:11, Jdg 9:48–49, Mat 21:1, Jhn 12:13, Rev 7:9
- 162Ki 14:13, Neh 12:39, Neh 12:37, Neh 3:26, Jer 32:29, Neh 8:3, Jer 19:13, 2Ch 33:5
- 172Ch 8:13, 2Ch 7:8–10, Ezr 3:4, Heb 11:13, 2Ch 30:21–23, 2Ch 35:18, 1Ch 29:22, Heb 4:8
- 18Num 29:35, Lev 23:36, Deu 31:10–13, Jhn 7:37
Темы в этой главе
60
Akkub, Amen, Anaiah, Ananiah, Bani, Beneficence, Blessing, Booth, Children, Commandments, Ephraim, Ezra, Feasts, Gates, Hanan, Hashbadana, Hashum, Hilkiah, Hodiah, House, Instruction, Interpreter, Israel, Prophecies Concerning, Jamin, Jerusalem, Jeshua, Joy, Jozabad, Kelaiah, Law, Levites, Maaseiah, Malchiah, Mattithiah, Meshullam, Mishael, Month, Myrtle, Nehemiah, Olive, Pedaiah, Pelaiah, Pine, Poor, Priest, Pulpit, Repentance, Sabbatic Year, Shabbethai, Shema, Sherebiah, Synagogue, Tabernacles, Feast of, Tirshatha, Trumpets, Urijah, Word of God, Worship, Zeal, Religious, Zechariah (Zecharias)